Baadhi ya wana JF shule hawajaenda japo darasani wameingia

Baadhi ya wana JF shule hawajaenda japo darasani wameingia

"Kuingia darasani sio kwenda shule"

Falsafa hii inathibitika pale yule anayejiita msomi anaposhindwa kujitambua katika jamii wakati jamii inamtambua kama msomi.

Napenda kutoa pongezi kwa wana JF wote wanaojitambua na kutimiza wajibu wao kwa nafasi zao katika jamii ikiwemo kulitumia jukwaa hili vyema ipasavyo.

Chakushangaza mambo haya hufanywa na watu wanajiita wasomi na pia ni watu ambao hutegemea kuitwa viongozi katika jamii yetu.

Sheria za jukwaa zipo wazi kuhusu kuzuia matusi, kejeli ama kusanifu watu na mambo mengine kama hayo lakini watu tumekuwa wajinga japo tunajiita wasomi.

Jambo ambalo tunapaswa kulitambua ni kwamba,

"The threads u post identfy urself while ur comments determines ur thinking capacity.

Kutokana na wengi wetu kutumia majina feki tumejikuta tunafanya vitu ambavyo si vyema na kujikosea heshima lakini kutumia jina feki kwa kujificha ili kutusi, kukejeli, kudharau, kutapeli na mengineyo, hakuondoi uhalisia wako zaidi ya kujitia aibu moyoni mwako mwenyewe.

Nini tatzo la wengi wetu.

Wengi wetu huwa hatupost chochote lakini tunasubiri wengine wapost ili tuwatusi, tuwakosoe, tuwaite wajinga, matapeli, hawajasoma na mengineyo.

Sasa kama wewe si mjinga wala si tapeli na pia umesoma sana, mbona hatuoni post yako hata moja japo hatq mara moja tu kwa mwezi?

Matokeo yake unaishia kuona post za wengine za kijinga kwa kukoment matusi ama maneno ya dharau kwa wengine.

Nini tofauti zetu humu.

Tofauti kubwa chache na muhimu ambazo watu wachache tunazo na wengi wetu hatuna zipo katika mambo machache sana lakn muhimu.

Kujitambua,

Nidhamu

Hekima,

Busara,

Yote haya hayapatikani darasani bali hutokana na uzoefu wa maisha pamoja na hofu ya Mungu.

So kama mimi nawe hatuna mambo hayo tajwa hapo juu lakini tunaelimu kubwa na pesa nyingi, basi elimu na pesa zetu zinatusaidia tu kupata ugali na lakini jamii ilojaa welevu bado itatuona wajinga tusiye maana.

Nini tunakaribiana ama kulingana.

Ukiangalia kwa haraka, wengi wetu humu tunalingana ama kutofautiana kwa mstari mwembamba sana kama vile.

*Viwango vya elimu,(taaluma)

*Vipato vyetu,

*Makazi,

*Uelewa,

Yote hayo tunakaribiana, sasa inakuwaje umuone mwenzako mjiiinga eti kisa hukubalianinae?

*Wapo kwao wanaitwa wajinga hapa.

*Wapo ambao walishatelekeza familia zao kwa anasa.

*Wapo walochezea fursa kama vile tuwaonavyo baadhi ya PHD hoders wajinga.

Wapo ambao hukosoa wengine lakini maisha yao magumu.

Lakini tukikutana humu kia mmoja wetu anajifanya anajua kukosoa na kuwaona wengine wajinga badala ya kujifunza jambo na na kutoa mchango wenye tija jukwaani.

Nidhamu inamisingi mitatu.

1. Kujitambua.

2. Kusoma mazingira na alama za nyakati.

3. Kufuata maelekezo.

Ukikosa moja kati ya misingi hiyo ni lazima utakuwa mtovu wa nidhamu katika nyanja zote.

WanaJF, thibitisheni elimu zenu kwa kuzingatia misingi mi3 ya nidhamu ambayo itawapa faida ya kuwa waadifu katika jamii, pia msisahau kuwa na hofu ya Mungu ambayo itawapa faida ya hekima na busara ili tuisaidie jamii kwa elimu au pesa tulizonalo badala ya kuacha mambo muhimu na kuwatolea wengine matusi.

Si vyema kuudharirisha utu wako na nafasi yako kwa kuwatusi wengine, kumbuka kabla ya elimu ulonayo ulipewa akili so usiidharau na kuidharirisha akili yako kwa kigezo cha kuitanguliza elimu yako.Kama wewe ni mmoja wao na nimekukwaza basi pole maana ukweli ndiyo pekee husimama pekee bila support.
mjomba humu kila mtu la lwake utaumiza kichwa chako bure tu
 
