Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Mkuu 50% ya project ni kubwa! Sema unachuki na JPM ndo maana hauoni alichofanya JPM hakujipendekeza kwao walikuja wenyewe baada ya kuona mziki wake! Angalia project kama zifuatazo
•Tanzania haikuwahi kuw ana Radar tokea uhuru amejenga nne kwa mkupuo Dar,mwanza,mbeya na klimanjaro
•Tanzania haikuwahi kuwa na Mahakama zakisasa tokea uhuru mahakama standard zilikuwa ni zile za kanda! Leo tunazungumzia mahaka zenye miundombinu ya kisasa!
•Nchi hii ilikuwa na hospital kubwa za kanda nyinhi za mashirika ya dini leo hii tuna hospital kubwa za hadhi ya kitaifa kule Musoma, mtwara,mbeya n.k Wao waliopita hawakufanya haya si kwa kuwa hawakuweza tu bali hata utendaji wao haukuwa katika viwango vya JPM!
•Vituo vya afya,hospital za wilaya, masoko.
•Uanzishwaji wa masoko ya madini mfano soko la dhahabu Geita limeinbiza takribani trilion tatu kwa miaka miwili na nusu!
•Upanuzi wa bandari hapo Dar, mtwara ma tanga!
•Ufufuami wa treni kutokea Dar mpaka moshi/arusha!
•Ujenzi wa flyover,busisi,mto wami n.k

Hayo ni ambo yanahitami usimamizi na fedha kwa hiyo kama matokeo yanaonekana kukopa kwake hakuna shida! Hata nyumbani kwako ukikopa benki ili ujenge nyumba na ukajenga kwa ubora na ikaonekana hakuna mtu atakaye kulaum! Ila kwa vile mmezoea maneno sio utendaji endeleeni kumsifia huyu mama ambaye hana hata historia ya utendaji kwenye maisha yake, kitu pekee kimemfikisha hapo ni kubebwa na siasa!
Hilo la radar ni uongo. Wakati wa Nyerere tulikuwa na radar 5 zenye coverage beyond our borders.
 
Hilo la radar ni uongo. Wakati wa Nyerere tulikuwa na radar 5 zenye coverage beyond our borders.
Kwa hiyo hizo radar kwenye viwanja vyetu vya ndege ni uongo? Vipi mengine niliyoandika ni ukweli? Maana umepinga radar vip menhine umekubali??
 
Magufuli katutenda deni la taifa, trilioni 78 Samia msalabani

Jamhuri October 26, 2021

Na Deodatus Balile

Kazi hii ya uandishi wa habari moja ya majukumu yake ni kuanika ukweli minong’ono inapotawala katika jamii.

Kwa sasa kuna minong’ono mingi. Minong’ono imeanza baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza hadharani mkopo wa Sh trilioni 1.3, alioukopa kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na akatangaza miradi lukuki itakayotekelezwa kwa kutumia mkopo huo.

Miongoni mwa miradi ya kihistoria ni ujenzi wa madarasa ya sekondari 15,000 nchi nzima na madarasa ya shule za msingi 3,000.

Kwa sasa inakadiriwa kuwa nchi ina upungufu wa madarasa 11,000, lakini Rais Samia ameamua kuona mbali.

Ameamua kufuta mfumo wa zima moto, ambapo kila mwaka wazazi wanakabwa koo vijijini kuchangia ujenzi wa madarasa.

Baadhi ya wazazi pia wameanza minong’ono kuwa watoto wao wamepewa mikopo kidogo, yaani Sh 600,000 kama ada vyuoni.

Hawajui kuwa miaka yote imekuwa hivyo na wakati mwingine wengi wanakuwa hawapati kabisa hata senti tano ya mkopo.

Sitanii, naomba nizungumzie kwa ufupi miezi sita ya Rais Samia akiwa Rais wa Tanzania baada ya kuapishwa Machi 19, 2021.

Nakumbuka vema kilichotokea, maana baada ya kifo cha Rais John Magufuli kulitokea kama sintofahamu hivi.
Wapo watu walioamini Rais Samia angeendelea kuwa Kaimu Rais, baadhi walidhani tunakwenda kwenye uchaguzi mpya na wengine hawakufahamu nini kitatokea.

Asubuhi ya Machi 18, 2021 niliamkia studio za Televisheni ya Taifa (TBC1) na TBC Taifa (radio) kufanya mahojiano na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba.

Hii ilikuwa ni baada ya kifo cha Rais John Magufuli, kilichotokea Machi 17, 2021. Ikumbukwe wiki moja kabla nilikuwa nimefanya mahojiano na kituo cha Star TV nikasema tuambiwe bayana Rais Magufuli yuko wapi na anafanya nini.

Machi 18 pamoja na kwamba nilikuwa bado Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), ambapo baadaye nilichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TEF Mei 22, 2021, ilinilazimu kutoa ufafanuzi huo uliokuwa tamko zito.

Sitanii, tamko nililolitoa lilizaa kuapishwa kwa Rais Samia kuwa Rais wa Awamu ya Sita Machi 19, 2021. Nilirejea Katiba ya Tanzania (1977) Ibara ya 37(5) inayosema: “Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya 40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka Rais atapendekeza jina la mtu atakayekuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua asilimia hamsini ya wabunge wote.”

Kwa mara ya kwanza kupitia makala hii ninakisema kilichotokea baada ya tamko hilo. Walinipigia simu watu wengi wakiwa na hofu.

Baadhi hawakufahamu Katiba inasemaje. Walinishutumu wakidai nimetangaza utaratibu wa kwangu, kwani baada ya kifo cha Rais kinachofuata ni uchaguzi.

Hii ilinipa shida kuona hata baadhi ya wabunge hawakufahamu nini kinafuata baada ya kifo hicho. Machi 18, 2021 itabaki kuwa siku ya kihistoria kwangu, kwani ujumbe nilioutoa ulitangazwa katika radio zote za ndani na za kimataifa na siku moja baadaye Rais Samia akaapishwa.

Sitanii, leo ninazungumzia mzigo wa madeni ambao Rais Magufuli amelitwisha taifa letu. Nimetangulia kusema na ninarudia, mimi ni msema kweli. Wala sipepesi macho katika kusema ukweli.

Wakati Rais Magufuli kwa miaka mitano yote alikuwa anawaaminisha Watanzania kuwa nchi inajenga miundombinu na inanunua ndege kwa kutumia fedha zetu wenyewe, uhalisia ni kinyume chake.

