Baada ya Vyuo kuendelea kufungwa nimeamua kufungua kioski home

Kama upo eneo ambalo ni mjini sana lazima watakufata tu. Lakini masuala ya TRA inategemea na kipato chako kwa maana hii: kwa sasa watakuacha ufanye biashara kwa kipindi fulani(mara nyingi miezi sita/sababu ndio unaanza) baadaye ndio watafuatilia/kuuliza mauzo yako ya siku ni kiasi gani ili wakukadirie(hapa kuwa makini maana unaweza ukalipa gharama kubwa ukiingia vibaya).
Vitu vya muhimu ni TIN namba na leseni ya biashara.
Lakini pia kama ni mtaji mdogo kabisa tumia kile kitambulisho cha mjasiriamali(20,000) ingawa sijui kama bado vinakubalika.

Wengine wataongezea
Hongera kwa kujiongeza.Kila la kheri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shukrani Sana Mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…