Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Toa mfano acha projo Huyo mama yenu hakopesheki ndo maana hela za UVICO zimekuwa za kudanganyia wananchi miradi uchwara!

Kwa kuona kwamba hakopesheki ameanzisha tozo ovyo ovyo! Unafikiri hao IMF&WB huwa hawajui kuwa Rais fulani ni mtendaji sio wa maneno! Hapa wanajua Mama ni Maneno sio vitendo! Ila JPM walijua ni vitendo sio maneno!
SukumaGang katika ubora!!!
 
Huu uzi ni mzuri kwa maslahi mapana ya taifa ila naona umegeuzwa kuwa battle kati ya watetea legacy vs waponda legacy
Kutetea legacy na kuponda legacy kwa hoja ni afya kwa taifa.
Kila mmoja anaponda au kutetea kwa maslahi ya nchi.
Kama unadhani mwendazake amekosea mahali, weka vitu hapa watanzania waone na wengine wajifunze.
Kama unaamini amefanya mazuri kwa faida ya nchi dondosha ushahidi tuone.
Naona mjadala unaenda vema kwa maslahi ya taifa
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Swali kwako ni dogo sana, pamoja na analysis zako hizo za kina kuna maswali mawili tu unatakiwa uyajibu:
  1. Kwanini Serikali awamu ya 5 ilikopa mikopo ktk mabenki ya biashara yenye riba kubwa ya mpaka 6% badala ya mabenki kama benki ya Dunia, Afrika na IMF ambazo riba zake hazizidi 2%. (Mind you, hiyo tofauti ni kubwa sana.)
  2. Kwanini Magu Asiwaambie ukweli watanzania kuwa anakopa pesa kutekeleza miradi badala yake alituaminisha kuwa anatekeleza miradi hiyo kwa fedha zetu wenyewe hapa ndani ikiwa pamoja na gharama za uchaguzi?
Majibu yake ni marahisi.
Mabenki ya biashara hayana masharti magumu kama ilivyo IMF na WB.
IMF na WB wanaweza kukukopesha lkn wanakupa masharti magumu kama vile kufutilia mbali baadhi ya taasisi za umma.
Kukuelekeza miradi ya kufanyia fedha wanayokukopesha, watakuambia usiajiri kwa miaka kadhaa, watakuambia ongeza kodi katika eneo na samehe kodi katika eneo hili.
Yaani ni vurugu tupu. Unakuwa unaendeshwa kama mashine.
 
Swali kwako ni dogo sana, pamoja na analysis zako hizo za kina kuna maswali mawili tu unatakiwa uyajibu:
  1. Kwanini Serikali awamu ya 5 ilikopa mikopo ktk mabenki ya biashara yenye riba kubwa ya mpaka 6% badala ya mabenki kama benki ya Dunia, Afrika na IMF ambazo riba zake hazizidi 2%. (Mind you, hiyo tofauti ni kubwa sana.)
  2. Kwanini Magu Asiwaambie ukweli watanzania kuwa anakopa pesa kutekeleza miradi badala yake alituaminisha kuwa anatekeleza miradi hiyo kwa fedha zetu wenyewe hapa ndani ikiwa pamoja na gharama za uchaguzi?
Mikopo haijawahi kuwa siri. Ndio maana hata mwandishi amesema inapatikana tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania. Nadhani mahali pengine unapoweza kupata ni Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) na Wizara ya Fedha kwenye Hotuba za Waziri wa Fedha za bajeti na za hali ya uchumi.
Lakini hata kauli za JPM zilikuwa kwamba hata fedha za mikopo ni za kwetu kwa sababu zitalipwa kwa kodi za Watanzania.
 
Uongo kwa kuniwekea maneno yako. Unakuja na story ambazo unataka nizijibu vitu ambavyo sijaongea.
Maneno umeongea mwenyewe halafu unasema nimekuwekea maneno?

Toa mfano MMOJA TU wa hayo maneno niliyokuwekea...

NI wewe mwenyewe ndie umesmema kwamba:-
Hivi unadhani mabeberu ata kwa kupitia private banks yanakopesha nchi maskini bila ya IMF na WB kufanya stress test kama unaweza kulipa madeni yako huko mbele based on your tax collections.
Yaani hapo unataka kudanganya LIVE kwamba hata private banks za kibeberu haziwezi kukopesha nchi maskini bila approval ya IMF....

