Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Sasa kama Hayati Magufuli alikopa sana, ni kwanini Rais wa sasa na yeye anaendelea kukopa?

Tufike pahala tuache upambe na chuki na kisha tuwe wakweli kwa maendeleo ya nchi yetu.
Nchi inamadeni alafu tunaendelea kukopa kwa kigezo kuwa deni letu ni stahimilivu!?

Tufike pahali sasa tujifunge mkanda, tuanze na kupunguza mishahara minono ya viongozi, zahara zote zisizo na tija zifutwe mfano:- Barabara imejengwa ikakamili alafu kiongozi anakwenda kuizindua kwa ziara yenye gharama kubwa.
Serikali iache kutumia magari ya gharama (V8) nk

Nina amini kama serikali itaamua kuacha matumizi ya anasa basi kwa kiasi hiki hiki ambacho kodi hukusanywa deni litalipwa.

Ila kama wananchi tutaendelea na ushabiki maandazi kwa hiki chama cha ccm basi siku moja tutajikuta nchi imeuzwa.
Nchi bora iuzwe kila mtu achukue chake ujinga na ushabiki mandazi umezodi
 
Dhana ya kuminya Uhuru wahabari utoaji takwimu ilikua kwajili ya Hilo na sivinginevyo uchaguzi 2015 uliimaliza ccm
 
Tatizo la kila moja wenu ni kuhangaika na personalities za watu na upambe ambo wengi ni nuksi na sababu kubwa ya viongozi kuchukiwa na raia...Kwanini mnapambanisha marais?

JK awamu yake iliisha ambapo wote JPM na Mama Samia walikuwa sehemu ya awamu hiyo...Tatizo ni ninyi wapambe, acheni kujitoa akili...Tanzania ni ya sisi sote...Na mtu akisifiwa haiondoi sifa ya mwingine...
Unaumilia maumivu kutokea pande zipi za dunia?!

Hakuna nilipopambanisha mtu, unalilia kwamba napambanisha marais... je, nikipambanisha?!

Na hivi nilivyokuwa na database ya facts si ndo utazidi kuumia!!
 
Mungu ameliokowa hili Taifa bila umwagaji damu, tunapaswa kumpa Mungu shukrani.

Kama Watanzania tunashindwa kumwambia Mungu asante kwa kutuondolea kiumbe katili alijejipachika mamlaka ya umungu mtu basi nchi yetu haitobalikiwa.

Mimi ndio maana sina tatizo na huyu mama naona wanasiasa wanamwingia kwa wrong timing tu, lakini mwendakuzimu alikuwa ni shetani, mpenda sifa na wengine waonekane si lolote si chochote.
Hata kama watu wanajifanya hawaoni lakini ukweli ndo huo... tulikuwa tunaelekea pabaya!!

Mara zote niliamini JK ndo rais msaanii zaidi kuwahi kutokea Tanzania, na asingetokea mwingine zaidi yake! Baada ya kuja JPM, ndo nikaja kugundua kwa usanii, JK cha mtoto!!

Na zile gia zake za kujifanya ana uchungu na wanyonge, basi akawageuza wengi kuwa ndondocha wake wa kuamini kila anachowaambia!!!

Eti kuna wengine wanatoa povu hata kwa hii habari ya Balile wakati Balile katumia takwimu za hiyo hiyo serikali lakini HAWATAKI... wanachukulia mambo yote too personal!!! Hapo wanaona ni chuki tu bila kuangalia facts zilizotolewa
 
Hata kama watu wanajifanya hawaoni lakini ukweli ndo huo... tulikuwa tunaelekea pabaya!!

Mara zote niliamini JK ndo rais msaanii zaidi kuwahi kutokea Tanzania, na asingetokea mwingine zaidi yake! Baada ya kuja JPM, ndo nikaja kugundua kwa usanii, JK cha mtoto!!

Na zile gia zake za kujifanya ana uchungu na wanyonge, basi akawageuza wengi kuwa ndondocha wake wa kuamini kila anachowaambia!!!

Eti kuna wengine wanatoa povu hata kwa hii habari ya Balile wakati Balile katumia takwimu za hiyo hiyo serikali lakini HAWATAKI... wanachukulia mambo yote too personal!!! Hapo wanaona ni chuki tu bila kuangalia facts zilizotolewa
wenye akili tunajua mchawi hapa ni ccm hii mideni itatua kabla ya muda wetu
 
wenye akili tunajua mchawi hapa ni ccm hii mideni itatua kabla ya muda wetu
Na mbaya zaidi... hili ni trela tu!!