Kwa kipindi cha miaka mitano tu, Rais Mafuguli amekopa fedha nyingi kuliko fedha zote alizokopa Rais Benjamin Mkapa kwa miaka 10 aliyokaa madarakani.

Kwa miaka mitano, amekopa pia fedha nyingi kuliko alizokopa Rais Jakaya Kikwete kwa miaka 10 naye aliyokaa madarakani.

Rais Mkapa alirithi madeni mengi mno. Alipambana nayo, akaiingiza nchi katika Mpango wa Kusamehe Madeni Nchi Maskini (HIPC) na hadi anatoka madarakani, Tanzania ilikuwa inadaiwa Sh trilioni 20 tu.

Rais Kikwete wakati wake deni la taifa liliongezeka kwa Sh trilioni 23, hivyo akatoka madarakani deni la taifa likiwa Sh trilioni 43 kwa miaka 10. Rais Magufuli kwa miaka mitano tu, deni la taifa limeongezeka kwa Sh trilioni 29 na kufikia Sh trilioni 72 hadi anafariki dunia Machi, 2021.

Sitanii, kwa kasi hii ya ukopaji ina maana kama angekaa madarakani kwa miaka 10 kamili na akaendelea na kasi ya ukopaji wa wastani wa Sh trilioni 29 kwa miaka mitano, basi angetoka madarakani deni la taifa likiwa Sh trilioni 101 kufikia mwaka 2025.

Kuna jambo baya halisemwi. Rais Magufuli amekopa mikopo ya kibiashara inayoanza kulipwa baada ya miaka mitatu na inapaswa kulipwa ndani ya miaka minane, ikiwa na riba za kati ya asilimia 6 na 8.

Baadhi ya mikopo hii imeiva tayari. Imeanza kukuza deni la taifa kwa kasi kutokana na riba. Deni la taifa sasa limefikia Sh trilioni 78.

Kwa vyovyote vile iwavyo, Rais Samia anapaswa kuchukua hatua za haraka, ikiwamo kuunda timu ya majadiliano na wakopeshaji kwa ajili ya kubadili masharti ya mikopo ya kibiashara aliyochukua Rais Magufuli.

Anapaswa kuomba msamaha wa riba na pengine kuomba kuongezewa muda wa kulipa deni kama ulivyo utaratibu wa mikopo kwa serikali nyingi duniani.

Mikopo mingi kwa serikali huwa inalipwa kati ya miaka 20 hadi 50 kulingana na ukubwa wa mkopo na hutozwa riba kati ya asilimia 0.3 hadi asilimia 1. Mikopo ya aina hii inapatikana katika Benki ya Dunia, Shirika la Maendeleo Duniani, Benki ya Maendeleo Afika na nyingine za aina hii.

Kwa bahati mbaya na kwa masikitiko makubwa, kwa miaka mitano Wazungu tuliowaita mabeberu, ila tukawa tunakopa fedha zao kupitia benki za biashara. Kwa hali halisi, madeni haya yakiiva yote, ikiwa hakuna majadiliano ya dharura kuomba marekebisho ya masharti ya mikopo tuliyochukua chini ya Rais Magufuli, itafika mahala asilimia 60 ya bajeti ya taifa letu itakuwa inakwenda kulipa madeni. Waliomo serikalini watajua la kufanya katika hili.

Sitanii, ninafahamu baadhi ya wasomaji watakuwa wanaanza kufuka moshi kwa kusema ukweli huu. Wanajiuliza taarifa hizi nimezipata wapi? Taarifa hizi si za siri. Ziko wazi kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Nimepitia taarifa za mapitio ya mwenendo wa uchumi tangu mwaka 2000 hadi 2021. Zipo mtandaoni na zinaonyesha deni lilivyokua hatua kwa hatua. Kwa nia ya kuweka uelewa unaofanana, ifuatayo ni hali ya deni la taifa tangu mwaka 2005 hadi 2021.

Oktoba 2005, deni la nje lilikuwa USD milioni 8,361.9 sawa na Sh 19,286,471,493,000 na deni la ndani lilikuwa Sh 1,712,800,000,000. Jumla kuu ya deni wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani lilikuwa Sh 20,999,271,493,000 (Sh trilioni 20.9). Nimekokotoa hesabu hizi kwa kutumia viwango vya BoT vya kuuza dola ya Marekani ambavyo ni USD 1 kwa Sh 2,306.47.

Oktoba 2015, wakati Rais Kikwete anatoka madarakani deni la nje lilikuwa USD milioni 15,321.3, sawa na Sh 35,338,118,811,000 na deni la ndani lilikuwa Sh 7,826,200,000,000. Jumla kuu deni la nje na deni la ndani lilikuwa ni Sh 43,164,318,811,000 (Sh trilioni 43.1).

Deni la taifa lilianza kupanda kwa kasi Oktoba 2016. Deni la nje lilipanda na kuwa USD milioni 16,407.6 sawa na Sh 37,843,637,172,000, huku deni la ndani nalo likipanda na kuwa Sh 10,089,000,000,000. Jumla kuu ya deni ikafikia Sh 47,932,637,172,000 (Sh trilioni 47.9).

Oktoba 2017 deni la nje lilipanda kwa kasi kubwa na kufikia USD milioni 19,074.4 sawa na Sh 43,994,531,368,000. Kutokana na makandarasi kutolipwa deni la ndani nalo lilikua na kufikia Sh 12,563,300,000,000. Jumla kuu ya deni kwa mwaka huo likawa Sh 56,557,831,368,000 (Sh trilioni 56.5).

Oktoba 2018, deni la nje lilizidi kupanda na kuwa USD milioni 20,759.1 sawa na Sh 47,880,241,377,000, huku deni la ndani nalo likipanda na kuwa Sh 14,116,100,000,000. Jumla kuu ikawa Sh 61,996,341,377,000 (Sh trilioni 61.9).

Oktoba 2019, mwanamume aliongeza tena deni la taifa, deni la nje likafikia USD milioni 22,569.4, sawa na Sh 52,055,644,018,000, huku deni la ndani likipanda na kufikia Sh 14,187,400,000,000. Jumla kuu ya deni ikafikia Sh 66,243,044,018,000 (Sh trilioni 66.2).

Oktoba 2020, deni la nje lilipanda na kufikia USD milioni 23,599.3, sawa na Sh 54,431,077,471,000, huku deni la ndani likifikia Sh 15,608,500,000,000. Jumla kuu ikafikia Sh 70,039,577,471,000 (Sh trilioni 70).