Ukaendelea kwamba:-
Embu fuatilia sakata la ‘Credit Suisse’ linaloendelea wamelimwa fine ya $475 million na kulazimishwa kufuta deni $200 million walilokopesha taasisi ya serikali msumbiji; yote kwa sababu huo mkopo ulitolewa kwa swirl bila ya kuwaambia IMF na WD.
Kwanza hiyo 200M sio kwamba walilazimishwa...

Narudia... chanzo cha sakata hili sio IMF kama unavyojaribu kuaminisha watu bali financial regulators wa US, UK na Uswisi. Baada ya wao kufanya uchunguzi, ndipo wakagundua violation of money laundering control na massive corruption!

Hiyo 200M uliyoitaja bila kufahamu undani wake, inahusishwa na settlement ya corruption kwa sababu, uchunguzi ulithibitisha maofisa wa benki kuweka kibindoni zaidi ya USD 50 Million na Wafanyakazi wa Serikali ya Msumbiji na wenyewe waliweka kibindoni zaidi ya USD 130M!

Ingawaje hizo pesa zililipwa na benki husika, lakini burden yake ilienda kwa serikali kwa sababu inakuwa cost of loan!! Ni kutokana na hilo, ndo maana Credit Suisse wakaji-commit kufuta mkopo kwa USD 200M kama compensation ya pesa iliyoingia mifukoni mwa watu lakini burden inahamia kwa serikali ya Msumbiji!
Issue ya Credit Suisse ni kukopesha taasisi ya serikali bila ya idhini ya serikali kuu huku deni likiwa na guarantee ya serikali.

Na kwa kanuni ya madeni ya serikali ni lazima yafanyiwe stress taste na frameworks wanazotumia ni za IMF na WD ata kama unaenda kukopa private bank kuona kama una uwezo wa kulipa.
Narudia... SIO KWELI

Issue sio Credit Suisse kukopesha bila idhini!!

Private banks hawahitaji idhini ya IMF ili kukopesha nchi!

Uhusika wa IMF kwa muktadha unaoeleza, ni kama ulivyo kwa any Creditor to her Debtor!!

Kwamba, taifa kama Msumbiji linapotaka mkopo toka popote pale, Lender atataka kufahamu financial status ya mkopaji, hii ikiwa ni pamoja na madeni aliyonayo na creditors wengine. Ni kutokana na hilo, ndo maana wengine wanakuwa na Credit Bureau!!

Sasa issue ya Msumbiji na IMF ilikuja wakati financial regulators niliowataja wakiendelea na uchunguzi wao dhidi ya Credit Suisse vs Mozambique! Hapo ndipo serikali ya Msumbiji ikazungumzia suala la guarantee waliyoweka kwenye mkopo MWINGINE toka kwa Credit Suisse!!

Hapo ndipo IMF wakafahamu kwamba kumbe kuna mkopo mwingine ambao wao walikuwa hawajui wakati walikuwa katika process za kutoa mkopo "mwingine" kwa Mozambique... hapo ndipo waka-cancel huo mkopo!!!

Kwahiyo ni issue ya IMF vs Serikali ya Msumbiji na sio IMF vs Credit Suisse!!!
Sasa kuelezea hizo stress taste zinahusu ni mlolongo mrefu ndio maana kila nchi ina DMO ya kufanya hiyo kazi. Hiki ndio nilichosema mimi.
Hayo uliyasema baadae baada kuweka wazi maelezo yasiyo sahihi uliyokuwa umetoa mwanzoni!!
Sasa wewe unataka ni entertain mawazo yako na maswali yasiyo na msingi
Kama hayana msingi mbona umeshindwa kujibu?! Nimekuuliza swali jepesi sana hapo juu, kwahiyo ningependa kurudia hapa...

TAJA MFANO MMOJA TU wa maneno niliyokuwekea!!
sijui ina maana private lending ni rahisi kukopa kushinda IMF na WB ndio nilichoandika hiko.
Hapo ulikuwa unajaribu kusema nini?!
Besides if you do not know ata hela wanazotoa IMF na WD asilimia kubwa ni za private banks; sema zinakuwa channeled through them ili ku control mikopo ya nchi na kuminimise risk za default.
We bhana acha kujifanya unajua sana wakati hakuna unachojua...

