Habarini za asubuhi wana jf, bila shaka mmmeamka salama hongereni kwa majukumu ya siku, kama mnavyokumbuka kuna kipindi nilileta mada kuhusu huyu workmate ambae ni mke wa mtu, samahani kwa wale nitakaowakwaza juu ya hili, nilijaribu kufuata ushauri wenu jinsi ya kumuepuka ila naona ni kama imeshindikana, nikimsalimia hivi hivi juu juu nikampita, analazimisha hug, sometmes hata kiss, nikisema nimnunie wapi, mara anaulize sijui una tatizo gani, mbona upo hivyo, tukiongea huwa naleta mazungumzo kuhusu mumewe, { ingawa simfahamu kihiivyo} anakuja juu na kuwa mkali, na kuniambia mabo ya mumewe hayanihusu,
Dhumuni la kuleta hapa hata mimi sifurahishwi na hili jambo, naogopa kumweleza, sijui atalipokeaje, hata nikiongea na simu au akiona sms kwenye simu yangu, lazima aniulize, anafatilia kuhusu jinsi nimevaaje, sijui nywele zimekua, punguza ndevu na ishu kama hizo, narudia tena, samahani kwa wale nitakaowakwaza, naombeni mnishauri jinsi kutoka kwenye huu mtego, naamini hunu kuna kila aina ya watu, wenye ufahamu mkubwa, wa kati na mdogo, karibuni napokea mawazo yenu yote.
ahsanteni sana