Bablee yuko wapi?



Sasa nimekuelewa mkuu. Basi kijana alikuja na ubunifu mzuri sana sema alichelewa kutoka tu.
 
haha kweli dogo alilewa sifa na alizidisha utozi na u-bulazaaaa men..talent without brain ni zero... haha hapo kwa diamond umeniacha kidogo ..hehe vipi je unaona amemzidi na king kiba au ni dadamond tuuuu..

Kwa King Kiba na Diamond bado hajafika level hizo but mi binafsi naamini kipaji chake. Afu isitoshe kila mtu ana ladha zake.
 
Nilipoona huyu jamaa kasema eti kaiga stle ya bluu nilishangaa mno nadhani bableeni ujana na marafiki ambao niliwahi kumuona nao siku za nyuma...ila ana kipaji kuliko huyo blue na diamond
Tema mate chini wewe. ..huyo bablee kipindi ana kanyimbo kake kizizi alitoa shooting anaonekana kabisa mshamba shapu na ule mkanda aliovaa wenye buckle kama sufuria. ..usimfananishe na byser ambaye alivyotoka aliliteka jijini lote la mzizima na Tanzania kwa ujumla
 
Last tym alikua ana bustani ya maua hapo kwa msuguri
 
ule wimbo kizizi ulimponza, kawa dokta manyaunyau siku hizi....mtaani kwenu kama kuna ndele wengi muite tu atakuja hana hiyana, hiyo ndio kazi yake
 
Khaaaa watu wabaya?
Eti buckle kama sufuria....
Ila kizizi ulikua poa bana,tena sana tu.
 
mpenzi niondolee hiki kizizi, niondolee kizizi kukupenda wewe nilikizi umukusudia kunipa uchizi, si ungenienzi sio hirizi, kwa kifupi kizizi.

kizizi na mii nami nakizizi kizizi namii nami na kizizi dah ngoma kali ile na kichupa chake kimetulia
 
Huyo ni kati ya wasanii waliotegemea mgongo wa Bluu kutoka, sasa wanaisoma namba wakati Bluu bado yumo
 
Huyo ni kati ya wasanii waliotegemea mgongo wa Bluu kutoka, sasa wanaisoma namba wakati Bluu bado yumo
wapi wewe.. blue mwenyewe alikiri wakati akipambana kutoka alikua anaiba swagga za huyu jamaa
 
Acheni kutudanganya. Bablee alikuwa anakopi. Ata bob junior kabla hajabadili style, nae alikuwa ni mtumwa wa style ya blue.
 
Zero brain,kijiwe posta,watoto wa jiteute mpo?
 
Nilipoona huyu jamaa kasema eti kaiga stle ya bluu nilishangaa mno nadhani bableeni ujana na marafiki ambao niliwahi kumuona nao siku za nyuma...ila ana kipaji kuliko huyo blue na diamond
Mkuu unamaanisha huyu diamond wa WCB au diamond mwingine?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…