Bado natafakari kifungo cha jela si adhabu stahiki na rekebu

Bado natafakari kifungo cha jela si adhabu stahiki na rekebu

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2016
Posts
14,311
Reaction score
36,056
Heri ya mwaka 2024 walimwengu

Mwaka huu umeingia nikiwa natafakari mambo kivingine hasa hili la kuwafungia watu wazima sehemu moja (jela) bila kujali wamefanya makosa gani, yaani adhabu ni moja kwa watu waliofanya makosa tofauti tofauti.

Kwanini tuwaweke wahalifu ndani? tuna waogopa? wametuzidi akili? hatuna kingine bora cha kuwafanyia? kwani mababu zetu kabla ya kuja wakoloni walikua wanafanyaje?

Mathalani mtu ameiba, kwanini tusichukue hicho alichoiba alafu tumnyang'anye na alicho nacho ili aanze upya na aendelee na shughuli nyingine?

au mtu amebaka katumia vibaya viugo vyake vya siri kwanini tusivikate aachwe anendelee na shughuli zake nyingine?

au mtu ameua yaani katoa roho ya mtu mwingine kwanini tuitoe roho yake chap alafu tuendelee na shughuli zetu nyingine?

Wazo la kuwakusanya waalifu sehemu moja ni wazo fikirishi na ni la hatari, hatuombi litokee jambo baya lakini natafakari tu siki likitokea lakutokea hao watu wakaingia mtaani kwa njia isiyo rasmi

Si vibaya tukijitafakarisha mambo ya kikubwa mwaka huu 2024
 
Nimejaribu kuwaza akili yako inawaza nini , nimekuelewa vyema unahoja ya msingi mkuu , ila kuna hukumu zingine ni kama umetumia Hasira kuwaza
 
Nimejaribu kuwaza akili yako inawaza nini , nimekuelewa vyema unahoja ya msingi mkuu , ila kuna hukumu zingine ni kama umetumia Hasira kuwaza
Tuendelee kutafakari mkuu
 
Umewaza kama mimi,kiukweli kukaa kwenye kuta za pembe nne usiombe


Una hoja usikilizwe
 
Back
Top Bottom