Babu Tale kumsaidia Chid Benz

mujimali

Senior Member
Joined
Jun 21, 2013
Posts
190
Reaction score
116
Chid Benz a.k.a chuma, ambae hivi karibuni afya yake imeshtua wadau wengi wa muziki na hata wale wasio wadau, kutokana na kudhoofika sana jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limechangiwa na utumiaji wa dawa za kulevya.

Mkali huyu wa "Dar es salaam stand up", alikiri na kuonesha majuto, na kuonesha nia thabiti ya kubadilika, hivyo kutaka msaada wa wadau mbali mbali.. Hatimaye msaada huo umewasili.

Hamis Tale au Babu Tale amejitokeza na kuonesha nia ya kumsaidia Chid benz, katika ukurasa wake wa Instagram amepost video clip anamuonesha akiwa yeye na Chid na kuandika caption inayoonesha dhahiri anayo nia ya kumrudisha chid kwenye mchezo.

Natumai huyu jamaa atabadilika kweli this time.
 
Hivi mtumia maunga anasaidiwaje kwa mfano zaidi ya yeye mwenyewe kuamua kuacha ????
 

Namshauri Babu Tale asimsaidie kabisa huyu jamaa kimziki.. Amsaidie kuondokana na madawa ya kulevya.. Muda wake alipewa na akashindwa kuutumia na kufanya ubabe… Babu Tale wasaidie vijana wadogo wanaochipukia kimuziki na wenye vipaji na hawana mtu wa kuwasaidia..

Huyu Chid asaidiwe aondokane na madawa ya kulevya then abadilishiwe kazi (kama magufuli anavyowachambua)..

IKIWEZEKANA Apewe jembe akalime huko Bagamoyo, au Kisarawe..
 
Aanze kujisaidia mwenyewe kwa kuacha unga.

Tale atamsaidia kimuziki,kama ataendelea na utumiaji naye atamkimbia.
 
Kipindi kile alivyokuwa na kesi angewekwa Segerea miezi sita wangeokoa maisha yake. Lakini walivyomsaidia kumuhonga hakimu na kumlipia faini walifikiri ndio wanampenda sana kumbe ndio wamempoteza. Watu wengine jela inawafaa kwa kubadilisha maisha
 
Huyu jamaa alishasaidiwaga na masela lakini akawa mbishi...akarudi kwenye dawa, sasa ndo yamemla zaida
 
Tale nae ni kizabizabina tu,tena si yeye pekee pamoja na fella na ruge hawa watu wanajifanya wao ndo incharge wa mziki hapa bongo walionavipaji na wanaweza kujitetea wanawakandamiza,wasioweza ndo wanataka wasikike kama Ally nipishe na rubi najionea fujo tu,ndo mana siku ya msiba wa ngwair JMO na P funk walichukizwa na wale wanajifanya wataileta maiti ya ngwair kwa uwezo wao wakati ngwair alipendwa na watanzania wengi na angeweza kuchangiwa maiti yake ikarudishwa,kumbe ni kama wanamlipa mshahara marehemu,sasa nadhani tale na washkadau wenzake wanataka kumlipa marupurupu yake chid,UBINADAMU UMEKWISHA KWELI.
 
Unachosema kina ukweli ndani yake. Hawa jamaa wanahisi wana-own mziki wa bongo, yani bila wao hutoki.
Ila tatizo na wasanii wengi siku izi wameshakubaliana na hio hali, wanahisi bila hao jamaa hutoki.
 

Nimekupenda bure tu, hata sjui kwa nini jmn...!.

Lol.
 
Point..
Kwaio hawa jamaa mtu analipwa baada ya matatzo dah ni wanyonyaji sana. Chid amesaidia sana wasanii wa Tale kama Tunda wengne nimesahau kwaio definitely Tale amefaidika sana kupitia chid ila sahv anasema anatoa msaada kwa Chid..
ubinadamu kazi sana.
#
 
Mziki ukipata nafasi ukaichezea ndio bhasi huyo jamaa hawezi kurudi tena kwenye peak milele milele Amina....
 
(Inasemekana) Yeye mwenyewe Tale ni Teja sasa atamsaidiaje Chid kibajaj Teja mwenzie?
 
CLOUDS NAHISI KAMA WATAITUMIA FURSA HII KUPIGA HELA, KWA SASA CHIDDY NI MTAJI MZURI TU
 
Ilalaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.....The Return Of King Kong
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…