Machi, 2021 wakati Rais Magufuli anafariki dunia, deni la nje la Tanzania lilikuwa limefikia USD milioni 24,429.2, sawa na Sh 56,345,216,924,000. Deni la ndani nalo lilipanda na kufikia Sh 16,116,500,000,000. Jumla kuu, deni la taifa lilifikia 72,461,716,924,000 (Sh trilioni 72.4).

Kilichofuata baada ya hapo, madeni yameanza kuiva kwa ajili ya kulipwa, huku mengine yakizalisha riba ya kufa mtu.

Makandarasi wengi Tanzania wanadai mabilioni kati ya hizo Sh trilioni 16 ambazo ni deni la ndani hawajalipwa siku nyingi. Kutokana na hali hiyo, madeni haya yaliyokopwa bila mpangilio katika benki za biashara yameanza kuwa msalaba kwa Rais Samia.

Taarifa ya hali ya Uchumi ya BoT ya Septemba, 2021 inayorejea mwezi Agosti, 2021 kutokana na mazingira hayo, deni la nje limekua na kufikia USD milioni 25,956.1 sawa na Sh 59,866,965,967,000, huku deni la ndani nalo likikua na kufikia Sh 18,225,000,000,000. Ukuaji huu unafanya kiwango cha deni la taifa kufikia jumla kuu ya Sh 78,091,965,967,000 (trilioni 78).

Sitanii, deni hili likigawanywa kwa Watanzania milioni 60, bila kujali mkubwa na mdogo, kila Mtanzania anadaiwa Sh 1,301,533 (Sh milioni 1.3). Hata hivyo, wataalamu wa uchumi wanasema deni hili si tishio kwa uchumi wa taifa letu kwa sasa kwani liko katika uwiano wa asilimia 30 kwa uchumi wa taifa letu, wakati kuna mataifa Afrika ambayo tayari yana uwiano wa asilimia 54 ya deni kwa uchumi wa nchi zao, ila wanaionya serikali iepuke mikopo ya kibiashara ina riba kubwa, masharti mabaya na inalipwa kwa muda mfupi.

Pale Dodoma, tumeona Rais Samia ameanzisha utaratibu mpya wa ukweli na uwazi katika mikopo. Ameeleza fedha alizokopa zitafanya nini kwa kuorodhesha miradi itakayotekelezwa na akatueleza amezikopa kutoka wapi.

Ninajiuliza, hivi ilikuwa ni kwa faida ya nani Rais Magufuli na wapambe wake kuficha ukweli kuwa miradi ya reli, barabara, umeme, ujenzi wa hospitali na mingine mingi aliyoijenga alikuwa anakopa?

Hivi sisi kama tungejua anakopa, tungemzuia? Lakini si tungepata fursa ya kumshauri asichukue mikopo ya kibiashara inayoanza kututoa utumbo sasa? Mungu ibariki Tanzania.

Copyright ©2021. Gazeti la Jamhuri


Mtalipa mpaka makalio kwa laana ya kuivamia Zanzibar,

Karma inawatesa vibaya sana hata bado . Roho za watu na damu mnayoimwaga na kubambikizia watu kesi za uongo , msifikiri ni bure tu.

MTATESEKA BSANA, KARMA HAIWAACHI KATU
 
Kwa hiyo hizo radar kwenye viwanja vyetu vya ndege ni uongo? Vipi mengine niliyoandika ni ukweli? Maana umepinga radar vip menhine umekubali??
Hayo mengine sina uhakika nayo ila la radar hauko sahihi
 
Tatizo lako unasoma articles zilizoandikwa kwa lugha ya layman na wewe unatafsiri word for word without understanding where the author is coming from in terms of regulation, industry norms and the reason for such penalties.

View attachment 1988676

Umeona hiyo FCA fines zao zimezingatia Credit Suisse waliamua kusamehe $200m so ni sehemu ya settlement vinginevyo fine ingekuwa kubwa zaidi tofauti na porojo zako.
Wacha wee....

Hatimae umetoa reference ile ile ya UK Financial Regulator....

Acha kuruka ruka ngugu mtetezi wa mikopo ya mabeberu!!

Ulisema walioendesha hiyo show ni IMF, nami nikakuambia ni UONGO! Nilikuambia Credit Suisse walikuwa wanachunguzwa na UK Financial Regulator, US Financial Regulator pamoja na Swiss Financial Regulator kwa sababu mkopo waliotoa ulikiuka misingi ya money laundering pamoja na kugubikwa na corruption!!!

Na ni hao ndio walifikisha kesi mahakamani! Hapa unajifanya kuleta reference, halafu unaacha details za kilichopelekea CS kupigwa faini kwamba:-

FCA.png

Sasa hao FCA ni IMF hao? We jamaa vipi wewe?

Na ili kuendelea kutetea uongo wako, hoja za msingi kwenye hiyo ripoti ya FCA umeziruka, na moja wapo ni hii hapa:-
As to the action brought by the DOJ, Credit Suisse pleaded guilty to one count of conspiracy to violate the federal wire fraud statute. The SEC’s order against Credit Suisse found that it violated antifraud provisions as well as internal accounting controls and books and records provisions of federal securities laws. Updated 21 October 2021.
Haya... onesha kwenye hiyo ripoti ni wapi wamesema Credit Suise hawakuwa approved na IMF kutoka mkopo! Au weka hiyo ripoti hapa tuone popote ilipotajwa IMF!

Halafu unaniambia kwamba Credit Suisse walisamehe $200M wakati nilishasema tayari kwamba:-
Hiyo 200M uliyoitaja bila kufahamu undani wake, inahusishwa na settlement ya corruption kwa sababu, uchunguzi ulithibitisha maofisa wa benki kuweka kibindoni zaidi ya USD 50 Million na Wafanyakazi wa Serikali ya Msumbiji na wenyewe waliweka kibindoni zaidi ya USD 130M!

Ingawaje hizo pesa zililipwa na benki husika, lakini burden yake ilienda kwa serikali kwa sababu inakuwa cost of loan!! Ni kutokana na hilo, ndo maana Credit Suisse wakaji-commit kufuta mkopo kwa USD 200M kama compensation ya pesa iliyoingia mifukoni mwa watu lakini burden inahamia kwa serikali ya Msumbiji!
Mbona unaruka ruka wewe?!

