Bado sielewi imekuwa kuwaje hadi Haji Manara akawa shabiki wa Simba

Hakuna ushabiki wa mpira wa kurithi,

Narudia tena haupo,

Ushabiki wa mpira unakuja automatically tu,

Ukitaka kuhakikisha hili concetrate kwenye machi timu usizozitambua hata kidogo,

Automatically unajikuta unaupenda upande fulani bila kushurutishwa,

Kwahiyo inawezekana kabisa familia nzima kuwa yangu au simba mtoto akawa opposite

Nimekua katika familia wakishabikia timu tofauti na mimi nashabikia timu tofauti.

Refer watoto wa CR7 na MESSI
 
Hivi inakuwaje mtu anarithi ushabiki kutoka kwa wazazi??? Nafikiri mshabiki wa mpira ni hali mtu anakuwa nayo yy mwenyewe kutoka moyoni bila kushawishiwa na mtu... Yani ni kama kumpenda mke mwema... Yani it comes naturally yani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeoa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unafananisha mafuta ya taa na maji..

Mpira sio imani ya dini bali ni mapenzi binafsi ya mtu.

Mi baba yangu Yanga damu na nikiwa mdogo nishanunuliwa jezi za njano za yanga na mzee alifanya kila aliwezalo watoto wake wote waipende yanga lakini mwisho wa siku mi ni shabiki wa simba maana kwa mapenzi yangu binafsi nilivutiwa na simba...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cha ajabu hapa hakuna hata mmoja anayelipia fee yake ya uanachama huko Simba/Yanga ila wote mnasema mnazipenda hizo timu.

Tofauti kati ya Mpenzi vs Mshabiki inabidi iwekwe bayana.
Sio kila timu unamfumo was mchango. Barcelona anao, Arsenal hana. Simba na Yanga wanao, Kagera Sugar hana.
 
Kwa mujibu wa Haji Manara mwenyewe, amelelewa na babu yake pia. Babu yake alikuwa Mwenyekiti wa Simba.

Ukiwa huyaelewi mapenzi na wasta (influence) ya babu kwa mjukuu anaemlea utakuwa mchawi.
 
Basi wewe unashida, sisi wengine tunachagua wenyewe kipi tukipende kipi tukiache. Mzee wangu hata sijui you team gani pamba au meko.

Ila mimi ni shabiki wa simba ninayetumia akili siyo wale lialia, kwenye ukweli yeye anabisha tu.

Hata mke nachagua mwenyewe!

Kwa kifupi mimi ni "team sipangiwi"
 
Tofauti ..unajua Beckham kwao London..Manchester alienda kucheza mpira tu...probably child hood timu yake sio Manchester United...hivyo Becs ni Arsenal ndio maana mtoto kashindwa kujificha..Haji kacheza mpaka Yanga kids ni fursa za maisha tu...
 
Baba ako hakuwa shabiki kindakindaki wa mpira ..angekuwa shabiki wa mpira haswa haswa lazima ungefuata timu yake tu...but kwakuwa hakuwa na interest yoyote na mpira obviously lazima ungefuata timu yake
 
Humfuatilii haji ndo maana umekuja kuandika upupu.kashaeleza mara kadhaa na baba yake kashaelezea.muwe mnaangalia hata interviews youtube kabla ya kuandika.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuwa mchezaji wa yanga hakumfanyia baba wa haji kuwa yanga kun aguero ni shabiki kidaki wa liverpool lakin hiyo haimfanyi asiifungie mancity ili liverpool awe bingwa!!unaweza kukuta haji babake amekua shabiki wa wa yanga kwasababu kachezea yanga tu...
 
At least I under
Kwa mujibu wa Haji Manara mwenyewe, amelelewa na babu yake pia. Babu yake alikuwa Mwenyekiti wa Simba.

Ukiwa huyaelewi mapenzi na wasta (influence) ya babu kwa mjukuu anaemlea utakuwa mchawi.
At least I understand now kumbe alilelewa na babu? I was so confused . Thanx for unconfusiding me
 
Kwani baba au mama yako akiwa Mwizi na mtoto lazima awe hivyo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…