Baadhi ya mastaa Yanga hawajaenda Mapinduzi Cup

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
373
Reaction score
829
#MICHEZO Nyota watano wa klabu @yangasc hawatakuwa sehemu ya kikosi ambacho kimeondoka leo chini ya kocha msaidizi Cedric Kaze kuelekea visiwani Zanzibar kushiriki Kombe la Mapinduzi lililoanza Januari Mosi.

Wachezaji hao ni Fiston Mayele, Aziz KI, Kibwana Shomari, Khalid Aucho, Yannick Bangala ambao wamepewa mapumziko. Meneja wa Yanga, Walter Harrison amesema kuwa sababu ya kuwatumia vijana kwenye Kombe la Mapinduzi Cup ni kuwapa uzoefu.

#Mapinduzi
 
Wanataka wakilikosa kombe wapate sababu.
 
Reactions: BRN
Labda Simba wanaogopa wasije wakakosa kabisa kuchukua kombe lolote msimu mzima.
 
Ni maamuzi mazuri ila wasiifanye kama mwaka jana, wakiona kuna mechi dhidi ya Simba au Azam. Wanaanza kuwasaka mitaani kuwasafirisha wachezaji waliokuwa wanakula bata mitaani hata fitness hawana. Watumie hao hao hata wakifungwa magoli saba sawa tu.
 
Watakuja na ndege ya asubuhi wakipigwa na Singida
 
Ni maamuzi mazuri ila wasiifanye kama mwaka jana, wakiona kuna mechi dhidi ya Simba au Azam. Wanaanza kuwasaka mitaani kuwasafirisha wachezaji waliokuwa wanakula bata mitaani hata fitness hawana. Watumie hao hao hata wakifungwa magoli saba sawa tu.
Tuna clement mzize..
 
Msimu uliopita hili ndo lilikuwa kombe pekee wanaloligombania mpaka wakachukua na msimu huu watachezesha wachezaji wake nyota ili watetee ubingwa wao wa mapinduzi cup
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…