Kama upo eneo ambalo ni mjini sana lazima watakufata tu. Lakini masuala ya TRA inategemea na kipato chako kwa maana hii: kwa sasa watakuacha ufanye biashara kwa kipindi fulani(mara nyingi miezi sita/sababu ndio unaanza) baadaye ndio watafuatilia/kuuliza mauzo yako ya siku ni kiasi gani ili wakukadirie(hapa kuwa makini maana unaweza ukalipa gharama kubwa ukiingia vibaya).
Vitu vya muhimu ni TIN namba na leseni ya biashara.
Lakini pia kama ni mtaji mdogo kabisa tumia kile kitambulisho cha mjasiriamali(20,000) ingawa sijui kama bado vinakubalika.
Wengine wataongezea
Hongera kwa kujiongeza.Kila la kheri
Sent using
Jamii Forums mobile app