Hivi unajua IMF wanaingiza dola billion ngapi kupitia contribution quota?!

Hivi umeshawahi kuona Quota Formular inayotumika kuchangia?!

Hivi mataifa kama US yanavyoiletea jeuri UN unadhani ni kwa sababu HQ ya UN ipo Marekani?

Acha kuongea vitu usivyovijua wewe

Halafu unashindwa hata kutumia common sense!!

Yaani IMF waweze ku-control mikopo na ku-minimize default risks kushinda private banks zenyewe?!!

Hivi akina Nyerere waliokuwa wanavimba waziwazi kwamba "...madeni yenu hayalipiki, na kwahiyo hatutalipa".... hivi unadhani mkopeshaji angekuwa ni Private Bank akina Nyerere wangeongea kwa tambo namna hiyo?!
View attachment 1988268

Na ndio maana IMF walipobaini kwa mara ya kwanza kuna mkopo wa siri walisitisha mkopo wao 2016 na donors wengine walifuata; hizo stress test zipo kwa sababu zake.

Nakuletea sasa link ya ruling kukuonyesha sababu ya hizo fines za Credit Suisse ni kutotoa taarifa IMF na WB (hayo mengine ya rushwa na nini ni sehemu ndogo tu) nchi maskini mikopo yao ipo regulated.
Hilo nishaeleza hapo juu... ACHA KUCHANGANYA MADESA...

Btw, mbona hujaweka hiyo link?! Au huyo screenshot ndo unaita link?
 
Mikopo haijawahi kuwa siri. Ndio maana hata mwandishi amesema inapatikana tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania. Nadhani mahali pengine unapoweza kupata ni Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) na Wizara ya Fedha kwenye Hotuba za Waziri wa Fedha za bajeti na za hali ya uchumi.
Lakini hata kauli za JPM zilikuwa kwamba hata fedha za mikopo ni za kwetu kwa sababu zitalipwa kwa kodi za Watanzania.
Kauli za kitapeli hizi, kwahiyo Marais waliopita walikuwa wanadanganya watu kama yeye mwendakuzimu?
 
Magufuli katutenda deni la taifa, trilioni 78 Samia msalabani

Jamhuri October 26, 2021

Na Deodatus Balile

Kazi hii ya uandishi wa habari moja ya majukumu yake ni kuanika ukweli minong’ono inapotawala katika jamii.

Kwa sasa kuna minong’ono mingi. Minong’ono imeanza baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza hadharani mkopo wa Sh trilioni 1.3, alioukopa kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na akatangaza miradi lukuki itakayotekelezwa kwa kutumia mkopo huo.

Miongoni mwa miradi ya kihistoria ni ujenzi wa madarasa ya sekondari 15,000 nchi nzima na madarasa ya shule za msingi 3,000.

Kwa sasa inakadiriwa kuwa nchi ina upungufu wa madarasa 11,000, lakini Rais Samia ameamua kuona mbali.

Ameamua kufuta mfumo wa zima moto, ambapo kila mwaka wazazi wanakabwa koo vijijini kuchangia ujenzi wa madarasa.

Baadhi ya wazazi pia wameanza minong’ono kuwa watoto wao wamepewa mikopo kidogo, yaani Sh 600,000 kama ada vyuoni.

Hawajui kuwa miaka yote imekuwa hivyo na wakati mwingine wengi wanakuwa hawapati kabisa hata senti tano ya mkopo.

Sitanii, naomba nizungumzie kwa ufupi miezi sita ya Rais Samia akiwa Rais wa Tanzania baada ya kuapishwa Machi 19, 2021.

Nakumbuka vema kilichotokea, maana baada ya kifo cha Rais John Magufuli kulitokea kama sintofahamu hivi.
Wapo watu walioamini Rais Samia angeendelea kuwa Kaimu Rais, baadhi walidhani tunakwenda kwenye uchaguzi mpya na wengine hawakufahamu nini kitatokea.

Asubuhi ya Machi 18, 2021 niliamkia studio za Televisheni ya Taifa (TBC1) na TBC Taifa (radio) kufanya mahojiano na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba.

