Badia za kunde

Badia za kunde

1)Kunde.... (za kupaaza) kg 1/2
2)pilipili mboga 1/2..
3)kitunguu maji 1/2.
4)kitunguu saumu 1/2teaspoon
5) chumvi kiasi....
6)baking powder/hamira 1tablespoon
7)mafuta ya kupikia
8)kotmiri/giligilani
Namna ya kutaarisha

1)roweka kunde for 4 hours
2)weka kwenye blender ama food processor bila ya kutia maji then weka pilipili mboga,kitunguu maji, saumu na chumvi na kotmiri/giligilani
3)tia baking powder/hamira kwenye mchanganyiko wako

4) weka mafuta kwenye karai na ukaange badia zako kwa kutengeneza viduara vidogo vidogo
5)kaanga hadi ziwe brown..weka moto mdogo mdogo ili ziwive vizuri ndani...

Badia tayari kwa kuliwa....
aiseee haya maakuli ni hatari tupu kudos..
 
Hizi ndo tamu, kuliko zile za dengu. Weekend ijayo itakuwa ya kujaribu mapishi yako kadhaa likiwemo hili. Ntakuonjesha mpishi mkuu unipe alama za ufaulu.

Hhahahaahaha sawa ahsantee....
 
  • Thanks
Reactions: bht
Unajua kuna baadhi ya maneno matamshi yake yanatofautiana kati ya Zenj na Tanganyika. Huku Bara tunaziita bajia. Kuna neno kama swali, Zenj ni suali. Sikulielewa swali/suali lako?

Mie nnavojua ni badia... za kunde tamu zaidi BAK...kwa chatne ya nazi au hiyo ya embe mbichi weee utamu hadi machoni lol...
 
Unajua kuna baadhi ya maneno matamshi yake yanatofautiana kati ya Zenj na Tanganyika. Huku Bara tunaziita bajia. Kuna neno kama swali, Zenj ni suali. Sikulielewa swali/suali lako?


Yeah ni kweli ila walau tunaelewana mfano kaimati nyinyi mwaita kalimati........
 
Unajua kuna baadhi ya maneno matamshi yake yanatofautiana kati ya Zenj na Tanganyika. Huku Bara tunaziita bajia. Kuna neno kama swali, Zenj ni suali. Sikulielewa swali/suali lako?

Besti...bajia kihindi zaidi...lol
 
Hahha kaenjoy sana na mifuko imejaa saiv zote anaweka kwenye kibubu cha mchumba...lol


Heee zitimie hiyo billion aloambiwa aleteee ila tu msije kutwambia tulendr mahari sie tupo tz mama eeeeh sheria hiyo mwisho bombay lol
 
Best nafahamu kwamba Badia ni neno la kihindi ambalo limekuwa adopted na Kiswahili kama yalivyo maneno mengine ya kihindi chai, lakini n.k. ila kuna tofauti ya matamshi kati ya bara na visiwani. Visiwani linatamkwa kama wanavyolitamka wenyewe wahindi na bara linatamkwa Bajia. Mzima lakini Best? usipotee hivyo banaaa!?

Besti...bajia kihindi zaidi...lol
 
Best nafahamu kwamba Badia ni neno la kidindi ambalo limekuwa adopted na Kiswahili kama yalivyo maneno mengine ya kihindi chai, lakini n.k. ila kuna tofauti ya matamshi kati ya bara na visiwani. Visiwani linatamkwa kama wanavyolitamka wenyewe wahindi na bara linatamkwa Bajia. Mzima lakini Best? usipotee hivyo banaaa!?

Mie mzima wa afya nashkuru. Sijapotea kiivyo besti majukumu tuu ...saivi nategemea mahanjumati ya eid yatawekwa sana na jaanu farkhina kwahio tutakutana jikoni. .lol
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Nafurahi kusikia umzima wa afya, Mungu ashukuriwe. Haya ngoja tusubiri mahanjumati ya Eid toka kwa Jaanu farkhina, mie jikoni kuzuka kama kawa maana huko ndio kunakochangia sana afya na uhai wetu.

Mie mzima wa afya nashkuru. Sijapotea kiivyo besti majukumu tuu ...saivi nategemea mahanjumati ya eid yatawekwa sana na jaanu farkhina kwahio tutakutana jikoni. .lol
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom