BAKITA acheni upotoshaji, Decoder ni King’amuzi, Transmitter ni Kisimbuzi

BAKITA acheni upotoshaji, Decoder ni King’amuzi, Transmitter ni Kisimbuzi

C&P
Tunapohama kutoka analojia kwenda digiti neno 'king'amuzi' limeshamiri sana. Ndipo majuzi kupitia Radio One kwenye kipindi cha lugha ya kiswahili Jumamosi waendesha kipindi wakawa wanajadili haya.

King'amuzi ni detector. Mfano vile vibao vinavyotumika kupapasia sehemu za vizuizi na kwenye maofisi ni ving'amuzi. Vinang'amua uwepo wa kitu kisicho cha kawaida na ndio maana vinatoa mlio.

Decoder (codec)-code-decode ni kutafsiri toka mfumo mmoja kwenda mwingine mfano mawimbi ya analojia kwenda digiti. Na kiswahili chake kutokana na wataalam ni kisimbuzi. Linatokana na neno 'simba'-ficha. Halafu 'simbua'. Hivyo kifaa cha kusimbua kuitwa kisimbuzi.

Tusibanange lugha yaeu adhimu kwa hisia binafsi..., tuiache BAKITA waliokabidhiwa jukumu hilo lituongoze kwa kuzingatia mawazo ya wengi.
Ndugu yangu, kwanini mnalazimisha vitu ambavyo vipo wazi? ‘Detector’ au (‘Identifier’) maana yake ni ‘Kitambuzi’, yaani kinauweza wa kutambua kama hii ni dhahabu halisi au sio halisi, maana yake kina ‘detect’ (identify), kudetect (Identify) ni ‘Kutambua’ , hivyo ‘Detector’ ni ‘Kitambuzi’; hicho kipindi sikukisikia, ningesikia ningewavamia studio kama makonda alivyofanya
 
Hao jamaa huwa wanatunga maneno tu, hawayahusishi na kifaa husika, hata kiingereza kililazimika kuchukua maneno ya lugha nyingine, mambo ya kupandikiziana maneno, ambayo baadae saiti "yanakataliwa" kwa kuwa hayatumiki
 
Hao jamaa huwa wanatunga maneno tu, hawayahusishi na kifaa husika, hata kiingereza kililazimika kuchukua maneno ya lugha nyingine, mambo ya kupandikiziana maneno, ambayo baadae saiti "yanakataliwa" kwa kuwa hayatumiki
Ni vyema maneno yakaazimwa toka lugha nyingine na kutoholewa kidogo Ili yaendane na kiswahili, kuliko kutunga neno jipya kabisa from nowhere
 
Nimeshangaa kusikia eti wanaojiita wataalam wa Kiswahili wakisema kwamba Tafsiri ya neno ‘Decoder’ ni ‘Kisimbuzi’, huo ni uongo wa wazi kabisa.

‘King’amuzi’ ni neno lililonyumbuliwa kutoka kwenye neno ‘ng’amua’ , kung’amua maana yake ni ‘Ku-decode’ , na hivyo kitu kinachofanya hiyo kazi ya ‘Ku-decode’ ndio kinaitwa ‘Decoder’, kwa kiswahili ni ‘King’amuzi’.

‘Kisimbuzi’ ni neno lililonyumbulishwa kimtambuka zaidi kutoka kwenye neno ‘Sambaza’ , kusambaza maana yake ni ‘Ku-transmit’ (au spread , mfano Ku-spread radiowaves) , na hivyo kitu kinachofanya kazi ya ‘Ku-transmit’ ndio kinaitwa ‘ Transmitter’ , Kwa kiswahili ni ‘Kisambazaji’ au kwa neno lililotoholewa ili matamshi yawe mazuri ndio tunaita ‘Kisimbuzi’ badala ya ‘Kisambazaji’.

Huko BAKITA wamejaa vilaza sanaView attachment 2559159
Hii ni Transmitter (Kisambazaji / Kisimbuzi) kinachosambaza mawimbi ya Radio)

View attachment 2559161
Hiki ndio king’amuzi kinachofanya kazi ya kung’amua (decode) mawimbi yaliyotumwa na Kisimbuzi na kisha kupokelewa na dish ili kupeleka taarifa sahihi za video na sauti kwenda kwenye screen na spika za TV.
Safi sana,yaani wao ndio wenye kiswahili chao lakini hawakijui hadi sisi tunakuwa kifimbo cheza wao.

Wamekalia kurekebisha.misemo ya kijinga tu kama vile Famasihara,vingine kumbe ni weupe
 
Nimeshangaa kusikia eti wanaojiita wataalam wa Kiswahili wakisema kwamba Tafsiri ya neno ‘Decoder’ ni ‘Kisimbuzi’, huo ni uongo wa wazi kabisa.

‘King’amuzi’ ni neno lililonyumbuliwa kutoka kwenye neno ‘ng’amua’ , kung’amua maana yake ni ‘Ku-decode’ , na hivyo kitu kinachofanya hiyo kazi ya ‘Ku-decode’ ndio kinaitwa ‘Decoder’, kwa kiswahili ni ‘King’amuzi’.

‘Kisimbuzi’ ni neno lililonyumbulishwa kimtambuka zaidi kutoka kwenye neno ‘Sambaza’ , kusambaza maana yake ni ‘Ku-transmit’ (au spread , mfano Ku-spread radiowaves) , na hivyo kitu kinachofanya kazi ya ‘Ku-transmit’ ndio kinaitwa ‘ Transmitter’ , Kwa kiswahili ni ‘Kisambazaji’ au kwa neno lililotoholewa ili matamshi yawe mazuri ndio tunaita ‘Kisimbuzi’ badala ya ‘Kisambazaji’.