Ni kweli kabisa kuna watu kazi yao sio kuchangia hoja upande chanya bali wao huchangia upande hasi, mfano unaweza kutoa post fulani inayohitaji ushauri au kueleweshwa wao wanaanza kukutusi na kukudharau kama vile hawafahamu nini maana ya mitandao ya kijamii, ubarikiwe mtoa mada na ushauri kwa ujumla [emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Kwa hiyo mleta mada ulitaka watu wote wafanane kitabia??
Hapo tu umefeli, usomi wako pia ni wa kuhoji! Watu wana njia tofauti za kuwasilisha hoja zao na mawazo yao, wewe kama msomi ulitakiwa kuwa mvumilivu nao na kuchukua ulichoona kinakufaa na kuacha kisichokufaa.
Kuleta uzi wa kuwafundisha watu wazima ktk jamii ambayo unajua wazi ina mseto wa watu wa aina tofauti ni mapungufu hayo.
Na JF ktk masharti yake haijasema ni ya "WASOMI" tu yaani walioenda darasani na kuelimika tu kama ulivyooweka.
Msomi wa kweli, naongelea an educated individual sio a literate individual anatakiwa akubali kuwa watu wana frame of reference zilizo tofauti.
Ila naheshimu mtazamo wako pia.
 
Kwa hiyo mleta mada ulitaka watu wote wafanane kitabia??
Hapo tu umefeli, usomi wako pia ni wa kuhoji! Watu wana njia tofauti za kuwasilisha hoja zao na mawazo yao, wewe kama msomi ulitakiwa kuwa mvumilivu nao na kuchukua ulichoona kinakufaa na kuacha kisichokufaa.
Kuleta uzi wa kuwafundisha watu wazima ktk jamii ambayo unajua wazi ina mseto wa watu wa aina tofauti ni mapungufu hayo.
Na JF ktk masharti yake haijasema ni ya "WASOMI" tu yaani walioenda darasani na kuelimika tu kama ulivyooweka.
Msomi wa kweli, naongelea an educated individual sio a literate individual anatakiwa akubali kuwa watu wana frame of reference zilizo tofauti.
Ila naheshimu mtazamo wako pia.
Kwahiyo Mkuu Hatuna Haja Ya Kuwasihi Na Kuwafundisha Watu Waache Hii Tabia Coz Tupo Tofauti?
 
Kwahiyo Mkuu Hatuna Haja Ya Kuwasihi Na Kuwafundisha Watu Waache Hii Tabia Coz Tupo Tofauti?
Na yeye akikufundisha kuwa kama yeye kuna tatizo? KAMWE, haitowezekana tukawa sawa. Tofauti tulizo nazo zilikusudiwa na Mungu.
Hivi vitu (HII TABIA, kama ulivyoiweka hapo juu) ni RELATIVE ila tunajaribu kuvifanya ABSOLUTE sababu ndo vinaonekana sahihi ktk jamii.
Hivyo waweza kuwafundisha ila tambua kuwa kamwe jamii haitoweza kuwa na mtazamo mmoja.
 
Na yeye akikufundisha kuwa kama yeye kuna tatizo? KAMWE, haitowezekana tukawa sawa. Tofauti tulizo nazo zilikusudiwa na Mungu.
Hivi vitu (HII TABIA, kama ulivyoiweka hapo juu) ni RELATIVE ila tunajaribu kuvifanya ABSOLUTE sababu ndo vinaonekana sahihi ktk jamii.
Hivyo waweza kuwafundisha ila tambua kuwa kamwe jamii haitoweza kuwa na mtazamo mmoja.
Sawa Mkuu Nakuelewa Sana Lakn Tambua Ya Kuwa Mafunzo Yapo Ili Kila Mmoja Achague Lake.
Hata Nyumba Za Ibada Tunaenda Kila Siku Na Kila Siku Tunapewa Neno So Ni Uamuzi Wetu Kubadilika Ama Kubaki Tulivyo Lakn Mafunzo Yapo Ta Tofauti Zipo.
 
Sawa Mkuu Nakuelewa Sana Lakn Tambua Ya Kuwa Mafunzo Yapo Ili Kila Mmoja Achague Lake.
Hata Nyumba Za Ibada Tunaenda Kila Siku Na Kila Siku Tunapewa Neno So Ni Uamuzi Wetu Kubadilika Ama Kubaki Tulivyo Lakn Mafunzo Yapo Ta Tofauti Zipo.
Uko sawa mkuu,unapoona kitu hakipo sawa ni muhimu kuweka sawa. Kila mtu yupo huru kulingana na mtazamo wake, na kila mtu anautashi wa kuchagua kile kimfaacho...

Umetoa ushauri ni uamuzi wa kila mmojawetu kuukubali ama kukataa.
 
Nilikuwa namtafta flani,, mana hajui kukosoa kwa lugha yenye staha,, kasemwa hata simuoni na kila uzi yupo kasoro huu , kapita kmyakimya
[emoji115] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] We Mchokozi Wew Bana, Mi Simo Nilikuwa Najenga Hoja Tu Ila Kama Anatabia Hii Basi Aache Maana Si Vyema Hata Kidogo.
 
[emoji115] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] We Mchokozi Wew Bana, Mi Simo Nilikuwa Najenga Hoja Tu Ila Kama Anatabia Hii Basi Aache Maana Si Vyema Hata Kidogo.

Mbona lugha yako poa tu mkuu
,,kukosolewa si mbaya ila kuwe ktk namna ambayo nitatamani kuwa kama mkosoaji,, mtu anakukosoa hadi unawaza Huyu sijamuona ila anahitaji psychologist
 
Back
Top Bottom