Siku ya jana, Elon Musk alimtembelea Rais wa Marekani Donald Trump kwenye ofisi ya Rais maarufu kama Oval Office.
Kilichovutia na kushtua wengi ni baada ya kumleta mwanae katika kikao chake na Donald Trump, jambo ambalo limeleta hisia tofauti kwa wachambuzi mbalimbali wa siasa.
Kupitia mitandao ya kijamii, Reublicans wengi wamesifia kitendo cha Elon Musk kumleta mwanae Ikulu wakisema kuwa, hiyo ni ishara ya kukuza na kuheshimisha taasisi ya familia pamoja na utamaduni mzuri wa kupata watoto.
Upande wa Democrats, wengi wameonesha kushangazwa na kitendo hicho wakisema kuwa, Elon kumpeleka mwanae Oval Office tena kuwa na na waandishi wa habari ni ishara ya dharau na kutokuheshimu ofisi ya Rais
Mcheki mtoto wa elon musk akiwa ikulu ya white house chini ya meza ya Rais trump!
Tambueni ya kwamba Elon Musk ndio tajiri namba moja duniani, alafu sio tajiri tu lakini ana miliki teknolojia ambayo ndio inategemewa duniani kwa hiyo ana superiority complex hata akiwa na Trump sababu fedha zake kwa sehemu zimechangia kumuingiza ikulu Trump, hapo ingekuwa ni mtu wakawaida asiyekuwa na sifa hizo angetolewa nduki.