Nilikuwa sijui kama kuna za kunde pia, lakini nilishawahi kula mahali zilikuwa tamu kuliko kawaida nadhani ndiyo hizo za kunde.
Mie nnavojua ni badia... za kunde tamu zaidi BAK...kwa chatne ya nazi au hiyo ya embe mbichi weee utamu hadi machoni lol...
Naomba nisaidie vitu vifuatavyo vyaitwaje in English:1)Kunde.... (za kupaaza) kg 1/2
2)pilipili mboga 1/2..
3)kitunguu maji 1/2.
4)kitunguu saumu 1/2teaspoon
5) chumvi kiasi....
6)baking powder/hamira 1tablespoon
7)mafuta ya kupikia
8)kotmiri/giligilani
Namna ya kutaarisha
1)roweka kunde for 4 hours
2)weka kwenye blender ama food processor bila ya kutia maji then weka pilipili mboga,kitunguu maji, saumu na chumvi na kotmiri/giligilani
3)tia baking powder/hamira kwenye mchanganyiko wako
4) weka mafuta kwenye karai na ukaange badia zako kwa kutengeneza viduara vidogo vidogo
5)kaanga hadi ziwe brown..weka moto mdogo mdogo ili ziwive vizuri ndani...
Badia tayari kwa kuliwa....
hata mi naona inalika lakini?
ha ha ha halafu hukomi bado umekomaa nayo tu...Ukienda msalani si ndoo balaaa!!Ukila uwe na glass na maji pembeni au maziwa lol..
Wenzio humu ndani kutwa twaasumbuliwa na heartburn kwa mapilipili lol...
Wewe bidada mimi maneno yako tuu yananiachaga hoi na kunifanya nijione sifahamu kiswahili fasaha. Maana mara badia, uzile, thomu n.k ukijumlisha na mahanjumati unayoyawekaga ndio kabisaa nabaki hoi.
Naomba nisaidie vitu vifuatavyo vyaitwaje in English:
Kunde (za kupaa/za lubya)
Dengu
Choroko
Mbaazi
Gilgiliani
Pilipili manga
ha ha ha halafu hukomi bado umekomaa nayo tu...Ukienda msalani si ndoo balaaa!!
Choroko-Mung beansWajua vizuri kiswahili...ila kuna viswahili vingi hapo kila mtu ana chake wewe ukiwa hufahamu kitu uliza wengine watakusaidia kiswahili ambacho wewe utaelewa...mfano shosti mimi49..
Choroko-Mung beans
Giligilani-coriander
Mbaazi-Black eyed beans
Kunde-Adzuki beans
Dengu-Split chickpeas
Pilipili manga-black pepper
Yeah si watu wote wamezoea ladha yake!Mimi49 waujua mvuje? Mimi kutia kwenye badia vijani vyake...ila wengi hawapendi
Yeah si watu wote wamezoea ladha yake!
1)Kunde.... (za kupaaza) kg 1/2
2)pilipili mboga 1/2..
3)kitunguu maji 1/2.
4)kitunguu saumu 1/2teaspoon
5) chumvi kiasi....
6)baking powder/hamira 1tablespoon
7)mafuta ya kupikia
8)kotmiri/giligilani
Namna ya kutaarisha
1)roweka kunde for 4 hours
2)weka kwenye blender ama food processor bila ya kutia maji then weka pilipili mboga,kitunguu maji, saumu na chumvi na kotmiri/giligilani
3)tia baking powder/hamira kwenye mchanganyiko wako
4) weka mafuta kwenye karai na ukaange badia zako kwa kutengeneza viduara vidogo vidogo
5)kaanga hadi ziwe brown..weka moto mdogo mdogo ili ziwive vizuri ndani...
Badia tayari kwa kuliwa....
Hivi wewe ni wa Mvita au wa Amu
Nimependa lafidhi yako.
Sijaelewa bado....
Nimeona kiswahili chako ni kama cha Mombasa (Mvita) au Lamu (Amu).
Hasa kama ulizitia viungo vingiYeah alafu za dengu zikilala zawa mbayaa...