Baba yake Majaliwa mvuvi ajitokeza na kudai..

Baba yake Majaliwa mvuvi ajitokeza na kudai..

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Nimepitia kwenye mitandao nimekuta kuna habari kubwa kumhusu Majaliwa kijana ambaye amevunja vichwa vya habari hapa juzi kwa kuongoza zoezi la kuwaokoa abiria wa ajali ya ndege huko Bukoba.
IMG-20221109-WA0031.jpg

Baba huyo ametoka hadharani na kudai kwamba pesa ambayo Majaliwa alipewa kama motisha ni ya familia na Majaliwa atawekewa mgao wake. Ameenda mbali zaidi akidai kuwa hali yao ya maisha ni ngumu na wadogoze Majaliwa wanahitaji kusaidiwa kupitia fedha hizo.
IMG-20221109-WA0033.jpg

Sakata la Majaliwa sasa linachukua sura mpya kutoka kwenye ngazi ya Kitaifa na sasa kuhamia kwenye himaya ya kifamilia ambapo msemaji wa familia ni baba. Msimamo wa baba huyo unaakisi aina ya malezi na desturi ambazo jamii inapaswa kuondokana nazo.
 
Mzee kaingia chaka miaka yote hiyo ila baada ya kusikia kuna mtonyo kaibuka kama msemaji mkuu.
Anataka kuleta mambo ya ukikutwa na bangi eneo lako ni yako pamoja na hukumu yake ila ukikutwa na madini basi ni ya serikali.

Mizee kama hii ndio inafanya wanaume wote waonekane wajinga.

Ingesemekana Majaaliwa kafanya kosa kuvunja mlango wa ndege, je napo angejitokeza pia? Nina hakika angesema mbovu kwa mama Majaliwa kuwa mtoto wake ni muhuni na afungwe tu. Ila kwenye pesa anakuwa ni mtoto kipenzi.

Yani kuhatarisha maisha ahatarishe mwingine zawadi ziwe za wote. Pumbavu.
 
Dah,,

Naomba wadau wasitishe kutoa pesa Kwa Majaliwa.

Kuna dalili ya family hii kutoana roho huko mbeleni.

Mama wa mtoto amesema huyo Mzee alikimbia family,
Leo kaibuka anasema apewe yeye pesa ni ya family.


Hivi mtu akiajiriwa kazini pesa za family au za muajiriwa?

Njaa mbaya sn
 
Sidhani kama hivi vina sifa ya kuitwa vyombo vya habari. Hivi ni vijiwe vya kupiga gumzo.
Nasikitika sana kwamba tumebaki na vijiwe vya kupiga gumzo kama unavyosema, hatuna vyombo vya habari kabisa hapa nchini.

Hebu fikiria,imetokea ajali, watu wamepoteza wapendwa wao lakini chombo cha habari kimeona habari ya kufuatilia na kuiendeleza ni ile ya kijana aliyekuwepo kwenye uokoaji, tumfuatilie na kuhoji wazazi wake wote. Tuwahoji maswali ambayo yatatengeneza habari kwa wiki nzima.

Hili ni tatizo sasa na hivi mama wa kijana alishasema baba aliwaacha hayupo nao nyùmbani hapo inatafutwa stori nyingine.

Hii ndio shida ya kujaza watu wenye shule ndogo sehemu zinazohitaji watu wabobevu kwenye taaluma husika.
 
Yani clouds wanazidi kujishusha na content zao zisizoelewa. Habari zao nowdays hazina tofauti na online media zilizoibuka kama Uyoga. Ruge kafa na hadhi ya kituo chali
 
Back
Top Bottom