Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 7,899
- 10,415
Badala ya kukaa kuisubiri large scale LNG nakuomba waziri wa nishati na serikali tujikite kwenye small scale LNG na Mobile CNG station, miradi midogo ambayo inaweza kufanywa nasisi wenyewe bila kutegemea mitaji ya nje.
Ni ukweli usiopingika kwamba large scale LNGs zinachukua muda mrefu kutekelezwa pote duniani. Muda mwingine kuanzia miaka 5 na kuendelea. Na bado mkianza ujenzi wa large scale LNG mnachukua muda mrefu kukamilisha. Sio chini ya miaka minne kutokana na complexity ya miradi yenyewe.
Na hii inatokana na kwanza; fedha zinazohitajika kwenye ujenzi wa mradi kuwa nyingi kupita kipimo. Mfano huu mradi wetu unahitaji Trillion 68. Ni fedha nyingi kuzipata ni issue. Lazima kampuni kubwa za nje ziungane zichange ndio zipate hiyo fedha.
Lakini pia kuchelewa kwa makubaliano na maelewano ni sababu zingine.
Kwa large scale LNG watanzania hawawezi kujenga. Lakini kuna issue hii ya small scale LNG na mobile CNG (mobile CNG station) hii ni miradi midogo inayogharimu fedha kidogo ambazo hata matajiri wa Tanzania wanaweza kufanya.
Ninaiomba serikali itengeneze mchakato huu ili watanzania maeneo mbalimbali ya Tanzania waweze kuuziwa gesi asilia kwa matumizi mbalimbali kama kupikia, kwenye magari na viwandani.
Small scale LNG itawezesha kuisafirisha gesi kwenye mitungi midogo au kwenye tenka ambazo zitaweza kufika maeneo mbalimbali kisha kuihifadhi kwenye distribution terminals.
Halikadhalika mobile CNG (Mobile CNG station) hii itasaidia pia kuweza kuisafirisha gesi mikoa mbalimbali na kuwauzia watu ikiwa ndani ya tenka maalumu ambazo zitasambazwa mikoa mbalimbali. Gharama za kuendesha hii miradi zitakua ni ndogo sana kuliko kujenga mabomba ya kuifikisha gesi kwenye maeneo hayo.
Faida za hii miradi miwili yaani small scale LNG na mobile CNG stations.
Small scale LNG inachukua muda mfupi kutekelezwa na kuanza, pia inagharimu mtaji kidogo. Hivyo inaweza kufanywa na wazawa kwa kutumia fedha za ndani n.k.
Mobile CNG station inaweza kumfikia mteja hata mahali ambako hakuna main CNG non-mobile station. Itaokoa fedha nyingi. Badala ya kujenga vituo vya kujaza gesi kila mahali tutakua na vituo vichache tu ambavyo vitatumika kujaza gesi kwenye mobile CNG stations ambazo baada ya kujazwa zitasambaza gesi mahali mbalimbali Tanzania. Vituo hivyo (mobile CNG stations) ndio vitatumika kujaza gesi kwenye magari mbalimbali katika maeneo ambayo hayana non-mobile stations.
Ni mimi Meneja wa Makampuni
+25570110786788
Ahsanteni.
Kazi iendelee.
Ni ukweli usiopingika kwamba large scale LNGs zinachukua muda mrefu kutekelezwa pote duniani. Muda mwingine kuanzia miaka 5 na kuendelea. Na bado mkianza ujenzi wa large scale LNG mnachukua muda mrefu kukamilisha. Sio chini ya miaka minne kutokana na complexity ya miradi yenyewe.
Na hii inatokana na kwanza; fedha zinazohitajika kwenye ujenzi wa mradi kuwa nyingi kupita kipimo. Mfano huu mradi wetu unahitaji Trillion 68. Ni fedha nyingi kuzipata ni issue. Lazima kampuni kubwa za nje ziungane zichange ndio zipate hiyo fedha.
Lakini pia kuchelewa kwa makubaliano na maelewano ni sababu zingine.
Kwa large scale LNG watanzania hawawezi kujenga. Lakini kuna issue hii ya small scale LNG na mobile CNG (mobile CNG station) hii ni miradi midogo inayogharimu fedha kidogo ambazo hata matajiri wa Tanzania wanaweza kufanya.
Ninaiomba serikali itengeneze mchakato huu ili watanzania maeneo mbalimbali ya Tanzania waweze kuuziwa gesi asilia kwa matumizi mbalimbali kama kupikia, kwenye magari na viwandani.
Small scale LNG itawezesha kuisafirisha gesi kwenye mitungi midogo au kwenye tenka ambazo zitaweza kufika maeneo mbalimbali kisha kuihifadhi kwenye distribution terminals.
Halikadhalika mobile CNG (Mobile CNG station) hii itasaidia pia kuweza kuisafirisha gesi mikoa mbalimbali na kuwauzia watu ikiwa ndani ya tenka maalumu ambazo zitasambazwa mikoa mbalimbali. Gharama za kuendesha hii miradi zitakua ni ndogo sana kuliko kujenga mabomba ya kuifikisha gesi kwenye maeneo hayo.
Faida za hii miradi miwili yaani small scale LNG na mobile CNG stations.
Small scale LNG inachukua muda mfupi kutekelezwa na kuanza, pia inagharimu mtaji kidogo. Hivyo inaweza kufanywa na wazawa kwa kutumia fedha za ndani n.k.
Mobile CNG station inaweza kumfikia mteja hata mahali ambako hakuna main CNG non-mobile station. Itaokoa fedha nyingi. Badala ya kujenga vituo vya kujaza gesi kila mahali tutakua na vituo vichache tu ambavyo vitatumika kujaza gesi kwenye mobile CNG stations ambazo baada ya kujazwa zitasambaza gesi mahali mbalimbali Tanzania. Vituo hivyo (mobile CNG stations) ndio vitatumika kujaza gesi kwenye magari mbalimbali katika maeneo ambayo hayana non-mobile stations.
Ni mimi Meneja wa Makampuni
+25570110786788
Ahsanteni.
Kazi iendelee.