Baadhi ya makosa ambayo enzi zetu ulikuwa ukifanya unagongwa bakora za kukutosha

Baadhi ya makosa ambayo enzi zetu ulikuwa ukifanya unagongwa bakora za kukutosha

Hizi ndio kali zaidi

16. Ukipigwa ukalia unapigwa ili unyamaze.
17. Ukipigwa umenyamaza unapigwa ili ulie.
 
1. Usiposalimia wakubwa asubuhi, unapigwa.
2. Usiposalimia wageni, unapigwa.
3. Ukinawa kabla ya wageni, unapigwa.
4. Ukilia bila sababu, unapigwa.
5. Ukinyanyuka wakati wa kula kabla ya wakubwa kuinuka, unapigwa.
6. Wakubwa wakiwa wamekaa wewe ukaenda kusimana pembeni, unapigwa.
7. Ukikaa wakubwa wamesimama, unapigwa.
8. Ukitumwa dukani ukachelewa kurudi, unapigwa.
9. Ukichelewa kurudi toka shuleni, unapigwa.
10. Ukiwahi kurudi shuleni, unapigwa.
11. Ukililia wageni wakati wanaondoka wakitoka, unapigwa.
12. Kujipitisha pitisha wageni wakiwa wanakula, unapigwa.
13. Kujibu ovyo wakubwa, unapigwa.
14. Kutukana watu wazima, watoto au rika lako, unapigwa.
15. Ukiwa mbishi bila sababu, unapigwa.
16. Ukipigwa ukalia unapigwa ili unyamaze.
17. Ukipigwa umenyamaza unapigwa ili ulie.
18. Ukipigwa shuleni ukaenda kusema nyumbani, unapigwa.
19. Ukianza kula nyama kabla ya wakubwa, unapigwa.
20. Ukila kwa jirani ukabainika, unapigwa.
21: Ukianza kunawisha wenyeji badala ya wageni mkimaliza kula unaitwa chumbani, unapigwa.
22. Ukianza kunawisha watoto badala ya wakubwa, unapigwa.
23. Ukimkuta mtu nzima hujampokea, unapigwa.
24. Ukienda kusema kama umepigwa, unapigwa.
25. Mtu mzima akipita kama mnacheza hamjamshughulikia, unapigwa.
26. Ukienda nyumba za watu, ukaona kitu au ukasikia story ukaileta nyumbani, unapigwa.
27. Ukipewa hela na mtu asiefahamika au hata anaejulikana inategemea mazingira gani, unapigwa.
28. Ukianza kuchaguwa chakula hiki nakula hiki sili, unapigwa.
29. Ukianza kuwa na marafiki wasioleweka makwao, unapigwa.
30. Mtu mkubwa akija kukuchongea nyumbani hata kama sio cha ukweli, unapigwa.
31. Ukikaa na wakubwa halafu ukaanza kucheka bila sababu, unapigwa.
32. Ukimwuliza Baba/ Mama umetoka wapi unapigwa.
33. Ukilala bila kula, unapigwa.
34. Ukiitwa ukaja kimyakimya bila ya kuanza kuitika unapigwa.
35. Endapo umepigwa na ukasusa chakula, unapigwa.
Wahenga njooni tukumbushane matukio mengine
No. 14 siyo tu kupigwa unawekwa kikao cha ukoo kabisa 😂
 
Usipolima kwa spidi shambani siku hiyo hautakula na usipokula utapigwa kwanini haukula

Kama mna mifugo usipoenda machungani utapigwa
 
Nasoma naona kama umeandika yote. Ila watoto wa zamani tulinyooka kitabia. Shuleni kwenyewe ukiwa mtovu wa nidhamu walimu wakakubaini utaishia kuandikwa kwenye kitabu cheusi, black book na ukifaulu huendi sekondari hata kama una akili nyingi. Sasa hivi ukiadhibu mtoto wa mtu kwa utovu wa nidhamu utajikuta matatani huko polisi. Zamani mtoto alikuwa ni wa jamii nzima, sio wa serikali pekee kama ilivyo sasa. Serikali inajifanya kulinda haki za watoto huku ikishindwa kulinda mmomonyoko wa maadili kwa watoto wanakua wakiwa wakubwa na tabia za kishenzi zisizopendeza
 
Back
Top Bottom