Baada ya Waziri Mkuu kujiuzulu akiwa madarakani, sasa huenda ikawa ni zamu ya Makamu wa Rais alie madarakani

Baada ya Waziri Mkuu kujiuzulu akiwa madarakani, sasa huenda ikawa ni zamu ya Makamu wa Rais alie madarakani

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
February 7,2008, aliekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Edward Lowassa, alilazimika kujiuzulu kutokana na kashifa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambayo ilibainika kuwa ilikuwa ni kampuni hewa(kwa mujibu wa kamati ya Mwakyembe wakati huo).

Wakati hayo yakitokea mwaka 2008, leo tumepata Makama wa Rais mpya(mteule) Mhe. Philip Mpango ambae kabla ya uteuzi huo, alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango, wizara inayosimamia taasisi kadha ikiwemo Benki Kuu.

Juzi tarehe 28,wakati akipokea taarifa ya CAG, Rais wa Jamuhuri ya Muungano, Mama Samia Suluhu Hassan, ametoa maagizo kwa CAG kuchunguza fedha za miradi ya maendeleo zilizotolewa Benki Kuu kuanzia mwezi January mwaka huu mpaka mwezi March mwaka huu.

Hivyo, iwapo taarifa ya ukaguzi ya CAG itaibua utata, utata unaoweza kugusa mpaka wizara ya fedha kama msimamizi wa Benki Kuu huku Mpango akiwa ndie alikuwa Waziri, basi yale yaliyotokea mwaka 2008 yanaweza kujirudia hata kama yeye atakuwa hahusiki moja kwa moja.

Ukiacha hili la ukaguzi wa CAG, yako mengine tunayoyasoma humu mitandaoni yanayogusa watendaji wengine waliokuwa chini ya Waziri Mpango, watendaji aliopaswa kuwasimamia.

Kwakuwa wahusika hawakanushi wala kutolea ufafanuzi yanayosemwa, na kwakuwa Waswahili wanatuambia: "lisemwalo lipo na kama halipo laja," basi tuache muda utasema.

Tusubiri.
 
Umepanic sana chief relax.

If you can't fight them join them.

Ni ushauri tu nakupa
 
Lete kwanza ushaidi wa Kakonko alikutwa na 1.6m za kimarekani. Kama huna bora unyamaze uone jinsi Nchi inavyoendeshwa.

Mwanaume kutwa kupiga majungu tu na chuki kwa mwanaume mwenzako.
 
Kabla ya kuteua jina la makamu wa Rais lazima kunafanyika background check ya mambo mengi; inapoonekana mtu Hana makandokando ndipo jina linapendekezwa. Mambo Mengi yaliyohusu fedha enzi za mwendazake , alikuwa anayashuhulikia yeye mwenyewe akishirikiana na Dotto ambae ndio alikuwa PAYMASTER GENERAL. Inasemekana mara nyingi Waziri wa fedha alikuwa bypassed!!! Hivyo usitegee smoking gun itakayomchafua Mpango kutokana na special Audit ya BOT.

Siwezi kumlia yamini GAVANA wa BOT kwa hii AUDIT na matokeo yake! Mwendazake kwa makusudi alimteua mawanasheria kuwa Gavana wa BOT ingawa sheria inapendekeza awe na background ya economics kama walivyokuwa watangulizi wake. Sasa kama madudu yalikuwa yanafanyika na yeye because of ignorance akawa anayapitisha basi he will have to be accountable for his actions; as the lawyers are fond of saying "IGNORANCE IS NO EXCUSE!"
 
Mkuu inashangaza kidogo kwamba tz yenye watu ml 50 hatuna uwezo wa wakupata watu Safi kwa nafasi nyeti mpaka wale wale,baba ,mtoto, mjukuu, hata kitukuu, hii nitabia mbaya Sana na inakela.

Afrika tulisha zikwa, ile kitu mfumo wa kimtandao watutafuna Sana, that's may be mungu hakukosea kutupa ngonzi nyeusi nasema maana Kama mungu mmoja why akatenga ngonzi ,macho,nywele ndefu KWA wengine kuliko sie
 
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Mbungo amethibitisha kumshikilia kwa mahojiano Mkurugenzi Mkuu wa Bandari Tanzania (TPA) Deusdedit Kakoko na kusema baada ya upekuzi nyumbani kwake wamemkuta na USD Elfu 3 na Fedha za Kitanzania Tsh. Milioni 1.5

Mbungo amekanusha kuhusu picha na video zinazosambaa mitandao zikionesha fedha nyingi zinazodaiwa kukutwa nyumbani kwa Injinia Kakoko na kusema hawajakuta rundo la fedha nyingi Kama inavyosambazwa.