Huko BAKITA wamejaa vilaza sanaView attachment 2559159
Hii ni Transmitter (Kisambazaji / Kisimbuzi) kinachosambaza mawimbi ya Radio)

View attachment 2559161
Hiki ndio king’amuzi kinachofanya kazi ya kung’amua (decode) mawimbi yaliyotumwa na Kisimbuzi na kisha kupokelewa na dish ili kupeleka taarifa sahihi za video na sauti kwenda kwenye screen na spika za TV.
Wewe umetoa wapi hii, kama huna elimu ukae kimya uliza wenye elimu tutakuelezea, mtaalamu wa Computer Science nitakuchambulia kwamba BAKITA walikuwa sahihi.

DECODER
Neno decorder imetokana muungamiko wa maneno mawili yaani DE-CODE ambapo CODE ni msimbo kwa kiswahili. Ku DE-CODE ni kubadilisha data kutoka mfumo wa CODE, kwenda NON CODE, mfumo rahisi wa taarifa kupokelewa na TV Zetu. (Ni kama Decryption technique) Hivyo neno KISIMBUZI nineno sahihi kwa maana kina simbua msimbo, ambapo ni rahisi mawimbi hayo kutambuliwa na TV zetu na kudisplay kwenye screen.

DETECTOR
Kitambuzi/King'amuzi ni kifaa kinachotimika kutambua uwepo wa kitu ama metal ama vitu vilivyo fichwa, mfano sensor zinazotumika kwenye mageti ya walinzi kwenye kumbi za starehe maofisini, zipo pia metal detector zinazotumika kutambua uwepo wa madini ya aina mbalimbali, hivyo hutumika migodini.

TRANSMITER
Hii hutafsiriwa kama "Kituma ishara" kifaa hiki hutumika kutuma na kubadili taarifa kutoka mfumo wa umeme kuwa katika mfumo wa mawimbi ya kielectomagnetic, hivyo kuwezesha taarifa kusambaa pasina kuunganishwa kwa njia ya waya. Taarifa za aina hii ni kama mawimbi ya mawasiliano ya redio na simu za mkononi.

Kwaufupi.
Kisimbuzi ni kifaa maalumu kinachotumika kusimbua misimbo fiche (encrypted codes), na kubadili taarifa kuwa katika mfumo rahisi unaoweza kutambulika na kutumika na TV zetu ( from coded form to non-coded form). King'amuzi (detector) ni kifaa maalum kinachotumika kutambua uwepo wa vitu vilivyofichika mfano chuma, na madini mengine.
 
Wewe umetoa wapi hii, kama huna elimu ukae kimya uliza wenye elimu tutakuelezea, mtaalamu wa Computer Science nitakuchambulia kwamba BAKITA walikuwa sahihi.

DECODER
Neno decorder imetokana muungamiko wa maneno mawili yaani DE-CODE ambapo CODE ni msimbo kwa kiswahili. Ku DE-CODE ni kubadilisha data kutoka mfumo wa CODE, kwenda NON CODE, mfumo rahisi wa taarifa kupokelewa na TV Zetu. (Ni kama Decryption technique) Hivyo neno KISIMBUZI nineno sahihi kwa maana kina simbua msimbo, ambapo ni rahisi mawimbi hayo kutambuliwa na TV zetu na kudisplay kwenye screen.

DETECTOR
Kitambuzi/King'amuzi ni kifaa kinachotimika kutambua uwepo wa kitu ama metal ama vitu vilivyo fichwa, mfano sensor zinazotumika kwenye mageti ya walinzi kwenye kumbi za starehe maofisini, zipo pia metal detector zinazotumika kutambua uwepo wa madini ya aina mbalimbali, hivyo hutumika migodini.

TRANSMITER
Hii hutafsiriwa kama "Kituma ishara" kifaa hiki hutumika kutuma na kubadili taarifa kutoka mfumo wa umeme kuwa katika mfumo wa mawimbi ya kielectomagnetic, hivyo kuwezesha taarifa kusambaa pasina kuunganishwa kwa njia ya waya. Taarifa za aina hii ni kama mawimbi ya mawasiliano ya redio na simu za mkononi.

Kwaufupi.
Kisimbuzi ni kifaa maalumu kinachotumika kusimbua misimbo fiche (encrypted codes), na kubadili taarifa kuwa katika mfumo rahisi unaoweza kutambulika na kutumika na TV zetu ( from coded form to non-coded form). King'amuzi (detector) ni kifaa maalum kinachotumika kutambua uwepo wa vitu vilivyofichika mfano chuma, na madini mengine.
Mbona umeongea kile kile nilichosema ila umaleta conclusion ni tofauti?

1.) Kung’amua kitu kilichokuwa encoded (encrypted) si ndio kudecode ama?! Sasa kinachong’amua si mdio decoder au? Sasa kitu kinachong’amua si ni king’amuzi au?!!

2.) Detector ni Kitambuzi , nami nimesema hivyo tangia awali

3.) Transmitter si inasambaza mawimbi sio? Sasa Kisambazaji hicho si ndio Kisimbuzi, ama?!!

34E2526B-B69E-4413-8832-FCD0336A01F7.jpeg
 
Back
Top Bottom