Baadhi ya Wafanyabiashara Iringa nao wagoma kufungua maduka

Baadhi ya Wafanyabiashara Iringa nao wagoma kufungua maduka

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Baada ya kuripotiwa kuwepo kwa mgomo kwa wafanyabiashara Mkoani Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, pia leo June 26, 2024 baadhi ya wafanyabiashara Mkoani Iringa nao wamefunga maduka yao.
IMG-20240626-WA0002.jpg

Mmoja kati ya wafanyabiashara ambaye naye amefunga duka lake, amesema kuwa nao wamechukua uamuzi huo kwa sababu baadhi ya madai yanayolalamikiwa na wafanyabiashara wa Kariakoo yanawagusa na wao.

Ikumbukwe mgomo huo ulianzia Jijini Dar es Salaam kwenye Mkoa wa kikodi wa Kariakoo june 24, 2024 ambapo baadhi ya maduka yameendelea kufungwa licha ya kuwepo kwa taarifa ya kufanyika kikao cha majadiliano baina ya wawakilishi wa wafanyabiashara na Serikali.

Ambapo katika kikao hicho ilielezwa Serikali kuchukua hatua mbalimbali kwenye baadhi ya madai ikiwemo kusitishwa kwa zoezi la ukaguzi wa risiti za Kielekroniki (EFD) na ritani za kodi iliyokuwa ikifanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kupitia mkoa wa kikodi wa Kariakoo, Jijini Dar es Salaam, wakati ukiandaliwa utaratibu rafiki wa utekelezaji wa suala hilo katika Soko Kuu la Kimataifa la Kariakoo.

IMG-20240626-WA0006.jpg

IMG-20240626-WA0003.jpg

IMG-20240626-WA0005.jpg
 
Baada ya kuripotiwa kuwepo kwa mgomo kwa wafanyabiashara Mkoani Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, pia leo June 26, 2024 baadhi ya wafanyabiashara Mkoani Iringa nao wamefunga maduka yao.
View attachment 3026493
Mmoja kati ya wafanyabiashara ambaye naye amefunga duka lake, amesema kuwa nao wamechukua uamuzi huo kwa sababu baadhi ya madai yanayolalamikiwa na wafanyabiashara wa Kariakoo yanawagusa na wao.

Ikumbukwe mgomo huo ulianzia Jijini Dar es Salaam kwenye Mkoa wa kikodi wa Kariakoo june 24, 2024 ambapo baadhi ya maduka yameendelea kufungwa licha ya kuwepo kwa taarifa ya kufanyika kikao cha majadiliano baina ya wawakilishi wa wafanyabiashara na Serikali.

Ambapo katika kikao hicho ilielezwa Serikali kuchukua hatua mbalimbali kwenye baadhi ya madai ikiwemo kusitishwa kwa zoezi la ukaguzi wa risiti za Kielekroniki (EFD) na ritani za kodi iliyokuwa ikifanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kupitia mkoa wa kikodi wa Kariakoo, Jijini Dar es Salaam, wakati ukiandaliwa utaratibu rafiki wa utekelezaji wa suala hilo katika Soko Kuu la Kimataifa la Kariakoo.

View attachment 3026494
View attachment 3026495
View attachment 3026496
Mmh🤣🤣
Mbona hili jengo la iringa plaza frem zake nyingi Bado hazijapata watu?

Labda upige picha miyomboni hapo nitaamini mleta taarifa
 
Halafu kesho kuna mwehu mmoja anasimama ma madungu yake kumsifu mama kwa kukuza uchumi!!
Stud now and ever
 
Mgomo wa wafanyabiashara umeendelea nchini mara baada ya kuanza Kariakoo Jijini Dar es Salaam na baadhi ya majiji lakini mapema hii leo wafanyabiashara wa Manispaa ya Iringa Mkoani Iringa wamefunga maduka yao wakidai kuwa kodi imekua kubwa kuliko kipato wananchoingiza.

Wakizungumza leo Juni 26, 2024 wamesema kuwa kufungwa kwa maduka hayo ni hitaji lao la kupata suluhu ya changamoto ambazo wamekua wakiziwasilisha mara kwa mara kwa Mamlaka ya mapato nchini lakini bado hayafanyiwi kazi.

“Sisi tumeamua kufanya hivi kutokana na namna ambavyo tumekuwa tunaumia kodi imekua kubwa kuliko kipato tunachoingiza ni kidogo na wao wanataka kila mwisho wa mwezi uwe umelipa lakini tofauti na hicho namna wanavyodai imekua changamoto hawajali kama umeuza haujauza”, amesema mmoja wa wafanyabiashara hao.
 
Serikali iturudishie zile Regional Trading Co(RTC).
 
Back
Top Bottom