"Taarifa za kukutwa na pesa nyingi ambazo picha na video zake zinasambaa sio kweli, sio za kwake sio sahihi ni Watu nadhani ni Maadui zake wanajaribu kutengeza hoja ya kuonesha alikuwa na hizo fedha”- Mbungo

Kukamatwa kwa Kakoko kunakuja kufuatia agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ambaye alimsimamisha kazi na kuagiza achunguzwe.
#MillardAyoUPDATES
 
February 7,2008, aliekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Edward Lowassa, alilazimika kujiuzulu kutokana na kashifa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambayo ilibainika kuwa ilikuwa ni kampuni hewa(kwa mujibu wa kamati ya Mwakyembe wakati huo)...
Kama ilivyokuwa 2015 kwa JPM ,sasa hivi tena Chadema wako bize kumsifia, kumfundisha na kumpa maelekezo mbalimbali Rais Samia bila kujua kuwa huyo ni rais anayetokana na ccm na anatekeleza ilani ya CCM.

Godbless Lema ,Tundu Lisu hawazungumzii kabisa maendeleo ya chadema wao ni bize kumpangia cha kufanya rais Samia.

Tundu Lisu ni kaimu mwenyekiti wa chadema lakini hutakaa usikie akiiongelea wala kuitangaza chadema popote. Kwani haoni kaimu mwenyekiti wa ccm Philip Mangula anavyokinadi chama chake?

Tundu Lisu ni mtanzania lakini hutakaa usikie popote akizungumzia mazuri ya nchi yake ,yeye ni kuchafua tu nchi yake.
 
Kabla ya kuteua jina la makamu wa Rais lazima kunafanyika background check ya mambo mengi; inapoonekana mtu Hana makandokando ndipo jina linapendekezwa. Mambo Mengi yaliyohusu fedha enzi za mwendazake , alikuwa anayashuhulikia yeye mwenyewe akishirikiana na Dotto ambate ndio alikuwa PAYMASTER GENERAL. Inasemekana mara nyingi Waziri wa fedha alikuwa bypassed!!! Hivyo usitegee smoking gun itakayomchafua Mpango kutokana na special Audit ya BOT.
Hata Lowassa alidai shida ilikuwa ni uwaziri mkuu hivyo tafakari sana haya mambo.
 
February 7,2008, aliekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Edward Lowassa, alilazimika kujiuzulu kutokana na kashifa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambayo ilibainika kuwa ilikuwa ni kampuni hewa(kwa mujibu wa kamati ya Mwakyembe wakati huo)...
Huyu bwana bila kukomaa na nyungu ilikuwa amtangulie bwana yule kwenda kuongoza malaika.

Yawezekana kabisa dirisha la ugonjwa wa Mpango likamnusuru akapenya salama.

Yawezekana kabisa kuwa kipindi hicho shamba lilikuwa mali ya bibi proper!

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
February 7,2008, aliekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Edward Lowassa, alilazimika kujiuzulu kutokana na kashifa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambayo ilibainika kuwa ilikuwa ni kampuni hewa(kwa mujibu wa kamati ya Mwakyembe wakati huo)...
Msipoteze muda Majaliwa yupo mno tu.
 
Hata Lowassa alidai shida ilikuwa ni uwaziri mkuu hivyo tafakari sana haya mambo.

Kwani wewe hujui kuwa Lowassa alitoswa na Jakaya Kikwete? Yeye ndio alitaka Lowassa aondoke kutokana na mahesabu yake ya URAIS!! Scenario kama hiyo haiwezi kujirudia, mkwere kila siku ni msanii!!
 
February 7,2008, aliekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Edward Lowassa, alilazimika kujiuzulu kutokana na kashifa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambayo ilibainika kuwa ilikuwa ni kampuni hewa(kwa mujibu wa kamati ya Mwakyembe wakati huo)...
Hili dongo linawagusa moja kwa moja wamiliki wa lile gang
 
Back
Top Bottom