Bajaji hazipaswi kabisa kusafirisha abiria barabara kuu

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Bajaji zililetwa kama usafiri wa walemavu. Baadaye zikaruhusiwa kusafirisha abiria kutoka maeneo ya pembezoni kuja barabara kuu. Leo hii sehemu nyingi zimegeuka usafiri barabara kuu.

Na hili ni baada ya wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakuu wa polisi kuona ni biashara nzuri na kuianza. Haingii kabisa akilini kupiga marufuku hiace na kuruhusu bajaji. Miji imeharibika kabisa. Huko Mbeya na Iringa ni vurugu tupu.

Wanasiasa na viongozi ndiyo huwa wa kwanza kuharibu taratibu, hii habari ya Bajaji barabara kuu iangaliwe upya kabla hatujafika sehemu tukashindwa kudhibiti.

Maana mwisho wake ni usafiri mzuri kama Costa zitaondoka barabarani na miji ikawa vurugu tupu.
 
Hapa Tunduma

Ni balaa
 
bajaji zilianza tokea amita bachani labda huku tanzania ilipokelewa vibaya
 
MPWA ENDELEA KUMWAGILIA MOYO

YANGA 3 HUKOO

UGALI WA WENZIO ADA UTAWASOMESHA WWEWEWATOTO ZAO
 
Wakati huo namimi najipanga kuingiza cha kwangu njiani aseee
 
Msituchoshe siyo kila mtu anataka kubananaw kwenye mwendokasi
 
Mnapanda hizo bajaji,ndomaana zinazidi kutamalaki,acheni kupanda muone kama hazitapungua
 
Mtuache wapanda bajaji, sio wote tunaweza kununua magari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…