Hii ilikuwa ni baada ya kifo cha Rais John Magufuli, kilichotokea Machi 17, 2021. Ikumbukwe wiki moja kabla nilikuwa nimefanya mahojiano na kituo cha Star TV nikasema tuambiwe bayana Rais Magufuli yuko wapi na anafanya nini.

Machi 18 pamoja na kwamba nilikuwa bado Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), ambapo baadaye nilichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TEF Mei 22, 2021, ilinilazimu kutoa ufafanuzi huo uliokuwa tamko zito.

Sitanii, tamko nililolitoa lilizaa kuapishwa kwa Rais Samia kuwa Rais wa Awamu ya Sita Machi 19, 2021. Nilirejea Katiba ya Tanzania (1977) Ibara ya 37(5) inayosema: “Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya 40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka Rais atapendekeza jina la mtu atakayekuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua asilimia hamsini ya wabunge wote.”

Kwa mara ya kwanza kupitia makala hii ninakisema kilichotokea baada ya tamko hilo. Walinipigia simu watu wengi wakiwa na hofu.

Baadhi hawakufahamu Katiba inasemaje. Walinishutumu wakidai nimetangaza utaratibu wa kwangu, kwani baada ya kifo cha Rais kinachofuata ni uchaguzi.

Hii ilinipa shida kuona hata baadhi ya wabunge hawakufahamu nini kinafuata baada ya kifo hicho. Machi 18, 2021 itabaki kuwa siku ya kihistoria kwangu, kwani ujumbe nilioutoa ulitangazwa katika radio zote za ndani na za kimataifa na siku moja baadaye Rais Samia akaapishwa.

Sitanii, leo ninazungumzia mzigo wa madeni ambao Rais Magufuli amelitwisha taifa letu. Nimetangulia kusema na ninarudia, mimi ni msema kweli. Wala sipepesi macho katika kusema ukweli.

Wakati Rais Magufuli kwa miaka mitano yote alikuwa anawaaminisha Watanzania kuwa nchi inajenga miundombinu na inanunua ndege kwa kutumia fedha zetu wenyewe, uhalisia ni kinyume chake.

Kwa kipindi cha miaka mitano tu, Rais Mafuguli amekopa fedha nyingi kuliko fedha zote alizokopa Rais Benjamin Mkapa kwa miaka 10 aliyokaa madarakani.

Kwa miaka mitano, amekopa pia fedha nyingi kuliko alizokopa Rais Jakaya Kikwete kwa miaka 10 naye aliyokaa madarakani.

Rais Mkapa alirithi madeni mengi mno. Alipambana nayo, akaiingiza nchi katika Mpango wa Kusamehe Madeni Nchi Maskini (HIPC) na hadi anatoka madarakani, Tanzania ilikuwa inadaiwa Sh trilioni 20 tu.

Rais Kikwete wakati wake deni la taifa liliongezeka kwa Sh trilioni 23, hivyo akatoka madarakani deni la taifa likiwa Sh trilioni 43 kwa miaka 10. Rais Magufuli kwa miaka mitano tu, deni la taifa limeongezeka kwa Sh trilioni 29 na kufikia Sh trilioni 72 hadi anafariki dunia Machi, 2021.

Sitanii, kwa kasi hii ya ukopaji ina maana kama angekaa madarakani kwa miaka 10 kamili na akaendelea na kasi ya ukopaji wa wastani wa Sh trilioni 29 kwa miaka mitano, basi angetoka madarakani deni la taifa likiwa Sh trilioni 101 kufikia mwaka 2025.

Kuna jambo baya halisemwi. Rais Magufuli amekopa mikopo ya kibiashara inayoanza kulipwa baada ya miaka mitatu na inapaswa kulipwa ndani ya miaka minane, ikiwa na riba za kati ya asilimia 6 na 8.

Baadhi ya mikopo hii imeiva tayari. Imeanza kukuza deni la taifa kwa kasi kutokana na riba. Deni la taifa sasa limefikia Sh trilioni 78.

Kwa vyovyote vile iwavyo, Rais Samia anapaswa kuchukua hatua za haraka, ikiwamo kuunda timu ya majadiliano na wakopeshaji kwa ajili ya kubadili masharti ya mikopo ya kibiashara aliyochukua Rais Magufuli.

