Bajeti Mbadala Ya Upinzani 2008/2009.

Bajeti Mbadala Ya Upinzani 2008/2009.

Lakini wewe si umesema sisi hatutakiwi kuwa Omba Omba? Sasa tuombe zaidi tena kivipi?

Na sisi tukija kuombwa tutoe?

hatutakiwi tuwe-omba omba kwa vile tuna rasilimali nyingi ambazo kama zingetumiwa vizuri tungejitosheleza. Tukiombwa inafaa wewe ndio utoe kwa niaba yetu, tena toa tu kwa moyo mkunjufu ndio uzalendo wenyewe huo.
 
hatutakiwi tuwe-omba omba kwa vile tuna rasilimali nyingi ambazo kama zingetumiwa vizuri tungejitosheleza. Tukiombwa inafaa wewe ndio utoe kwa niaba yetu, tena toa tu kwa moyo mkunjufu ndio uzalendo wenyewe huo.

Ndio maana napinga huu mpango mzima wa kuomba na kupeana misaada. Wewe unataka tuendelee kuomba lakini kutoa hutaki!
 
Ndio maana napinga huu mpango mzima wa kuomba na kupeana misaada. Wewe unataka tuendelee kuomba lakini kutoa hutaki!

sitaki kabisa suala la kuomba, nalipiga vita kwa vile hakuna sababu ya kupelekea kufanya hivyo. Ila wewe kama wajisikia kutoa toa tu, tena kwa kila mtanzania, ungesaidia kupunguza ugumu wa maisha wa wenye maisha magumu.
 
sitaki kabisa suala la kuomba, nalipiga vita kwa vile hakuna sababu ya kupelekea kufanya hivyo. Ila wewe kama wajisikia kutoa toa tu, tena kwa kila mtanzania, ungesaidia kupunguza ugumu wa maisha wa wenye maisha magumu.

Kama sasa unapiga vita kuomba tuko wote katika kukataa kuomba na kupeana. Hii itakuondolea presha ya kutakwa kutoa kama nchi na Mwananchi.
 
Kama sasa unapiga vita kuomba tuko wote katika kukataa kuomba na kupeana. Hii itakuondolea presha ya kutakwa kutoa kama nchi na Mwananchi.

mimi nawasecond wote wanaopenda kutoa, hivyo toa tu, ninachogomba hapa ni suala zima la kuomba, Tanzania hatutakiwi kuomba kabisaaaaa
 
mimi nawasecond wote wanaopenda kutoa, hivyo toa tu, ninachogomba hapa ni suala zima la kuomba, Tanzania hatutakiwi kuomba kabisaaaaa

Nadhani ni kweli nchi yetu ina rasilimali, na tujifunze kujitegemea bila kuomba misaada Magharibi.

Mla mbuzi hulipa ng'ombe. Ndio maana sitaki upewe pewe vinono, usije kuja lipishwa.
 
Nadhani ni kweli nchi yetu ina rasilimali, na tujifunze kujitegemea bila kuomba misaada Magharibi.

Mla mbuzi hulipa ng'ombe. Ndio maana sitaki upewe pewe vinono, usije kuja lipishwa.

mimi kupewa napewa alhamdulillah- na kulipa silipi kwa vile napewa kiungwana na kwa dhati kabisa, ila kuomba ndio siombi na pia kutoa sitoi kwa vile sina cha kutoa.
 
hakuna sababu zinazolazimisha bajeti ya upinzani kuwa ndogo kuliko ya serikali. if the money is needed is needed hamna ulazima wa kusema wapunguze iwe chini ya serikali kwa kuwa tu wataonekana wema kwa wananchi.
serikali imetoa fungu dogo katika sehemu nyeti kama miundo mbinu na elimu. hivi bila ya miundo mbinu nchi itaendelea kweli?
tanzania pesa ipo, na kama ingekuwa haipo isingechotwa namna kama vile kwenye EPA. zile pesa za EPA hivi ni asilimia ngapi ya pesa za bajeti iliyotolewa na serikali? na huo ni mfano mdogo tu. tukija kwenye richmond na kiwira ....tutakuta asilimia kubwa ya pesa zinazohitajika kwenye bajeti zinaenda kwenye mikono ya mafisadi bila ya sababu za msingi
 
Ni kuwa wapinzani wameonyesha vyanzo vipya vya mapato ,ndio maana wameweza kuwa na fedha nyingi kuliko serikiali.

Ukisoma revenue book utaona kuwa kuna mapungufu makubwa sana kwenye hotuba ya serikali
 
9. Mhe. Spika, naomba nitumie fursa hii fupi kuwakumbusha tena Watanzania kupitia Bunge lako Tukufu, kuwa tokea Nchi yetu ipate Uhuru (Tanganyika) 1961 kukawa na “Republic of Tanganyika” na baada ya Mapinduzi (Zanzibar) 1964, kukawa na “People’s Republic of Zanzibar” na hatimaye Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Nchi yetu imeongozwa na TANU na ASP na Hatimaye CCM. Hivyo ni dhahiri kuwa mafanikio na mapungufu yote ya maendeleo ya Nchi yetu yametokana na Uongozi na Sera za CCM.