In short ni kwamba hukuwa ni details... ulikurupuka kuongea kitu ambacho hukutafiti huku ukibaki kujimwambafai kwamba eti u mtaalamu wa Public Finance, na kuleta porojo za namna gani IMF hutoa mikopo!!
Pili, deni la taifa sio lote ni la wizara ya fedha (serikali kuu), humo kuna majumuisho na madeni ya taasisi zingine za serikali. But
Mjadala wetu ni wapi tumeongelea deni letu la taifa? Kitu ambacho niliku-challenge ni pale ulipoonesha kwamba it's okay kukopa private banks kwa sababu hizo banks huwa hazitoi mkopo kwa nchi maskini bila kupewa hidhini IMF Approval...

Na ukaendelea kudai kwamba, hata JK na Mkapa sio kwmaba hawakutaka kukopa kwa private banks bali walikuwa hawakupesheki!

Hapo ndipo nikakuambia suala la kukopa private banks sio la kuonea fahari kwa sababu mikopo ya hawa jamaa inaambatana na janja janja nyingi including corruption!

Na nikakupa hadi mfano wa serikali ya JK ilipokopa over USD 600 Million Stanibic ambayo na yenyewe walimwingizia middle man zaidi ya Shilingi 10 Billion za Tannzani!

Au unaeleza hayo katika harakati zako za kutetea hiyo mikopo iliyochukuliwa?
Mfano TANESCO anapokopa anatakiwa alipe mwenyewe pamoja na hivyo deni lao litakuwa kwenye vitabu vyao na vitabu vya serikali; ukishindwa kulipa kama ni government guarantee loan serikali inatakiwa kugharamia hilo deni.
Sasa inahusiana na mjadala wetu? Btw, unadhani TANESCO wanaweza kuchukua mkopo bila guarantee ya serikali?! Na kwa akili yako, TANESCO wakishindwa kulipa unadhani nani atakuwa responsibile?
Hizo kampuni za Mozambique zilienda kukopa bila ya idhini ya serikali yet mkopo unadhamana ya serikali na hawakujua mpaka hizo taasisi ziliposhindwa kulipa.
Look at you...

Eti hizo kampuni zilienda kukopa bila idhini ya serikali na hapo hapo serikali ikawadhamini?!

Unadhamini vipi kitu ambacho hujakibariki? Hivi unajua unachokiongea wewe?
Can you see why IMF would be pissed wakati wameweka frameworks za stress test, wewe unakwepa njia zao kwenda kukopesha nchi maskini na uishirikishi serikali kuu.
Hujui unachokiongea...

Angalau ungesema "...wewe unaenda KUKOPA"!

IMF wana-deal na serikali na sio taasisi inayokopesha!!

Na ndo maana nikakupa mfano wa ANY LENDER VS ANY DEBTOR!

As long as Credit Suisse ndio walitoa mkopo, hapo ni CS ndio walikuwa na wajibu wa kufahamu loan portfolio ya Mozambique ili kujiridhisha endapo wataweza kulipa, lakini sio Credit Suisse kutaka approval ya IMF kabla ya kutoa mkopo!!

Na hiyo sababu ya ANY LENDER VS ANY DEBTOR ndiyo iliwaingiza (sio kwenye kesi) IMF kwa Msumbiji!

Kwamba, IMF walitaka kutoa mkopo kwa Msumbiji lakini uchunguzi wa named Financial Regulators ukafichukua mkopo waliochukua Msumbiji kwa Credit Suisse! Mkopo huo wa CS hukufahamika na IMF, na ndo maana wakaamua ku-cancel mkopo waliotaka kuwapa Mozambique!
Vualla mambo yanaenda ndivyo sivyo, ndio maana wanakwambia hawakufuata rules na rushwa ilitumika, in other word hawakufuata taratibu za kimataifa za kukopesha nchi maskini.
Ni nani waliosema hivyo? Ni IMF, au?!

Achana na habari za IMF kwenye hii mada kwa sababu unachanganya madesa! Na hizo sio taratibu za kimataifa za kukopesha nchi maskini bali ni taratibu zinazo-apply duniani kote!!

However, as a banker, kuna more risky customers! Sasa unaokutana na mteja wa aina hiyo, unatakiwa kuwa makini zaidi katika kufuata operation procedures!!
Serikali kuu inaweza kopa bila ya idhini ya IMF/WB but there is a catch ukishindwa kulipa madeni yako, structural adjustment policies zinafuata. Ukikataa kupangiwa nao ukopeshwi tena mnakufa njaa.
Kwa kuchanganya changanya mambo tu, u hodari!
Na ukienda tena private bank upati mkopo kwa sababu ulishindwa kulipa deni lao you are not credit worthy na huyo CEO si ajabu akatimuliwa kazi kwa kutoa mikopo yenye high risk bila ya kufuata taratibu za IMF.
Yaani CEO wa Private Bank afukuzwe kazi kwa sababu hakufuata taratibu za IMF?!

We jamaa acha kuongea mambo usiyoyajua!! Fine, umesema wewe ni mtaalamu wa Public Finance lakini HUJUI LOLOTE KUHUSU MAMBO YA KIBENKI!!

Huyo CEO atafukuzwa endapo taratibu hazikufuatwa, including kufanya DUE DILIGENCE!!

Uzuri wa mabenki ni mmoja! Kama umefuata taratibu zote, kisha ukatoa mzigo lakini ukaishia kwa wajanja! Au finally ikagundulika mliowapa pesa ni matapeli... hapo bankers hawawezi kuwa held responsible unless kama hawakufanya due diligence ya kutosha!

Kwamba, watu wanaweza kuja na docs ZOTE zinazoonekana ni halali, kwa mfano kutoka Serikali X! Hapo ukifuata taratibu zote na ukatoa mzigo kwa kutumia hizo docs... utakuwa free kwenye kipengele cha kufuata taratibu!

Lakini je, ulifanya Due Diligence kujiridhisha mamlaka husika zinahusika na hizo docs zinazoonekana ni legit?

Back in the days iliwahi kutokea issue kama hiyo pale NMB Morogoro Rd Branch!

Wajanja wameenda pale na docs ZOTE HALALI kutoka Wizara ya Afya! Jamaa wakafungua akaunti kama signatories wa wizara! Ulipoingizwa mpunga tu, jamaa wakatoa mzigokutoka kwenye akaunti, na wakapotea!

Hapo NMB Morogoro Rd Branch walifuata taratibu zote za kufungua akaunti lakini hawakufanya due diligence kujiridhisha kwamba zilitoka kwenye mamlaka halali!!

Kuna "Wajanja" wengine wanaitumia sana BRELA kupiga mpunga!! Kwa mfano, watu wanaweza kwenda benki na legit docs za kampuni X maybe inayofanya kazi na serikali! Hapo wataenda hadi na Docs za BRELA kuthibitisha existence ya kampuni husika!