Anapaswa kuomba msamaha wa riba na pengine kuomba kuongezewa muda wa kulipa deni kama ulivyo utaratibu wa mikopo kwa serikali nyingi duniani.

Mikopo mingi kwa serikali huwa inalipwa kati ya miaka 20 hadi 50 kulingana na ukubwa wa mkopo na hutozwa riba kati ya asilimia 0.3 hadi asilimia 1. Mikopo ya aina hii inapatikana katika Benki ya Dunia, Shirika la Maendeleo Duniani, Benki ya Maendeleo Afika na nyingine za aina hii.

Kwa bahati mbaya na kwa masikitiko makubwa, kwa miaka mitano Wazungu tuliowaita mabeberu, ila tukawa tunakopa fedha zao kupitia benki za biashara. Kwa hali halisi, madeni haya yakiiva yote, ikiwa hakuna majadiliano ya dharura kuomba marekebisho ya masharti ya mikopo tuliyochukua chini ya Rais Magufuli, itafika mahala asilimia 60 ya bajeti ya taifa letu itakuwa inakwenda kulipa madeni. Waliomo serikalini watajua la kufanya katika hili.

Sitanii, ninafahamu baadhi ya wasomaji watakuwa wanaanza kufuka moshi kwa kusema ukweli huu. Wanajiuliza taarifa hizi nimezipata wapi? Taarifa hizi si za siri. Ziko wazi kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Nimepitia taarifa za mapitio ya mwenendo wa uchumi tangu mwaka 2000 hadi 2021. Zipo mtandaoni na zinaonyesha deni lilivyokua hatua kwa hatua. Kwa nia ya kuweka uelewa unaofanana, ifuatayo ni hali ya deni la taifa tangu mwaka 2005 hadi 2021.

Oktoba 2005, deni la nje lilikuwa USD milioni 8,361.9 sawa na Sh 19,286,471,493,000 na deni la ndani lilikuwa Sh 1,712,800,000,000. Jumla kuu ya deni wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani lilikuwa Sh 20,999,271,493,000 (Sh trilioni 20.9). Nimekokotoa hesabu hizi kwa kutumia viwango vya BoT vya kuuza dola ya Marekani ambavyo ni USD 1 kwa Sh 2,306.47.

Oktoba 2015, wakati Rais Kikwete anatoka madarakani deni la nje lilikuwa USD milioni 15,321.3, sawa na Sh 35,338,118,811,000 na deni la ndani lilikuwa Sh 7,826,200,000,000. Jumla kuu deni la nje na deni la ndani lilikuwa ni Sh 43,164,318,811,000 (Sh trilioni 43.1).

Deni la taifa lilianza kupanda kwa kasi Oktoba 2016. Deni la nje lilipanda na kuwa USD milioni 16,407.6 sawa na Sh 37,843,637,172,000, huku deni la ndani nalo likipanda na kuwa Sh 10,089,000,000,000. Jumla kuu ya deni ikafikia Sh 47,932,637,172,000 (Sh trilioni 47.9).

Oktoba 2017 deni la nje lilipanda kwa kasi kubwa na kufikia USD milioni 19,074.4 sawa na Sh 43,994,531,368,000. Kutokana na makandarasi kutolipwa deni la ndani nalo lilikua na kufikia Sh 12,563,300,000,000. Jumla kuu ya deni kwa mwaka huo likawa Sh 56,557,831,368,000 (Sh trilioni 56.5).

Oktoba 2018, deni la nje lilizidi kupanda na kuwa USD milioni 20,759.1 sawa na Sh 47,880,241,377,000, huku deni la ndani nalo likipanda na kuwa Sh 14,116,100,000,000. Jumla kuu ikawa Sh 61,996,341,377,000 (Sh trilioni 61.9).

Oktoba 2019, mwanamume aliongeza tena deni la taifa, deni la nje likafikia USD milioni 22,569.4, sawa na Sh 52,055,644,018,000, huku deni la ndani likipanda na kufikia Sh 14,187,400,000,000. Jumla kuu ya deni ikafikia Sh 66,243,044,018,000 (Sh trilioni 66.2).

Oktoba 2020, deni la nje lilipanda na kufikia USD milioni 23,599.3, sawa na Sh 54,431,077,471,000, huku deni la ndani likifikia Sh 15,608,500,000,000. Jumla kuu ikafikia Sh 70,039,577,471,000 (Sh trilioni 70).

