Baba Chaula: Nimepigiwa simu na namba ngeni, kaniambia nitoe Tsh. Milioni 3 ili Chaula apatikane

Baba Chaula: Nimepigiwa simu na namba ngeni, kaniambia nitoe Tsh. Milioni 3 ili Chaula apatikane

Mnaweza laumu serikali lakini kumbe ni lack of exposure and awareness yao ni ndogo.

Biashara za kuteka watu hela zipo,
Biashara za kukodi wauaji zipo,

Sema ukute viongozi wanashupaza vichwa mana hawajui hilo huku wakiona lawama wanapewa wao.
Kwa hiyo madai ya Mbowe kuhusu Polisi kuhusika kwa kuwataja majina wahusika ni madai ya uongo?

Mambo yote uliyoyaongea yapo katika jamii, lakini madai ya vyombo vya dola vinavyohusika na ulinzi wa roho za raia, kwetu sisi ndiyo habari kubwa kuliko hizi zinazozushwa sasa hivi kufunika uovu wa vyombo vya Serikali.

Ungelitaka ueleweke vizuri ungeanza kulaani kwanza Polisi watekaji, ndiyo uje sasa na hoja ya mahaba na 'gavumenti' yako na tena uijengee hoja ya utetezi yenye akili, maana raia wengi Tz kwa sasa, washazielewa mbivu na mbichi, waweza usieleweke.
 
hao ni matapeli, mtoto yuko na polisi! Amuachie Mungu atatoa suluhisho!
Pia kuna uwezekano watekaji wake ambao wanaweza kuwa ni hao watekaji wenye namba halali vifuani mwao ili kuwapoteza maboya wananchi wakaandaa watu wa kuwapigia simu wazazi kudai pesa ili kujenga mazingira kuwa kijana alitekwa na watu wenye nia ya kujipatia pesa na siyo wao.
 
Ukijiona kwenu maisha ya kuungaunga usijiingize kwenye masuala ya uwanaharakati wa vyama vya siasa.

Unapomtukana Rais ina maana umeitukana system nzima ya nchi.

Vijana kuweni makini mdomo uliponza kichwa. Mwenye mamlaka kashika mpini ,wewe raia umeshika makali. Ukimkosoa au kushamshauri tumia lugha za kistaarabu na kiungwana. Laa sivyo itakayoteseka ni familia yako
 
Ukijiona kwenu maisha ya kuungaunga usijiingize kwenye masuala ya uwanaharakati wa vyama vya siasa.

Unapomtukana Rais ina maana umeitukana system nzima ya nchi.

Vijana kuweni makini mdomo uliponza kichwa. Mwenye mamlaka kashika mpini ,wewe raia umeshika makali. Ukimkosoa au kushamshauri tumia lugha za kistaarabu na kiungwana. Laa sivyo itakayoteseka ni familia yako
Watu waisome hii na waielewe. Kiafrica mfumo unaweza kukufanya lolote na familia isiwe na pa kusemea zaidi ya maumivu kuwaachia. Mimi hizi habari za siasa sijui kupiga kura sina mda nazo'
 
View attachment 3083542
Mzee Yusuph Sisala Chaula akiwa na mwanaye Shadrack Chaula

Kufuatia taarifa za kupotea katika mazingira yanayodaiwa ‘kutekwa’ kwa Shadrack Chaula ambaye ni Msanii wa Sanaa ya Uchoraji, baba mzazi wa kijana huyo, mzee Yusuph Sisala Chaula amesema amepigiwa simu akitakiwa kutoa Shilingi Milioni 3 ili aweze kumpata mwanaye.

Mzee Chaula anasema “Nimepigiwa simu na namba ambayo siifahamu, namba yenyewe ni 0763 55.... na wala mhusika hakujitambulisha, ameniambia natakiwa kukubali kutoa Shilingi milioni tatu ili niweze kumpata mtoto wangu.

“Nikamwambia sawa kama ni mzima na yuko salama sawa ngoja tutafute hiyo fedha. Baada ya kujadiliana na familia tukaona bora tutoe hiyo taarifa Polisi kwa kuwa wao ndio wanaohusika na upelelezi.
View attachment 3083527
Shadrack Chaula
“Nimetoa taarifa na kuikabidhi namba husika kwa Mkuu wa Kituo cha Polisi Kiwila pamoja na kwa mpelelezi wa suala hilo la kupotea kwa mtoto wangu katika mazingira ya kutatanisha.

“Simu hiyo nilipigiwa mchana wa Agosti 30, 2024 na hadi sasa Agosti 31 bado sijapata mrejesho wowote kutoka kwa Jeshi la Polisi kuhusu hiyo namba au huyo mtu aliyepiga, pia sijajulisha mpaka sasa upelelezi wa Shadrack umefikia wapi.”

JamiiForums ilipowasiliana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, SACP Benjamin Kuzaga kuhusu suala hilo amesema “Bado sijapata taarifa kuhusu suala hio, nipo kwenye mbio za Mwenge, labda nikirejea nitapata taarifa.”

Pia soma:
~ Baba Chaula: Polisi niambieni mwanangu kama yu hai tu basi inatosha, nahisi roho yangu inashindwa kuvumilia haya maumivu

~ Aliyehukumiwa kwenda jela miaka 2 kwa kuchoma picha ya Rais amechukuliwa na watu wasiyojulika, mpaka sasa hajulikani alipo
Awe makini tu, wasije kuna watu wakawa wanataka kupiga hela tu na watokomee
 
Back
Top Bottom