Baadhi ya Wabunge wa Bunge la Tanzania lapendekeza makato ya mishahara kupambana na corona virus

Wanaotakiwa kukatwa mishahara ni wabunge maana ndo wanalipwa mishahara na maposho kibao, sijui milioni kumi na ngapi kwa mwezi. Watumishi wa umma asilimia kubwa mishahara yao haizidi milioni moja, ukiweka makato wanajikuta na laki tatu na hapo hapo hawajaambulia chochote miaka hii mitano, ngoja tusubiri tuone hao wakataji watakata bei gani kwenye hii 150,000/= ya mwalimu hapo juu..
 
Halafu serikali ikisikiliza huo ujinga na kusitisha hiyo miradi na contractors kutushtaki kwenye mahakama za "ki-miga" hao contractors watashinda. Baada ya hapo ndege (mali) zetu zitaanza kukamatwa huko nje.

Guess what? Wapuuzi haohao watakuja kuilaumu serikali kwa kutuingiza hasara. Tatizo wengi wanaopinga maendeleo akili zao kama za panzi, hazina kumbukumbu.

Rejea suala la ile barabara ya Bagamoyo. Ni bunge lililoishinikiza serikali kuvunja mkataba na mkandarasi baada ya kupuyanga. Alipokuja kupewa tuzo mahakamani huko Ufaransa na ndege yetu kukamatwa Canada, tarumbeta zikaibuka kuisiliba serikali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwenye majina ya hao wabunge aweke tuwajue ila naamini hawawezi kuwa "wale jamaa".
 
Bajeti ya mwenge inatosha,waachane na mishahara,wagonjwa wenye 20!
 
Chadema kama chama kikuu cha upinzani wanapaswa kuonyesha njia mbadala au kuwa mfano kwa kufanya mambo " mema" ambayo CCM hawakuyatilia maanani.

Mfano pale Kenya baadhi ya wabunge wameomba kukatwa kati ya asilimia 30 hadi 50 ya mishahara yao kusaidia mapambano haya nchini mwao. Huko Ulaya kama UK, France na Spain wabunge wamechanga na kusababisha watu wa kada nyingine kuiga mfano.

Hapa Tanzania nimewaona wafanyabiashara wakichangia mfano Rostam Aziz na wengine wengi.

Chadema mnaweza kutuongoza watanzania katika kuchangia janga hili la Corona kwa sababu mna uzoefu na mambo haya ya michango.

Nawatakia Pasaka yenye baraka.

Haleluya....... Haleluya........Haleluya!

Maendeleo hayana vyama.
 
Juzi nilipoona waziri wa nishati akikomaa eti ujenzi wa bwawa jipya haujawahi kusimama na hautasimama kamwe nikasema hatuna viongozi tuna "Kiki Mongers"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…