Sasa bankers wakiwa makini kwenye due diligence, wanaweza kukuta ni kweli kampuni ipo, na imesajiriwa BRELA lakini walio mbele yako sio TRUE OWNERS wa kampuni husika! Sasa kwanini wamekuja kufungua akaunti ya kampuni ambayo sio yao?

More likely, watakuwa wamepiga cheque ya kampuni husika, na wanajua ili kutoa pesa kutoka kwenye hiyo cheque, ni LAZIMA wafungue akaunti yenye jina lililopo kwenye cheque (of that company)!
Ndio maana pia kuna ranking the nations credit kutoka kwa watu ‘Moody’s’ na ‘Standard and Poor‘ kuwaambia private lenders credit worthiness za nchi.

Hizo ni baadhi ya sababu nchi maskini kwenda kukopa bila ya kuongea na IMF mambo yakienda kombo inajitengenezea matatizo makubwa siku wakirudi kutaka mikopo yao.
Naona unageuza gia angani...

Kwahiyo sasa ni "...nchi maskini kwenda kukopa bila ya kuongea na IMF" na sio tena:-
Hivi unadhani mabeberu ata kwa kupitia private banks yanakopesha nchi maskini bila ya IMF na WB kufanya stress test kama unaweza kulipa madeni yako huko mbele based on your tax collections.
Yaani umeshasahau ulisema hata hizo private banks za mabeberu hazikopeshi nchi maskini bila IMF kufanya yao, halafu hapa unapinduka na kusema nchi maskini haziwezi kukopa kwenye private banks bila IMF kufanya yao!!

Na hata kwenye post yako hii umesahau ulisema:-
Can you see why IMF would be pissed wakati wameweka frameworks za stress test, wewe unakwepa njia zao kwenda kukopesha nchi maskini na uishirikishi serikali kuu.
Hivi hiyo sentensi inamaanisha nini kama sio private banks kutokopesha nchi maskini bila kufuata miongozo ya IMF?

Halafu few hours ago, ulileta fix zingine kwamba mapato makubwa ya IMF yanatokana na mikopo wanayochukua kutoka private banks!

Kituko ni pale unapojaribu kuaminisha watu kwamba MWENYE PESA YAKE/CREDITOR, yaani Private Banks, hawezi kukopesha bila kupewa idhini DEBTOR wake wakati huyo Creditor wala haendeshi shughuli zake chini ya mamlaka ya huyo anayemdai!
Mozambique wameshindwa kulipa madeni yao mengine jamaa donors wamewaka watalipa wao ‘Credit Suisse’ waliotengeneza madeni ya nyongeza nchi maskini bila ya ridhaa yao.
Ona fix ulizokuwa unapiga watu mwanzoni kabla sija-reveal uongo wako na hatimae ukabadilika na kuanza kuongelea habari za FCA!!

Hebu twende taratibu ndugu mwananchi...

Credit Suisse wamepewa za uso na IMF au FCA, pamoja na other finacial regulators (SEC & FINMA)?
Matter of fact crisis za 70 na 80’s zilitengenezwa na private banks kukopesha nchi maskini ovyo; na ndio sababu zilizopelekea kufutwa kwa madeni ya nchi maskini na donor lenders, private banks wao wakaja ‘Brady bonds’ na reforms za kukopesha nchi maskini zikafanywa na IMF/WB ili makosa yasijirudie tena.
Endelea tu kuchanganya madesa....

Btw, ni nani alikudanganya "...private banks wakaja na Brady Bonds"?!

Hivi unafahamu huyo ni Brady ni nani?!

FYI, kwanza hiyo crisis haikutokea in 70's bali in 80's!!

Na Brady Bond ni matokeo ya ku-fail mpango wa awali ambao ulinzishwa na James Baker, na program yenyewe ilikuwa inaitwa Baker Plan!!

Failure ya Baker Plan, iliyokuwa imeletwa na James Baker during Reagan Administartion, ndiyo ikaleta Brady Plan during Bush Sr Administration!

Both, James Baker na Nicholus Brady at the time walikuwa Treasury Secretaries. Hivyo basi, Brady Bond zilizotokana na Brady Plan ilikuwa ni mpango wa Serikali ya Marekani na sio private banks!!
Ni hivi kuna topics personal nikisoma comment najua huyu ni mbobezi, huyu ni average na huyu unga unga; na wewe private finance bado sana. Una unga unga tu kwa kusoma article at face value but can’t reason behind the course of action.
Umebaki tambo tu lakini HUJUI LOLOTE....

Na hivi unakumbuka ulisema eti nakupotezea muda ingawaje hujaacha kuni-quote?!

Hatimae nimebaini ni wewe ndie unanipotezea muda manake mara kwa mara unaleta mambo tofauti lakini unayaleta bila kuwa na ufahamu nayo!!

So, stay blessed, coz' you're the one now wasting my time!

Jifunze kwanza kusimama kwenye hoja moja, na ukija na hoja tofauti basi iwe inalenga kukazia hoja ya msingi iliyobeba mjadala!!

On top of that, unapoleta hizo hoja tofauti basi uwe na uelewa wa hicho unacholeta! Sio tu unampelekea bosi chai, njiani unasikia kwa mbali watu wwanazungumzia Brady Bonds na hatimae unafanikiwa kudaka mawili matatu, kutoka kwao, basi hapo hapo unakurupuka kuja hapa kabla hujawa na uelewa whicho ulichosikia!!
 
Magufuli katutenda deni la taifa, trilioni 78 Samia msalabani

Jamhuri October 26, 2021

Na Deodatus Balile

Kazi hii ya uandishi wa habari moja ya majukumu yake ni kuanika ukweli minong’ono inapotawala katika jamii.

Kwa sasa kuna minong’ono mingi. Minong’ono imeanza baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza hadharani mkopo wa Sh trilioni 1.3, alioukopa kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na akatangaza miradi lukuki itakayotekelezwa kwa kutumia mkopo huo.

Miongoni mwa miradi ya kihistoria ni ujenzi wa madarasa ya sekondari 15,000 nchi nzima na madarasa ya shule za msingi 3,000.

Kwa sasa inakadiriwa kuwa nchi ina upungufu wa madarasa 11,000, lakini Rais Samia ameamua kuona mbali.

Ameamua kufuta mfumo wa zima moto, ambapo kila mwaka wazazi wanakabwa koo vijijini kuchangia ujenzi wa madarasa.

