#COVID19 BAKWATA: Waliochanjwa UVIKO-19 mwaka mmoja au miaka miwili iliyopita hawataruhusiwa hijja hadi watakaporudia kuchanja

#COVID19 BAKWATA: Waliochanjwa UVIKO-19 mwaka mmoja au miaka miwili iliyopita hawataruhusiwa hijja hadi watakaporudia kuchanja

Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema waliochanjwa chanjo ya Uviko-19 mwaka mmoja au miaka miwili iliyopita hawataruhusiwa kwenda hijja hadi watakaporudia kuchanja chanjo hiyo.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumamosi Juni 24,2022 na Mkurugenzi wa Hija wa Bakwata, Alhaj Haidari Kambwili, katika semina ya mahujaji inayofanyika ofisi za Makao Makuu ya Bakwata jijini Dar es Salaam ikiwa ni maandalizi ya wahusika kwenda nchini Saudi Arabia kuhiji.

Kwenda kuhiji katika mji Makka uliopo nchini Saudi Arabia kwa mwenye uwezo ni moja kati ya nguzo tano za uislamu.

Kambwili amesema miongoni mwa masharti wanayopaswa kuyafuata wanaotaka kwenda hija ni kuchanja saa 72 kabla ya kuanza safari.

Kambwili amesema utaratibu huo wameelekezwa na nchi ya Saud Arabia ikiwa ni mkakati endelevu wa nchi hiyo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19.

Source:Mwananchi
Wachanje haraka sn
 
Wataalamu wa nje kama Dr Fauci wa marekani alisema hata waliochanja J&J wanaweza wakachanja chanjo zingine za Pfizer au Moderna kwa ajili ya Booster !! Lakini wataalamu wetu ndio sijawasikia kuhusu hii issue !! Tafadhali wajitokeze ili tukapate hizo booster !! Sisi wengine chanjo chanjo huwa hatuziogopi tunaogopaga vita tu kama vya UKRAINE maana vinatupandishia bei mahitaji yetu muhimu ya kila siku !!
Sisi hatuna wataalamu mkuu
 
Hapo ndio utajua ubaguzi wa waarabu, USA chanjo sio kigazo tena cha kuingia kwao
 
Wenye umri zaidi ya Miaka 65 hawaruhusiwi

"This year's pilgrimage will be limited to vaccinated Muslims under age 65, the hajj ministry has said.

Those coming from outside Saudi Arabia, who must apply for hajj visas, are required to submit a negative Covid-19 PCR result from a test taken within 72 hours of travel."
 
Sio kweli mbona chanjo ya ndui unachanja mara moja tu na inadumu maisha yote
Ziko hata za ugonjwa wa manjano nk mbona hukaa miaka kibao
Mtengeneza chanjo anaeleza umuhimu wa booster shot, anatokea mtu hajafanya utafiti wowote anasema chanjo hiyo ni ya maisha kama zilivo za ndui, manjano nk. Hii ndio nchi yetu ilipo!! sayansi dhidi ya imani, takwimu dhidi ya ubishi!!
 
Back
Top Bottom