Machi, 2021 wakati Rais Magufuli anafariki dunia, deni la nje la Tanzania lilikuwa limefikia USD milioni 24,429.2, sawa na Sh 56,345,216,924,000. Deni la ndani nalo lilipanda na kufikia Sh 16,116,500,000,000. Jumla kuu, deni la taifa lilifikia 72,461,716,924,000 (Sh trilioni 72.4).

Kilichofuata baada ya hapo, madeni yameanza kuiva kwa ajili ya kulipwa, huku mengine yakizalisha riba ya kufa mtu.

Makandarasi wengi Tanzania wanadai mabilioni kati ya hizo Sh trilioni 16 ambazo ni deni la ndani hawajalipwa siku nyingi. Kutokana na hali hiyo, madeni haya yaliyokopwa bila mpangilio katika benki za biashara yameanza kuwa msalaba kwa Rais Samia.

Taarifa ya hali ya Uchumi ya BoT ya Septemba, 2021 inayorejea mwezi Agosti, 2021 kutokana na mazingira hayo, deni la nje limekua na kufikia USD milioni 25,956.1 sawa na Sh 59,866,965,967,000, huku deni la ndani nalo likikua na kufikia Sh 18,225,000,000,000. Ukuaji huu unafanya kiwango cha deni la taifa kufikia jumla kuu ya Sh 78,091,965,967,000 (trilioni 78).

Sitanii, deni hili likigawanywa kwa Watanzania milioni 60, bila kujali mkubwa na mdogo, kila Mtanzania anadaiwa Sh 1,301,533 (Sh milioni 1.3). Hata hivyo, wataalamu wa uchumi wanasema deni hili si tishio kwa uchumi wa taifa letu kwa sasa kwani liko katika uwiano wa asilimia 30 kwa uchumi wa taifa letu, wakati kuna mataifa Afrika ambayo tayari yana uwiano wa asilimia 54 ya deni kwa uchumi wa nchi zao, ila wanaionya serikali iepuke mikopo ya kibiashara ina riba kubwa, masharti mabaya na inalipwa kwa muda mfupi.

Pale Dodoma, tumeona Rais Samia ameanzisha utaratibu mpya wa ukweli na uwazi katika mikopo. Ameeleza fedha alizokopa zitafanya nini kwa kuorodhesha miradi itakayotekelezwa na akatueleza amezikopa kutoka wapi.

Ninajiuliza, hivi ilikuwa ni kwa faida ya nani Rais Magufuli na wapambe wake kuficha ukweli kuwa miradi ya reli, barabara, umeme, ujenzi wa hospitali na mingine mingi aliyoijenga alikuwa anakopa?

Hivi sisi kama tungejua anakopa, tungemzuia? Lakini si tungepata fursa ya kumshauri asichukue mikopo ya kibiashara inayoanza kututoa utumbo sasa? Mungu ibariki Tanzania.

Copyright ©2021. Gazeti la Jamhuri
Wale wajinga wenye akili kama punje ya sukari..watakuja hapa kupinga na kutetea ujinga uliofanywa na malaika muovu
 
Majibu yake ni marahisi.
Mabenki ya biashara hayana masharti magumu kama ilivyo IMF na WB.
IMF na WB wanaweza kukukopesha lkn wanakupa masharti magumu kama vile kufutilia mbali baadhi ya taasisi za umma.
Kukuelekeza miradi ya kufanyia fedha wanayokukopesha, watakuambia usiajiri kwa miaka kadhaa, watakuambia ongeza kodi katika eneo na samehe kodi katika eneo hili.
Yaani ni vurugu tupu. Unakuwa unaendeshwa kama mashine.
Watu hawataki kusikia haya...Wapo tu kuwaza yao ya kisiasa....
 
Nadhani upo Ubelgiji. Utakaporudi tafuta mtu wa kukupitisha pale mataa usije ukapotea.
Kumbuka nimesema mradi ambao ni "matunda ya JPM"!!

Hapo mataa ni wapi?! Kama ni Ubungo, na kwavile wengi reference yenu ni interchange... ule ni mradi wa BRT!!