Baadhi ya wazazi pia wameanza minong’ono kuwa watoto wao wamepewa mikopo kidogo, yaani Sh 600,000 kama ada vyuoni.

Hawajui kuwa miaka yote imekuwa hivyo na wakati mwingine wengi wanakuwa hawapati kabisa hata senti tano ya mkopo.

Sitanii, naomba nizungumzie kwa ufupi miezi sita ya Rais Samia akiwa Rais wa Tanzania baada ya kuapishwa Machi 19, 2021.

Nakumbuka vema kilichotokea, maana baada ya kifo cha Rais John Magufuli kulitokea kama sintofahamu hivi.
Wapo watu walioamini Rais Samia angeendelea kuwa Kaimu Rais, baadhi walidhani tunakwenda kwenye uchaguzi mpya na wengine hawakufahamu nini kitatokea.

Asubuhi ya Machi 18, 2021 niliamkia studio za Televisheni ya Taifa (TBC1) na TBC Taifa (radio) kufanya mahojiano na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba.

Hii ilikuwa ni baada ya kifo cha Rais John Magufuli, kilichotokea Machi 17, 2021. Ikumbukwe wiki moja kabla nilikuwa nimefanya mahojiano na kituo cha Star TV nikasema tuambiwe bayana Rais Magufuli yuko wapi na anafanya nini.

Machi 18 pamoja na kwamba nilikuwa bado Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), ambapo baadaye nilichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TEF Mei 22, 2021, ilinilazimu kutoa ufafanuzi huo uliokuwa tamko zito.

Sitanii, tamko nililolitoa lilizaa kuapishwa kwa Rais Samia kuwa Rais wa Awamu ya Sita Machi 19, 2021. Nilirejea Katiba ya Tanzania (1977) Ibara ya 37(5) inayosema: “Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya 40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka Rais atapendekeza jina la mtu atakayekuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua asilimia hamsini ya wabunge wote.”

Kwa mara ya kwanza kupitia makala hii ninakisema kilichotokea baada ya tamko hilo. Walinipigia simu watu wengi wakiwa na hofu.

Baadhi hawakufahamu Katiba inasemaje. Walinishutumu wakidai nimetangaza utaratibu wa kwangu, kwani baada ya kifo cha Rais kinachofuata ni uchaguzi.

Hii ilinipa shida kuona hata baadhi ya wabunge hawakufahamu nini kinafuata baada ya kifo hicho. Machi 18, 2021 itabaki kuwa siku ya kihistoria kwangu, kwani ujumbe nilioutoa ulitangazwa katika radio zote za ndani na za kimataifa na siku moja baadaye Rais Samia akaapishwa.

Sitanii, leo ninazungumzia mzigo wa madeni ambao Rais Magufuli amelitwisha taifa letu. Nimetangulia kusema na ninarudia, mimi ni msema kweli. Wala sipepesi macho katika kusema ukweli.

Wakati Rais Magufuli kwa miaka mitano yote alikuwa anawaaminisha Watanzania kuwa nchi inajenga miundombinu na inanunua ndege kwa kutumia fedha zetu wenyewe, uhalisia ni kinyume chake.

Kwa kipindi cha miaka mitano tu, Rais Mafuguli amekopa fedha nyingi kuliko fedha zote alizokopa Rais Benjamin Mkapa kwa miaka 10 aliyokaa madarakani.

Kwa miaka mitano, amekopa pia fedha nyingi kuliko alizokopa Rais Jakaya Kikwete kwa miaka 10 naye aliyokaa madarakani.

Rais Mkapa alirithi madeni mengi mno. Alipambana nayo, akaiingiza nchi katika Mpango wa Kusamehe Madeni Nchi Maskini (HIPC) na hadi anatoka madarakani, Tanzania ilikuwa inadaiwa Sh trilioni 20 tu.

Rais Kikwete wakati wake deni la taifa liliongezeka kwa Sh trilioni 23, hivyo akatoka madarakani deni la taifa likiwa Sh trilioni 43 kwa miaka 10. Rais Magufuli kwa miaka mitano tu, deni la taifa limeongezeka kwa Sh trilioni 29 na kufikia Sh trilioni 72 hadi anafariki dunia Machi, 2021.

Sitanii, kwa kasi hii ya ukopaji ina maana kama angekaa madarakani kwa miaka 10 kamili na akaendelea na kasi ya ukopaji wa wastani wa Sh trilioni 29 kwa miaka mitano, basi angetoka madarakani deni la taifa likiwa Sh trilioni 101 kufikia mwaka 2025.

Kuna jambo baya halisemwi. Rais Magufuli amekopa mikopo ya kibiashara inayoanza kulipwa baada ya miaka mitatu na inapaswa kulipwa ndani ya miaka minane, ikiwa na riba za kati ya asilimia 6 na 8.

Baadhi ya mikopo hii imeiva tayari. Imeanza kukuza deni la taifa kwa kasi kutokana na riba. Deni la taifa sasa limefikia Sh trilioni 78.

Kwa vyovyote vile iwavyo, Rais Samia anapaswa kuchukua hatua za haraka, ikiwamo kuunda timu ya majadiliano na wakopeshaji kwa ajili ya kubadili masharti ya mikopo ya kibiashara aliyochukua Rais Magufuli.

Anapaswa kuomba msamaha wa riba na pengine kuomba kuongezewa muda wa kulipa deni kama ulivyo utaratibu wa mikopo kwa serikali nyingi duniani.

Mikopo mingi kwa serikali huwa inalipwa kati ya miaka 20 hadi 50 kulingana na ukubwa wa mkopo na hutozwa riba kati ya asilimia 0.3 hadi asilimia 1. Mikopo ya aina hii inapatikana katika Benki ya Dunia, Shirika la Maendeleo Duniani, Benki ya Maendeleo Afika na nyingine za aina hii.

Kwa bahati mbaya na kwa masikitiko makubwa, kwa miaka mitano Wazungu tuliowaita mabeberu, ila tukawa tunakopa fedha zao kupitia benki za biashara. Kwa hali halisi, madeni haya yakiiva yote, ikiwa hakuna majadiliano ya dharura kuomba marekebisho ya masharti ya mikopo tuliyochukua chini ya Rais Magufuli, itafika mahala asilimia 60 ya bajeti ya taifa letu itakuwa inakwenda kulipa madeni. Waliomo serikalini watajua la kufanya katika hili.

