Baba Mtakatifu Francisko ateua Makadinali wapya 21

Baba Mtakatifu Francisko ateua Makadinali wapya 21

Didododi

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2023
Posts
347
Reaction score
465
Snapinsta.app_462285177_989227089912564_3636072309805860310_n_1080.jpg

Baba Mtakatifu Francisko, ameteua Makardinali wapya Ishirini na Moja (21), mmoja anamiaka 99 na ametangaza kuwasimika rasmi Disemba 08, 2024 katika Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili.

Baba Mtakatifu ametangaza uteuzi huo Dominika ya Oktoba 6, 2024 majira ya mara baada ya Sala ya Malaika wa Bwana na kusema kuwa watasimikwa siku ya Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili, ambayo hufanyika kila mwaka Disemba 08.

Amesema lengo la kuwa na wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za dunia kwenye Baraza la Makardinali ni kushuhudia Kanisa moja, Takatifu, Katoliki na la Mitume, ambapo mpaka sasa kuna Makardinali 256.

Aidha, amesema kazi ya Makardinali kutoka sehemu mbalimbali za dunia, wanaitwa na kutumwa kutangaza na kushuhudia huruma na upendo wa Mungu kwa waja wake.

Hata hivyo, Mababa wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican wanasema, kwa nguvu ya Ukatoliki (Catholicitatis) huu ni kwa sababu kila sehemu kuna wawakilishi wa Baba Mtakatifu, ambao mara zote hupeleka vipaji vyake na kwa Kanisa lote na daima hufanya juhudi kila mmoja ili kupata ukamilifu katika umoja.

Baba Mtakatifu Fransisko amewaomba waamini kuendelea kuwaombea Makardinali hao ili kwa kuteuliwa kwao wakashikamane kabisa na Kristo Kuhani Mkuu, mwenye Huruma na mwaminifu na ili wamsaidie kiuaminifu katika majukumu yake kwa watu wa Mungu.

#Redio Maria Tanzania
 
Kanisa la sinodi... Ushiriki, ushirika na umisionari.
 
Inawezekana anandaa mrithi wake kwa kuhakikisha mchakato wa upatikanaji wake uwe mkali na jumuishi ili akipita, awe wa wote kwa itikadi yoyote ile atakayobeba?
 
Mbona vijana hawali shavu kwenye hizi teuzi?
 
Mvi zimejaa nyingi kweli hapo ukumbini, Baraza limejaa wazee, may be ndo wenye busara na wanaojua mission na vision kisawasawa, taasisi kubwa kama hiyo kujaza vijana wa Sasa hivi ni kujitakia kufa Bure.
 
Baba Mtakatifu Fransisko amewaomba waamini kuendelea kuwaombea Makardinali hao ili kwa kuteuliwa kwao wakashikamane kabisa na Kristo Kuhani Mkuu
Very confusing, wao si ndiyo wamepewa mamlaka ya kutuombea?
Sisi tunawaombeaje wakati hatuna vigezo vya kuongea na Mungu isipokuwa wao tu?
 
Very confusing, wao si ndiyo wamepewa mamlaka ya kutuombea?
Sisi tunawaombeaje wakati hatuna vigezo vya kuongea na Mungu isipokuwa wao tu?
Wewe utakuwa ni Mkatekumeni bila shaka. Mkatoliki hawezi kuuliza maswali ya aina hii.
 
Back
Top Bottom