Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 24,665
- 25,388
Huenda hatma ya uanachama wa wabunge wa viti maalumu wa chadema, maarufu kama wabunge wa COVID-19, ikajulikana mara tu ya bunge kuvunjwa. Inasemekana watapokelewa kwa mapokezi maalumu rasmi chadema mwezi June mwaka huu, mara baada ya ya vikao rasmi vya maridhiano na muafaka wa pamoja kufikiwa.
Wabunge hao waliotengwa na chadema tangu mara baada ya uchaguzi mkuu wa 2020, wataendelea na shughuli zao mjengoni huku mazungumzo yasiyo rasmi baina yao na uongozi mpya wa Chadema taifa yakiendelea vizuri na kutoa matumaini ya muafaka mwema wa pamoja kufikiwa baina yao, huenda ikawa mapema zaidi hata kabla ya mwezi June, muda wa mwisho uliowekwa kuelekea uchaguzi mkuu. Haya yote yanatokea na kufanyika, baada ya mvurugano wa kisheria ngazi ya chama na mahakamani kwa takribani miaka mitano iliyopita.
Taarifa za chini ya kapeti kadiri alivyodokeza mnyetishaji wa tetesi hiii, zinaeleza kwamba wabunge hao tayari wamezilipia kadi zao za uanachama kwa muda mrefu zaidi, lakini pia wanauunga mkono uongozi mpya pamoja na uelekeo wake, na tayari wameupokea vizuri sana hata wito wa mwenyekiti wa Chadema taifa, kwa wanachama na wadau wa chama hicho kukichangia chama hicho kwa hali na mali ili hatimae kipate nguvu ya rasilimali fedha kujiendesha. Na tayari baadhi yao wameshachangia kwa njia ya mtandao na kiasi kingine kimewasilishwa HQ kama ujumbe maalumu kwa uongozi mpya.
Mazungumzo rasmi baina ya wabunge hao na uongozi mpya wa Chadema yanasemekana yanaweza kuanza wakati wowote kuanzia sasa, ili hatimae kua na muafaka wa pamoja mapema iwezekanavyo kwasababu wabunge hao wanahitajika zaidi ndani ya chadema, kuliko wao wanavyohitaji kurudi chadema, kutokana na nguvu ya ushawishi walionao kwenye chama na jamii kwa ujumla.
Ifahamike kwamba sio wabunge wote watakaorejea chadema, baadhi yao wanaelekea vyama vingine vya siasa na kuendelea na maisha mengine.
Ndugu mdau una maoni gani na uelekeo huu wa Chadema na wabunge hawa wa viti maalumu?🐒
Mungu Ibariki Tanzania
Wabunge hao waliotengwa na chadema tangu mara baada ya uchaguzi mkuu wa 2020, wataendelea na shughuli zao mjengoni huku mazungumzo yasiyo rasmi baina yao na uongozi mpya wa Chadema taifa yakiendelea vizuri na kutoa matumaini ya muafaka mwema wa pamoja kufikiwa baina yao, huenda ikawa mapema zaidi hata kabla ya mwezi June, muda wa mwisho uliowekwa kuelekea uchaguzi mkuu. Haya yote yanatokea na kufanyika, baada ya mvurugano wa kisheria ngazi ya chama na mahakamani kwa takribani miaka mitano iliyopita.
Taarifa za chini ya kapeti kadiri alivyodokeza mnyetishaji wa tetesi hiii, zinaeleza kwamba wabunge hao tayari wamezilipia kadi zao za uanachama kwa muda mrefu zaidi, lakini pia wanauunga mkono uongozi mpya pamoja na uelekeo wake, na tayari wameupokea vizuri sana hata wito wa mwenyekiti wa Chadema taifa, kwa wanachama na wadau wa chama hicho kukichangia chama hicho kwa hali na mali ili hatimae kipate nguvu ya rasilimali fedha kujiendesha. Na tayari baadhi yao wameshachangia kwa njia ya mtandao na kiasi kingine kimewasilishwa HQ kama ujumbe maalumu kwa uongozi mpya.
Mazungumzo rasmi baina ya wabunge hao na uongozi mpya wa Chadema yanasemekana yanaweza kuanza wakati wowote kuanzia sasa, ili hatimae kua na muafaka wa pamoja mapema iwezekanavyo kwasababu wabunge hao wanahitajika zaidi ndani ya chadema, kuliko wao wanavyohitaji kurudi chadema, kutokana na nguvu ya ushawishi walionao kwenye chama na jamii kwa ujumla.
Ifahamike kwamba sio wabunge wote watakaorejea chadema, baadhi yao wanaelekea vyama vingine vya siasa na kuendelea na maisha mengine.
Ndugu mdau una maoni gani na uelekeo huu wa Chadema na wabunge hawa wa viti maalumu?🐒
Mungu Ibariki Tanzania