Mnaona imejengwa wakati wa JPM kwa sababu, mwanzoni BRT Design ilihusisha kuweka traffic lights tu pale makutano! Hata hivyo, mabasi ya BRT ndiyo yalikuwa yamependelewa kwenye plan ile, kwa maana, gari zingine ZOOOTE hazikutakiwa kupinda kulia wakishafika pale mataa!

Kwa mfano, kama gari inatoka Buguruni na inaenda town, ilitakiwa ikifika mataa, wale kushoto kama wanaenda Kimara kisha huko mbele wakapige U-turn na kushika lane ya kwenda town!

In 2013, TANROAD wakaona wamechemka kwa hiyo design kwa sababu ingeleta balaa(congestion) kubwa sana pale Ubungo Mataa.

Kutokana na hilo, TANROADS wakaamua kuandaa design na proposal nyingine ambayo waliwasilisha kwa JK. Sasa kwavile World Bank ndio financier wa BRT, kama kawaida yake ya kutochoka kujikomba, JK akaagiza warudi tena World Bank; na World Bank wakakubali ku-finance ujenzi wa interchange baada ya kukubaliana na hoja zilizotolewa!

Sasa kazi kubwa afanye mwingine, credit aje kupewa mwingine?! Mbona Samia anavyotoa pesa kwa ajili ya SGR na Nyerere Dams, mbona hamumpi credit zake lakini zote zinaenda kwa JPM?

Kwa sababu ukweli ni kwamba, ni JPM ndie ana-deserve hizo credits kwa sababu ndie kafanya kazi kubwa kuhakikisha miradi hiyo inasimama!!! Hata mkataba wa juzi wa kununua ndege zingine (kwangu naona ni jambo la ovyo, except kwa ndege ya mizigo), bado credit zinaenda kwa JPM kwa sababu ndie alihakikisha suala hilo linafanyika!
 
I knew it, lile zee lilikuwa baba la uongo, ona sasa linaumbuka.
Yaani Magu sikuwahi kabisa kumuamini, na mara zote niliamini sijawahi kuingia king na uongo wake wowote ule ... kumbe nilikuwa najidanganya aisee!!!

Pamoja na kufuatilia kwangu kote kwa haya mambo, Magu aliniamnisha kabisa kwamba ndege zimenunuliwa cash kwa pesa zetu!!

Juzi nasoma ripoti ya PAC ndo nakuja kushangaa ndege nazo ni mkopo wa zaidi ya Sh 800 Billion... NIKACHOKA!!
 
Kumbuka nimesema mradi ambao ni "matunda ya JPM"!!

Hapo mataa ni wapi?! Kama ni Ubungo, na kwavile wengi reference yenu ni interchange... ule ni mradi wa BRT!!

Mnaona imejengwa wakati wa JPM kwa sababu, mwanzoni BRT Design ilihusisha kuweka traffic lights tu pale makutano! Hata hivyo, mabasi ya BRT ndiyo yalikuwa yamependelewa kwenye plan ile, kwa maana, gari zingine ZOOOTE hazikutakiwa kupinda kulia wakishafika pale mataa!

Kwa mfano, kama gari inatoka Buguruni na inaenda town, ilitakiwa ikifika mataa, wale kushoto kama wanaenda Kimara kisha huko mbele wakapige U-turn na kushika lane ya kwenda town!

In 2013, TANROAD wakaona wamechemka kwa hiyo design kwa sababu ingeleta balaa(congestion) kubwa sana pale Ubungo Mataa.

Kutokana na hilo, TANROADS wakaamua kuandaa design na proposal nyingine ambayo waliwasilisha kwa JK. Sasa kwavile World Bank ndio financier wa BRT, kama kawaida yake ya kutochoka kujikomba, JK akaagiza warudi tena World Bank; na World Bank wakakubali ku-finance ujenzi wa interchange baada ya kukubaliana na hoja zilizotolewa!

Sasa kazi kubwa afanye mwingine, credit aje kupewa mwingine?! Mbona Samia anavyotoa pesa kwa ajili ya SGR na Nyerere Dams, mbona hamumpi credit zake lakini zote zinaenda kwa JPM?