Sitanii, ninafahamu baadhi ya wasomaji watakuwa wanaanza kufuka moshi kwa kusema ukweli huu. Wanajiuliza taarifa hizi nimezipata wapi? Taarifa hizi si za siri. Ziko wazi kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Nimepitia taarifa za mapitio ya mwenendo wa uchumi tangu mwaka 2000 hadi 2021. Zipo mtandaoni na zinaonyesha deni lilivyokua hatua kwa hatua. Kwa nia ya kuweka uelewa unaofanana, ifuatayo ni hali ya deni la taifa tangu mwaka 2005 hadi 2021.

Oktoba 2005, deni la nje lilikuwa USD milioni 8,361.9 sawa na Sh 19,286,471,493,000 na deni la ndani lilikuwa Sh 1,712,800,000,000. Jumla kuu ya deni wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani lilikuwa Sh 20,999,271,493,000 (Sh trilioni 20.9). Nimekokotoa hesabu hizi kwa kutumia viwango vya BoT vya kuuza dola ya Marekani ambavyo ni USD 1 kwa Sh 2,306.47.

Oktoba 2015, wakati Rais Kikwete anatoka madarakani deni la nje lilikuwa USD milioni 15,321.3, sawa na Sh 35,338,118,811,000 na deni la ndani lilikuwa Sh 7,826,200,000,000. Jumla kuu deni la nje na deni la ndani lilikuwa ni Sh 43,164,318,811,000 (Sh trilioni 43.1).

Deni la taifa lilianza kupanda kwa kasi Oktoba 2016. Deni la nje lilipanda na kuwa USD milioni 16,407.6 sawa na Sh 37,843,637,172,000, huku deni la ndani nalo likipanda na kuwa Sh 10,089,000,000,000. Jumla kuu ya deni ikafikia Sh 47,932,637,172,000 (Sh trilioni 47.9).

Oktoba 2017 deni la nje lilipanda kwa kasi kubwa na kufikia USD milioni 19,074.4 sawa na Sh 43,994,531,368,000. Kutokana na makandarasi kutolipwa deni la ndani nalo lilikua na kufikia Sh 12,563,300,000,000. Jumla kuu ya deni kwa mwaka huo likawa Sh 56,557,831,368,000 (Sh trilioni 56.5).

Oktoba 2018, deni la nje lilizidi kupanda na kuwa USD milioni 20,759.1 sawa na Sh 47,880,241,377,000, huku deni la ndani nalo likipanda na kuwa Sh 14,116,100,000,000. Jumla kuu ikawa Sh 61,996,341,377,000 (Sh trilioni 61.9).

Oktoba 2019, mwanamume aliongeza tena deni la taifa, deni la nje likafikia USD milioni 22,569.4, sawa na Sh 52,055,644,018,000, huku deni la ndani likipanda na kufikia Sh 14,187,400,000,000. Jumla kuu ya deni ikafikia Sh 66,243,044,018,000 (Sh trilioni 66.2).

Oktoba 2020, deni la nje lilipanda na kufikia USD milioni 23,599.3, sawa na Sh 54,431,077,471,000, huku deni la ndani likifikia Sh 15,608,500,000,000. Jumla kuu ikafikia Sh 70,039,577,471,000 (Sh trilioni 70).

Machi, 2021 wakati Rais Magufuli anafariki dunia, deni la nje la Tanzania lilikuwa limefikia USD milioni 24,429.2, sawa na Sh 56,345,216,924,000. Deni la ndani nalo lilipanda na kufikia Sh 16,116,500,000,000. Jumla kuu, deni la taifa lilifikia 72,461,716,924,000 (Sh trilioni 72.4).

Kilichofuata baada ya hapo, madeni yameanza kuiva kwa ajili ya kulipwa, huku mengine yakizalisha riba ya kufa mtu.

Makandarasi wengi Tanzania wanadai mabilioni kati ya hizo Sh trilioni 16 ambazo ni deni la ndani hawajalipwa siku nyingi. Kutokana na hali hiyo, madeni haya yaliyokopwa bila mpangilio katika benki za biashara yameanza kuwa msalaba kwa Rais Samia.

Taarifa ya hali ya Uchumi ya BoT ya Septemba, 2021 inayorejea mwezi Agosti, 2021 kutokana na mazingira hayo, deni la nje limekua na kufikia USD milioni 25,956.1 sawa na Sh 59,866,965,967,000, huku deni la ndani nalo likikua na kufikia Sh 18,225,000,000,000. Ukuaji huu unafanya kiwango cha deni la taifa kufikia jumla kuu ya Sh 78,091,965,967,000 (trilioni 78).

Sitanii, deni hili likigawanywa kwa Watanzania milioni 60, bila kujali mkubwa na mdogo, kila Mtanzania anadaiwa Sh 1,301,533 (Sh milioni 1.3). Hata hivyo, wataalamu wa uchumi wanasema deni hili si tishio kwa uchumi wa taifa letu kwa sasa kwani liko katika uwiano wa asilimia 30 kwa uchumi wa taifa letu, wakati kuna mataifa Afrika ambayo tayari yana uwiano wa asilimia 54 ya deni kwa uchumi wa nchi zao, ila wanaionya serikali iepuke mikopo ya kibiashara ina riba kubwa, masharti mabaya na inalipwa kwa muda mfupi.

Pale Dodoma, tumeona Rais Samia ameanzisha utaratibu mpya wa ukweli na uwazi katika mikopo. Ameeleza fedha alizokopa zitafanya nini kwa kuorodhesha miradi itakayotekelezwa na akatueleza amezikopa kutoka wapi.

Ninajiuliza, hivi ilikuwa ni kwa faida ya nani Rais Magufuli na wapambe wake kuficha ukweli kuwa miradi ya reli, barabara, umeme, ujenzi wa hospitali na mingine mingi aliyoijenga alikuwa anakopa?

Hivi sisi kama tungejua anakopa, tungemzuia? Lakini si tungepata fursa ya kumshauri asichukue mikopo ya kibiashara inayoanza kututoa utumbo sasa? Mungu ibariki Tanzania.

Copyright ©2021. Gazeti la Jamhuri
Chief Hangaya naye kaongeza deni la Trilion 1.3 sasa tumefikia 79.3 Trilion
 
We ni kenge kama kenge wengine,,pesa za masharti ya kibiashara ni pesa at your own risk na hizo mikopo hazina masharti yoyote na wanapenda Sana ukope kwa staili hiyo Ili upigwe vizuri..

By the way mikopo mingi ya kibiashara haitolewi na WB na IMF bali kutoka financial markets kama mabenki binafsi.

Samia hakopeshwi mikopo ya kibiashara bali concessional loans ambayo hadi ukopeshwe basi wamekuamini na wanataka uwazi na uwajibikaji .
Kabla ya kuita wenzako kenge, umesoma na kuelewa kilichoandikwa?

