Baba Chaula: Polisi niambieni mwanangu kama yu hai tu basi inatosha, nahisi roho yangu inashindwa kuvumilia haya maumivu

Baba Chaula: Polisi niambieni mwanangu kama yu hai tu basi inatosha, nahisi roho yangu inashindwa kuvumilia haya maumivu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Kufuatia taarifa za kupotea katika mazingira yanayodaiwa ‘kutekwa’ kwa Shadrack Chaula ambaye ni Msanii wa Sanaa ya Uchoraji, baba mzazi wa kijana huyo, mzee Yusuph Sisala Chaula amesema anaomba ajulishwe tu mwanaye kama yu hai au la ili moyo wake uwe na amani.

Amesema “Unajua inaweza kufa roho moja lakini hiyo moja ikafa na nyingine kadhaa kutokana na mawazo. Siku ya nne sasa sijui mwanangu yuko wapi.

“Polisi wamesema wanaendelea na uchunguzi lakini mpaka sasa wapo kimya na sina taarifa zozote, kama yupo hai waniambie tu ili nafsi yangu itulie, kama ameshikiliwa na Vyombo vya Usalama waniambie tu pia nijue yupo hai tutaenda kumuona.

“Hata kama yupo gerezani waniambie tu nitajua yupo hai na ipo siku nitaenda kumuona, naongea kwa uchungu sana, najiona nashindwa kuvumilia haya maumivu, sijui nini kitatokea, lakini naomba Serikali iniambie tu mwanangu yuko hai hata kama wanaendelea kumshikilia kuliko huu ukimya uliopo sasa.

“Mara ya mwisho tumewasiliana na Mpelekezi tuliyepewa asimamie suala hilo jana (Agosti 5, 2024) baada ya hapo hatujapata taarifa nyingine ya ziada.”

JamiiForums ilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, jana Agosti 5, 2024, alipoulizwa kuhusiana na suala hilo alisema “Nipo msibani tutawasiliana baadaye.” Baada ya hapo simu yake haikupokelewa.

Alipotafutwa leo Agosti 6, 2024, simu haikupokelewa, akatuma ujumbe “Nitakupigia baadaye.”

Ikumbukwe Julai 8, 2024, Shadrack Chaula aliachiwa huru kutoka gerezani baada ya kulipa faini ya Tsh. Milioni 5 ikiwa ni siku chache tangu kuhukumiwa kifungo cha Miaka Miwili jela au kulipa Faini hiyo kwa kosa la kutoa taarifa za uongo Mtandaoni.
 
Polisi watajuaje kama yupo hai au amekufa? Au mara ya mwisho wamemchukua wao?
 
polisi kama wangekua wamemshikilia wao basi kungekua na taarifa kwasababu alivunja sheria hivyo sidhani kama polisi wangekua na sababu yeyote ya kumshikilia kkwa siri wakati amevunja sheria na iko wazi, labda polisi wangesaidia tu kufanya uchunguzi wa kina juu ya upoteaji wa kijana huyo na sio kuwatolea lawama kua wanahusika na uopotevu wa kijana wenu.
 
“Hata kama yupo gerezani waniambie tu nitajua yupo hai na ipo siku nitaenda kumuona, naongea kwa uchungu sana, najiona nashindwa kuvumilia haya maumivu, sijui nini kitatokea, lakini naomba Serikali iniambie tu mwanangu yuko hai hata kama wanaendelea kumshikilia kuliko huu ukimya uliopo sasa.
Huo ukoo ni wa moto, hao wahusika wajiandae kuanza kupukutika mmoja mmoja
 
Kufuatia taarifa za kupotea katika mazingira yanayodaiwa ‘kutekwa’ kwa Shadrack Chaula ambaye ni Msanii wa Sanaa ya Uchoraji, baba mzazi wa kijana huyo, mzee Yusuph Sisala Chaula amesema anaomba ajulishwe tu mwanaye kama yu hai au la ili moyo wake uwe na amani.

Amesema “Unajua inaweza kufa roho moja lakini hiyo moja ikafa na nyingine kadhaa kutokana na mawazo. Siku ya nne sasa sijui mwanangu yuko wapi.

“Polisi wamesema wanaendelea na uchunguzi lakini mpaka sasa wapo kimya na sina taarifa zozote, kama yupo hai waniambie tu ili nafsi yangu itulie, kama ameshikiliwa na Vyombo vya Usalama waniambie tu pia nijue yupo hai tutaenda kumuona.

“Hata kama yupo gerezani waniambie tu nitajua yupo hai na ipo siku nitaenda kumuona, naongea kwa uchungu sana, najiona nashindwa kuvumilia haya maumivu, sijui nini kitatokea, lakini naomba Serikali iniambie tu mwanangu yuko hai hata kama wanaendelea kumshikilia kuliko huu ukimya uliopo sasa.

