Babu kaniambia ili tushinde Leo huko Burundi Kikosi cha Kuanza Taifa Stars kiwe hivi.....

Babu kaniambia ili tushinde Leo huko Burundi Kikosi cha Kuanza Taifa Stars kiwe hivi.....

Hata mech ya simba na wamakonde ulikuja na ngojera hizi hizi , mwisho simba wakatolewa

Mpira ni mchezo wa wazi, kama huna maandalizi utapigwa tu
Kushinda sio maandalizi tu. Kunatokana na mambo mengi. KWANI BARCELONA ILIVYOTOLEWA NA LIVERPOOL ilikuwa haina MAANDALIZI?
 
Mohamed Hussein ameitwa lini? hiyo ramli ni uongo

Kwa huu Upumbavu wako nikikuita Mpumbavu nitakuwa nakukosea / nakosea? Una uhakika huyo Mohamed Hussein ' Tshabalala ' hajaitwa Taifa Stars? Angalia Kikosi cha leo hasa wale walioko Benchi je Jina lake halipo? Kuna Watu nikiwa nawadharau hapa Jamvini msiwe mnakasirika au mnaninunia.
 
Game inaonyeshwa ndani ya kishumbusi gani?

Kile ambacho Kampuni yao inaongoza kwa Kuwatoa ' Kafara ' Wafanyakazi wake ambao na Wao pia wanaongoza kwa ' Kurogana ' hadi Kufa Vifo vya ghafla kwa sababu ya Vyeo na Maslahi. Kinaitwa Tabata Media / Tabata Tv Kiongozi.
 
1. Juma Kaseja / Beno Kakolanya
2. Shomary Kapombe / Hassan Ramadhan Kessy
3. Mohamed Hussein Tshabalala
4. Erasto Nyoni
5. Kelvin Yondan
6. Jonas Mkude / Mohamed Issa Banka
7. Simon Msuva / Salim Ayei
8. Abubakari Salum / Frank Domayo
9. Abdillahi Yusuph / Idi Nado
10. Mbwana Samatta
11. Ally Ng'anzi / Hassan Dilunga

Kuna Ushindi wa Goli 2 kwa 1 au 1 kwa O katika Kipindi cha Kwanza hivyo tunatakiwa tuwawahi kwani ndiyo Nyota yetu ya Ushindi inavyosema kwa Mchezo wa leo, ila kama hatutashinda ndani ya dakika 45 za Kwanza kwa aina ya Uchawi wa Kufuru ambao Waburundi nao wameufanya ( kwani nao hawatanii na wamejipanga vilivyo ) basi kuna uwezekano wa Taifa Stars ikafungwa Goli / Bao 1 tu.

Hiki Kikosi nilichokitaja hapo naomba Kizingatiwe tafadhali na Watu wa Benchi la Ufundi wapewe haraka asubuhi hii hii na wakifanya tu Mabadiliko basi yawe ni hayo tu ambayo nimeyaweka hapo juu na siyo mengineyo. Huyu ' Babu ' huwa hakosei na hajawahi Kuniangusha hivyo TFF msipuuze bali mlizingatie na muwe makini.

Kila la Kheri.
Na mpemba kasemaje?
 
Huyo Shamte sijui kamtoa wapi, uchochoro kasababisha tukojozwe
 
Kile ambacho Kampuni yao inaongoza kwa Kuwatoa ' Kafara ' Wafanyakazi wake ambao na Wao pia wanaongoza kwa ' Kurogana ' hadi Kufa Vifo vya ghafla kwa sababu ya Vyeo na Maslahi. Kinaitwa Tabata Media / Tabata Tv Kiongozi.
Ya kweli haya??
 
Back
Top Bottom