Kwa sababu ukweli ni kwamba, ni JPM ndie ana-deserve hizo credits kwa sababu ndie kafanya kazi kubwa kuhakikisha miradi hiyo inasimama!!! Hata mkataba wa juzi wa kununua ndege zingine (kwangu naona ni jambo la ovyo, except kwa ndege ya mizigo), bado credit zinaenda kwa JPM kwa sababu ndie alihakikisha suala hilo linafanyika!
Mungu ameliokowa hili Taifa bila umwagaji damu, tunapaswa kumpa Mungu shukrani.

Kama Watanzania tunashindwa kumwambia Mungu asante kwa kutuondolea kiumbe katili alijejipachika mamlaka ya umungu mtu basi nchi yetu haitobalikiwa.

Mimi ndio maana sina tatizo na huyu mama naona wanasiasa wanamwingia kwa wrong timing tu, lakini mwendakuzimu alikuwa ni shetani, mpenda sifa na wengine waonekane si lolote si chochote.
 
Wewe Balile acha unafiki! Mama kakopa hela ya UVICO na ile miradi ni kudanyanya wananchi ili waone anafanya kazi! Nambie sasa miezi sita angalia mwenendo wa miradi inavyosuasua mfano, Ujenzi wa barabara nyingi unasuasua hata mwendo kasi Dar bila shaka unaona, ujenzi wa madaraja makubwa kama Mto wami na Busisi!

Kwa ujumla hakuna jipya! Huo mkopo unaodai ukweli na uwazi ni mkopo wa Corona na kwa taarifa yako pamoja na tozozote ila mapato yamepungua ila kwenye media mnaambia anakusanya trilion karibia mbili kwa mwezì!
Huyu Balile anatumika kumsafisha Samia,unaweza kuona uandishi wake,hawa waandishi ndo maana Mkapa alikuwa anawatukana
 
Kumbuka nimesema mradi ambao ni "matunda ya JPM"!!

Hapo mataa ni wapi?! Kama ni Ubungo, na kwavile wengi reference yenu ni interchange... ule ni mradi wa BRT!!

Mnaona imejengwa wakati wa JPM kwa sababu, mwanzoni BRT Design ilihusisha kuweka traffic lights tu pale makutano! Hata hivyo, mabasi ya BRT ndiyo yalikuwa yamependelewa kwenye plan ile, kwa maana, gari zingine ZOOOTE hazikutakiwa kupinda kulia wakishafika pale mataa!

Kwa mfano, kama gari inatoka Buguruni na inaenda town, ilitakiwa ikifika mataa, wale kushoto kama wanaenda Kimara kisha huko mbele wakapige U-turn na kushika lane ya kwenda town!

In 2013, TANROAD wakaona wamechemka kwa hiyo design kwa sababu ingeleta balaa(congestion) kubwa sana pale Ubungo Mataa.

Kutokana na hilo, TANROADS wakaamua kuandaa design na proposal nyingine ambayo waliwasilisha kwa JK. Sasa kwavile World Bank ndio financier wa BRT, kama kawaida yake ya kutochoka kujikomba, JK akaagiza warudi tena World Bank; na World Bank wakakubali ku-finance ujenzi wa interchange baada ya kukubaliana na hoja zilizotolewa!

Sasa kazi kubwa afanye mwingine, credit aje kupewa mwingine?! Mbona Samia anavyotoa pesa kwa ajili ya SGR na Nyerere Dams, mbona hamumpi credit zake lakini zote zinaenda kwa JPM?

Kwa sababu ukweli ni kwamba, ni JPM ndie ana-deserve hizo credits kwa sababu ndie kafanya kazi kubwa kuhakikisha miradi hiyo inasimama!!! Hata mkataba wa juzi wa kununua ndege zingine (kwangu naona ni jambo la ovyo, except kwa ndege ya mizigo), bado credit zinaenda kwa JPM kwa sababu ndie alihakikisha suala hilo linafanyika!
Tatizo la kila moja wenu ni kuhangaika na personalities za watu na upambe ambo wengi ni nuksi na sababu kubwa ya viongozi kuchukiwa na raia...Kwanini mnapambanisha marais?

JK awamu yake iliisha ambapo wote JPM na Mama Samia walikuwa sehemu ya awamu hiyo...Tatizo ni ninyi wapambe, acheni kujitoa akili...Tanzania ni ya sisi sote...Na mtu akisifiwa haiondoi sifa ya mwingine...
 
Back
Top Bottom