Babuuu huyoo Loliondo

nyamungo mwanetu vikombe vipo vya kutosha hata serikali kupitia wilaya ya ngorongoro wamempa sapoti ya vikombe wasaidizi wa kuokota kuni, karibu kwa babu matibabu jero na imani yako
 
Hizi picha za watu wakiwa na kikombe zinaonyesha mengi sana , kuna jamaa mmoja kashikilia kikombe namfahamu sasa najua alikuwa hana tatizo la kisukari wala presha, nilipomuonja nikampigia nikamuuliza anatatizo gani ? Jamaa kaniambia hajaenda kwa babu nikamwambia aingie JF aone picha , mpaka sasa kazima simu sijui kwa nini.
Mnaoleta picha mnaweza kuwapa wengine ugojwa mpya......
 

Use African solutions blessed with God to solve African problems.
 
Hujakosea sana mkuu.... mwisho wa siku babu atatutabiria mteule moja wa Mungu tumuunge mkono!!!

Kiukweli watanzania wengi ni wagojwa!!!

Assume anatuambia ni EL au RA:::::::::::::::::::::::::::::::::::
 
...kuna mtu namfahamu ameenda kule na mkewe, wamerudi jamaa anasema kapona mkewe amelazwa hoi taabani... nikamuuliza kulikoni shemeji akajibu kwamba alilazimishwa na mumewe kwenda yeye hakuwa akiumwa... NIKAJIULIZA KUNA SIRI GANI KWA BABU? na bado nitaendelea kujiuliza siku ile matokeo yatakapokuwa tofauti na leo JE LAWANA ZITASUKUMWA KWA NANI? ....lazima babu hatolaumiwa ila zigo hilo nina uhakika litamuangukia mtu! Maneno haya hayatopita kamwe... ni suala la muda tu! Kwani mababu wengi sana watapatikana mwaka huu...kama mlivokwishasikia! Wanaokumbuka vema...zamani kulikuwa na kina Profesa Vulata na..... hii leo wako wangapi wa aina ile?!! Ninachokubali mimi ni kuwa KWELI WATANZANIA WENGI WAGONJWA!!! NA UGONJWA WENYEWE UMEKAA SEHEMU MBAYA!! Huenda babu akafaniiwa KUwATIBIA!!!
 

Mkuuu, hili ni taifa la wapiga ramli, kuanzia kwa wakubwa hadi watoto wadogo. Hili suala la babu linatuvua nguo na kutuacha uchi kama taifa. Laiti ningeweza kuwa kinyonga kwa kubadili utaifa haraka. Totally frustrated..kuanzia babu mwenyewe, wagonjwa wake na viongozi wetu wote!
 
Use African solutions blessed with God to solve African problems.
...mkuu apo pana maana pana zaidi kuliko neno lenyewe!!! Lakini je ni nani analiona hilo???

Assume anatuambia ni EL au RA:::::::::::::::::::::::::::::::::::
Je nani atakataa na ashakunywa dawa ya babu Kinjekitile!! Kama hakuinywa yeye ni jamaa yake wa karibu... na ole wao watakaoenda kinyume na matakwa ya babu kwa mteule wake! Je hatowaambia kwamba wataota mikia wasipomchagua aliemsema?

Ndugu zangu.... HILI LA BABU NI KIPIMO TOSHA CHA AKILI ZETU NA MUSTAKABLIWA TANZANIA,... Leo hakuna anaekumbuka mgao wa umeme wala dowans, mfumko wa bei umesahaulika... watu hawafanyi kazi tena... wala hakuna anaekumbuka gongo la mboto wala maandamano na migomo.... SOTEEEE AKILI NA SHIDA ZETU LOLIONDO!!!
 

Hilo ndilo suala la msingi..Taifa zima halina akili!
 
Mkuu usishangae.... NI SIFA KWA TAIFA!!! Mbona hajatokea kwingine ila Tanzania? Mkuu mlima Kiimanjaro unapatikana Tanzania... na pale loliondo ndipo alipopatikana mwanadamu wa kale!!! Naogopa sana kusema apo mkuu... Kweli watu wanajua kupiga hesabu nchi hii!! BONGO!!! Ndio maana sishangai magazeti yanapoandika madaktari bingwa wamekutana na wagonjwa wao kwa babu yaaani!!! JAMANI KWELI WATANZANIA TUNAUMWA! Nadhani sasa itabidi atokee BIBI KUTUTIBIA!!!
 

Mkuu,
Harafu na wasiwasi na usalama wa babu, maana baada ya wagonjwa anaowatibu kutotibika wataamua kumvamia babu kwa ghadhabu. Ndio maana nasema wawachukue wangonjwa hospitalini na wawatume kwa babu na baada ya mda wawapime tena.

Hapo babu wanaweza mkamata, lakini pia yawezekana babu anatibu hataki tu ku delegate hiyo kazi kwa mtu mwingine/ wachawi na wanaojiita waganga wa kienyeji ndo wanatabia hiyo. Kama hakuna mtu anayemwamini atakufa na teknolojia yake ya kupaa na ungo bila kumrithisha yoyote.
 
Basi kama hujasema mimi nakusaidia kusema hivyo. Yaani tumekosa kiongozi wa kutuongoza hadi tunakuwa kama kondoo wanaoishi jangwani?
 
NI HERI TUNDELEE KUSEMA ILI IONEKANE TOFAUTI YA WAO NA SISI, KULIKO KUNYAMAZA TUKAONEKANA AFADHALI YA WAO KULIKO SISI! Ama wakatufananisha nao..... kweli Tanzania kuna wasomi kwa hili la babu NIMEAMINI!! Hatuna hata uthubutu wa kujiuliza KWANINI?
 
Basi kama hujasema mimi nakusaidia kusema hivyo. Yaani tumekosa kiongozi wa kutuongoza hadi tunakuwa kama kondoo wanaoishi jangwani?
...na bora umenisaidia kusema... ni bora kusema kuliko kunyamaza na hali mambo yanakwenda sivo ndivyo! Naamini kwa haya yanayoendelea ztatokea DOWANS nyingi na zote tutazilipa! Na kwa mfumo huuhuu Tanzania haitatoka katika lindi la MARADHI, UMASKINI, UJINGA, na UONGOZI DHAIFU! kwani raia imara hutoa viongozi shupavu na viongozi shupavu hujenga taifa bora!!

Amaa kweli TUMEDATA!! ndio maana wakati wa chaguzi matokeo ni tofauti na fikra za watu! kwa hili hatuna wa kumlaumu! nashawishika kuamini kinyume na fikra zangu!!!

TUMEKUWA KAMA PUNDA WA DOBI....
 

Mkuu,

Sina hamu na nchi hii. Mtoto analia, mama naye anaangua kilio na libaba nalo limeungana nao kulipua vilio!

We are totally doomed!!!

Ndo maana Jenarali anatusaidia hapa

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…