“Mara ya mwisho tumewasiliana na Mpelekezi tuliyepewa asimamie suala hilo jana (Agosti 5, 2024) baada ya hapo hatujapata taarifa nyingine ya ziada.”

JamiiForums ilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, jana Agosti 5, 2024, alipoulizwa kuhusiana na suala hilo alisema “Nipo msibani tutawasiliana baadaye.” Baada ya hapo simu yake haikupokelewa.

Alipotafutwa leo Agosti 6, 2024, simu haikupokelewa, akatuma ujumbe “Nitakupigia baadaye.”

Ikumbukwe Julai 8, 2024, Shadrack Chaula aliachiwa huru kutoka gerezani baada ya kulipa faini ya Tsh. Milioni 5 ikiwa ni siku chache tangu kuhukumiwa kifungo cha Miaka Miwili jela au kulipa Faini hiyo kwa kosa la kutoa taarifa za uongo Mtandaoni.
Mwanae alitaka sifa,kwaiyo wapo nae huko wanampa hizo sifa
 
Kila siku kuna habari za watu kupotea,kutekwa,lakini waziri na rais wote wanasema nchi ipo salama na hakuna utekaji. INAWEZEKANA VIONGOZI WANAISHI TANZANIA YAO NA RAIA TUNAISHI TANZANIA YETU, yaani yanayotokea hawana taarifa.
Simlimchukulia poa Samia,sasa mnashughulikiwa na deep state nadhani sio Samia tena, kilio chenu wamekisikia cha kumnanga samia na kumkumbuka magufuli, kwaiyo wanamuenzi jiwe pamoja nanyi
 
Huwez kugusa tabaka tawala ukabaki salama tusidanganyane wandugu .
Hizi harakati zetu tuzifanye tukijua hatuko ulaya au marekani kwenye Uhuru wa kujieleza tuko Africa ambapo viongozi hawapendi kuambiwa ukweli.
Unapojifanya mwamba baada ya kubugia katoto kako tambua freedom after speech haiko guaranteed
 
Huyu ndo yule aliechoma picha ya raisi?..
 
Hawa si ndo familia iliyosema kwamba wanaomba msamaha kwa kijana kuchoma picha Tena arochora mwenyewe ?

Namuhurumia kijana maana akiwekwa kwenye karakana uwa si pazuri Ila simuhurumii huyo mzee hata Kidogo,

Britanicca
 
Unamtukana Rais........ugomvi huku siingilii ngoja ninywe ulanzi hapa
 
Kufuatia taarifa za kupotea katika mazingira yanayodaiwa ‘kutekwa’ kwa Shadrack Chaula ambaye ni Msanii wa Sanaa ya Uchoraji, baba mzazi wa kijana huyo, mzee Yusuph Sisala Chaula amesema anaomba ajulishwe tu mwanaye kama yu hai au la ili moyo wake uwe na amani.

Amesema “Unajua inaweza kufa roho moja lakini hiyo moja ikafa na nyingine kadhaa kutokana na mawazo. Siku ya nne sasa sijui mwanangu yuko wapi.

“Polisi wamesema wanaendelea na uchunguzi lakini mpaka sasa wapo kimya na sina taarifa zozote, kama yupo hai waniambie tu ili nafsi yangu itulie, kama ameshikiliwa na Vyombo vya Usalama waniambie tu pia nijue yupo hai tutaenda kumuona.

“Hata kama yupo gerezani waniambie tu nitajua yupo hai na ipo siku nitaenda kumuona, naongea kwa uchungu sana, najiona nashindwa kuvumilia haya maumivu, sijui nini kitatokea, lakini naomba Serikali iniambie tu mwanangu yuko hai hata kama wanaendelea kumshikilia kuliko huu ukimya uliopo sasa.

“Mara ya mwisho tumewasiliana na Mpelekezi tuliyepewa asimamie suala hilo jana (Agosti 5, 2024) baada ya hapo hatujapata taarifa nyingine ya ziada.”

JamiiForums ilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, jana Agosti 5, 2024, alipoulizwa kuhusiana na suala hilo alisema “Nipo msibani tutawasiliana baadaye.” Baada ya hapo simu yake haikupokelewa.

Alipotafutwa leo Agosti 6, 2024, simu haikupokelewa, akatuma ujumbe “Nitakupigia baadaye.”

Ikumbukwe Julai 8, 2024, Shadrack Chaula aliachiwa huru kutoka gerezani baada ya kulipa faini ya Tsh. Milioni 5 ikiwa ni siku chache tangu kuhukumiwa kifungo cha Miaka Miwili jela au kulipa Faini hiyo kwa kosa la kutoa taarifa za uongo Mtandaoni.
Ungemkanya mapema haya yasingetokea, Palestine kushindana na Israel nadhani unajua kinachofanyikaga.

Hope Polisi watakujibu.
 
Back
Top Bottom