10. Mhe. Spika ni wajibu wetu sote kujiuliza, katika kipindi hichi chote cha uongozi wa Chama kimoja. Je sera zilizokuwepo, Mtanzania wa kawaida maisha yake yameboreka?


Haya ni ni baadhi ya maneno ambayo watanzania wanatakiwa kuyajua.
 
Sehemu nilioipenda ni ile ya kuweka kodi kwa mapato ya watumishi wakati wa warsha semina na kadhalika.
pia kupunguza road licence!!
 
Yaani kweli mie ni Maimuna, nilikuwa sijui wabunge hawakatwi kodi kwenye pesa zao. Jamani ni nchi gani hii, mnapiga kelele na kodi kumbe nyie mnapata mtelemko. Mmh nchi bila kodi............
 
halafu watapitisha baadhi ya mishahara ya makampuni binafsi ikatwe paye ya 30%
 
Ni kweli maisha hayajaboreka,watu tunakufa na njaa kwa sababu ya watu wachache kula na kusaza wakiwa katika makasri yao huku wakidai ni vijisenti tu kwa level zao.
 
Ni kweli Fidel80, unachokisema ni sahihi.Na inaonekana wapinzani kweli wanawazo mbadala katika kuikomboa nchi hii.Vipaumbele vyao ndio hasa VIMENIKOSHA ROHO.
 
Haya maneno ni mazito sana na yanaonyesha hali halisi inayomkabili mtanzania wa kawaida. Assume mtu yuko kijijini ni Mkulima si wameisha sahau mafuta. Halafu huku Bongo viongozi wakiendeleza ufisadi? Nafikiri mwaka huu kama alivyosema PM Mawaziri wanaweza kupata kazi tena ya kuzomewa.

56. Mheshimiwa Spika, Inaeleweka kuwa sehemu kubwa ya mapato ya bidhaa zinazoagiziwa kutoka nje zinatokana na bidhaa za Petroli na Mafuta. Serikali imeweka viwango vya kodi katika mafuta vya juu hivyo kufanya gharama za usafiri wa abiria na bidhaa kuwa kubwa na kumuongezea mzigo Mtanzania anayeishi kijijini na kuyafanya maisha yake kuwa magumu zaidi. Kwa mfano kodi zote kwa jumla katika Petroli ni Tshs 545.10 kwa lita na kwa dizeli Tshs. 520.80 kwa lita. (Bei za mafuta ya dizeli kwa makao makuu ya mikao kwa tarehe 16-31 Mei 2008 ilikuwa kama ifuatavyo kwenye baadhi ya mikoa, Dar es salaam 1,654.09 petrol na 1,884.89 kwa dizeli kwa lita huku mafuta ya taa yakiwa 1,488.24 kwa lita, Kagera 1,748.93 petrol na 1,979.73 kwa dizeli kwa lita huku mafuta ya taa yakiwa 1,583.08 kwa lita, Kigoma 1,930 petrol na 2,080 dizeli kwa lita huku mafuta ya taa 1,550 kwa lita na hali katika mkoa wa Mbeya 1,850 petrol na 2,000 dizeli kwa lita huku mafuta ya taa 1,500 kwa lita) . kati ya wastani wa bei ya 1800/- kwa lita. Hizi ni bei za mijiji, vijijini ambako kuna umasikini uliokithiri na mahitaji ya nishati kwa ajili ya usafiri,kilimo n.k. wastani wa bei ni Tshs.2,200 kwa lita.
 
Hili swali linafurahisha sana

Hata hivyo Waziri alieleza kuwa "Kwa magari yenye ujazo wa injini unaozidi 5,000cc kiwango cha ada kitakuwa shilingi 100,000 kwa mwaka. Haya ni magari ya mizigo na mabasi ya abiria." Mwaka huu Waziri anaeleza kuwa magari yenye ujazo wa injini unaozidi cc5000 yamepunguziwa kiwango cha ada kutoka shilingi 175,000 hadi shilingi 150,000. Ikiwa mwaka jana Waziri alilieleza Bunge kiwango cha ada kiwe shilingi 100000/-, mwaka huu anapendekeza kiwe shilingi 150,000/-. Je hili ni ongezeko au punguzo.?
 
UFISADI KILA MAHALI

i. Halmashauri za Wilaya zilizo katika maeneo ambayo bidhaa hizi zinapatikana ziwe mawakala wa kukusanya mapato kutokana na bidhaa za maliasili. Uamuzi huu utapunguza kwa kiasi kikubwa ufisadi uliopo sasa katika Wizara ya Maliasili. Kila Halmashauri inayokusanya kodi ipatiwe gawio kutoka sehemu ya makusanyo;
 
Bajeti ya wapinzania hata ya mwaka jana ilikuwa imesoma shule sana. Lakini kuna watu wanaendelea kuwaaminisha watanzania kwamba wapinzani bado hawawezi kutawala!
 
Back
Top Bottom