We jamaa wa wapi wewe?!
 
Mkubali tu hana mbinu za kupata kodi hivyo ameamua kuumiza watu wa chini.

Mpaka kufika mwezi wa babe shule karibia zote za msingi na swkondari zilikuwa zimeoewa pesa za ujenzi wa madarasa. Hii unamaanisha hizo bajeti zilikuwepo na pesa zilikuwepo cha kushangaza , Tumewekewa tozo tukaambiwa pesa zinakwenda kujenga madarasa. Mkopo imechukuliwa tumepewa sababu hizo hizo. Nina ushahidi na hili kwa sababu nilikuwa na tenda ya kusaply mbao, na kutengeneza milango na madawati na bililipwa mwezi wa nane pesa zote. Kwa taatifa yako hadi shule zingine zilipewa pesa za kujenga madarasa zaidi ya uhitaji.

Hizo tozo na mkopo ni pesa inapigwa tu.
Tunaposema mama hafai tunamaanisha tunachosema.
Nani anapiga Hela sasa kati ya wewe na Raismaana tenda ya ku supply mbao umepewa wewe kwenye shule?
 
Chief Hangaya naye kaongeza deni la Trilion 1.3 sasa tumefikia 79.3 Trilion
Na kuna mtu hapo juu nimemwambia inabidi tukae kwa kutulia kwa sababu mambo bado sana...

Ukitoa hizo 1.3 Trillion... SGR haijafika popote! Kwahiyo Serikaya ya Chifu Hangaya itaendelea kukopa kwa ajili ya SGR!!

Kuna Bwawa la Umeme... huko nako wataendelea kukopa!!

Kwa hayo mawili, siwezi kumlaumu kwa sababu hakuna namna... tushaingia shipa!!

Lakini kama hiyo haitoshi, wameingia mkataba wa kununua ndege zingine wakati zilizopo bado ni loss-making with no predictable feature!!

Hapo tena, atakopa pesa! Na IMF hawawezi kukukopesha eti ukanunue ndege! Hapo atalazimika kwenda private banks ambazo zimejaa janja janja nyingi, including corruption and riba zisizo rafiki!!
 
ndo mwisho wako wa kufikili mkuu? ivi mtu kama mwigulu tangu lini akaamika? unataka niamini taarifa iliyotolewa na BOT, au mwigulu, acha ushabiki maandazi
BoT ipo chini ya wizara gani?

Boss wa wizara husika ni nani?
 
Kwani deni linalipwa na pesa za nje?

Ni msaada tu ndio huwa za nje, borrowed zote ni za ndani. Unachanga unalipa... ukikamilisha mradi ni wako.

We ukikopa ukajenga nyumba then ukikamilisha mkopo ni bank imekujengea au we mwenyewe?
Wasipoiona hii,watakuwa wamevaa miwani ya mbao.
 
Mzee wakati wa Mwendazake hiyo tovuti ya BoT si ilikuwepo, mbona hukuitumia na kuleta taarifa kama hizi? Nakumbuka kuna wakati gazeti lako lilisifiwa hadharani na JPM kwa kuibua uozo sijui bandarini ama wapi lakini hili ambalo unasema linatutoa utumbo hukulisema. Leo ndio umeliona, kweli ya Mungu mengi.
Sasa hilo nalo swali! Hakusema kwasababu alikuwa anahofia maisha yake. Kila mtu anajua kilichokuwa kinawapata waandishi wa habari waliokuwa wanamkosoa.
 
Sasa hilo nalo swali! Hakusema kwasababu alikuwa anahofia maisha yake. Kila mtu anajua kilichokuwa kinawapata waandishi wa habari waliokuwa wanamkosoa.
Kwa hiyo waandishi wote walikaa kimya? Kusema kwamba tumekopa iwe shida? Mbona BoT walikuwa wakiweka kwenye website yao, mbona wap hawakupata shida? Unafiki tu
 
Na kuna mtu hapo juu nimemwambia inabidi tukae kwa kutulia kwa sababu mambo bado sana...

Ukitoa hizo 1.3 Trillion... SGR haijafika popote! Kwahiyo Serikaya ya Chifu Hangaya itaendelea kukopa kwa ajili ya SGR!!

Kuna Bwawa la Umeme... huko nako wataendelea kukopa!!

Kwa hayo mawili, siwezi kumlaumu kwa sababu hakuna namna... tushaingia shipa!!

Lakini kama hiyo haitoshi, wameingia mkataba wa kununua ndege zingine wakati zilizopo bado ni loss-making with no predictable feature!!

Hapo tena, atakopa pesa! Na IMF hawawezi kukukopesha eti ukanunue ndege! Hapo atalazimika kwenda private banks ambazo zimejaa janja janja nyingi, including corruption and riba zisizo rafiki!!
Hayo mengine mie siyajui but hili la atcl nalijua vizuri serikali inatedpond kutokana na mpango ws biashara ambao umetayarishwa kwa kuliendeleza hilo shirika

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Kuiva kwa deni maana yake muda wa kuanza kulipa deni lako na riba yake umefika. Haimaanishi kuwa hilo sasa ni deni jipya on top of that.

Na tunapocalculate deni la Taifa maana yake vitu vyote hivyo unavyovisema tumeshaviinclude ndani yake.

Kwa hiyo ukiambiwa mwaka 2005 Kikwete alikuta deni la Trillion 20, basi hilo ndo deni alilolikuta, akizembea kulipa linajiaccumulate, na hiyo accumulation inaongezwa kwenye deni, na kile atajachokopa yeye nacho kinaongezwa kwenye deni.

Kwa hiyo kama Magufuli alikuta deni la Trillion 42 mwaka 2015, basi ndo deni hilo alilokuta limeshainclude vyote (riba na mkopo wa JK), Sasa na yeye Magufuli kaavha deni la Trillion 70, maana yake kaongeza Trilion zake za kutosha tu kwenye deni alilokuta. Yeye kama rais ilibidi Alipe, hakuna excuse kuwa ni madeni ya watangulizi wangu. Kwani Mkapa, JK hawakuwa na watangulizi?, Mbona wao rate ya ukuaji wa deni haikuwa kama ya Magufuli?


Hapa kwa kifupi unasema kwamba JPM si kwamba alikuwa anakopa sana ila tu hakuwa mlipaji mzuri wa deni alilolikuta ndio maana deni mmekuwa kwa kasi?
 
Back
Top Bottom