Mradi wa SGR bado sana!! Kwahiyo tutaendelea kukopa maradufu kwa ajili ya SGR!!!

Hata Bwawa la Nyerere, bado!!! Kwahiyo tutaendelea kukopa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi!!

Na kwavile kote huko tunatumia mikopo ya kibiashara... it's a matter of time kabla hatujaanza kutafutana!!!
 
Mzee wakati wa Mwendazake hiyo tovuti ya BoT si ilikuwepo, mbona hukuitumia na kuleta taarifa kama hizi? Nakumbuka kuna wakati gazeti lako lilisifiwa hadharani na JPM kwa kuibua uozo sijui bandarini ama wapi lakini hili ambalo unasema linatutoa utumbo hukulisema. Leo ndio umeliona, kweli ya Mungu mengi.
Kwani yeye ni mpumbavu. Ulitaka ajipige Risasi mwenyewe. Wakati wa Magufuli nani alikuwa jasiri mbele ya kifo
 
Mzee wakati wa Mwendazake hiyo tovuti ya BoT si ilikuwepo, mbona hukuitumia na kuleta taarifa kama hizi? Nakumbuka kuna wakati gazeti lako lilisifiwa hadharani na JPM kwa kuibua uozo sijui bandarini ama wapi lakini hili ambalo unasema linatutoa utumbo hukulisema. Leo ndio umeliona, kweli ya Mungu mengi.
Anatafuta teuzi kwa nguvu, anasema kazi ya uandishi wa habari ni kuibua ukweli, mbona kipindi chote alikuwa kimya Sasa hivi ndio anajifanya anajua wajibu wake.
 
Kwani yeye ni mpumbavu. Ulitaka ajipige Risasi mwenyewe. Wakati wa Magufuli nani alikuwa jasiri mbele ya kifo
Shujaa huwa halilii bunduki! Kama aliogopa basi aendelee kuogopa badala ya kuleta unafiki
 
Mzee wakati wa Mwendazake hiyo tovuti ya BoT si ilikuwepo, mbona hukuitumia na kuleta taarifa kama hizi? Nakumbuka kuna wakati gazeti lako lilisifiwa hadharani na JPM kwa kuibua uozo sijui bandarini ama wapi lakini hili ambalo unasema linatutoa utumbo hukulisema. Leo ndio umeliona, kweli ya Mungu mengi.
Wapo waliojitokeza kumkabili Magufuli na kumwambia live, kupitia press conferences na hata bungeni (Tundu Lissu), kupitia mitandaoni tena kwa kutumia majina yao halisi (Ben Saanane), kupitia taratibu za kikazi ( Prof. Assad na Prof. Benno Ndulu). Kwa kweli waliothubutu kumkabili NDULI Magufuli hawakuwa wengi, na sababu ni majanga yaliyowakuta hao waliothubutu.
Tundu Lissu alinusurika kuwa executed kwa muujiza wa Mungu tu. Ben Saanane hakuwa na bahati hiyo. Assad alikumbana na misukosuko kibao, na Prof. Ndulu pia.

Wapo ambao naweza kuwaita wanafiki, mfano Spika Ndugai. Lakini wale wa aina ya Balile wala siwalaumu. Kama walishindwa kutimiza wajibu wao wakati ule, wakiutimiza sasa hivi kuna shida gani?
Hata hivyo mimi na wewe hatuwezi kulinganishwa na watu aina ya Balile. Wao wanaongea kwa majina yao halisi. Mimi na wewe tunaojificha kwenye keyboard tunapata wapi ujasiri wa kuwakosoa??
 
Magufuli katutenda deni la taifa, trilioni 78 Samia msalabani

Jamhuri October 26, 2021

Na Deodatus Balile

Kazi hii ya uandishi wa habari moja ya majukumu yake ni kuanika ukweli minong’ono inapotawala katika jamii.

Kwa sasa kuna minong’ono mingi. Minong’ono imeanza baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza hadharani mkopo wa Sh trilioni 1.3, alioukopa kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na akatangaza miradi lukuki itakayotekelezwa kwa kutumia mkopo huo.

Miongoni mwa miradi ya kihistoria ni ujenzi wa madarasa ya sekondari 15,000 nchi nzima na madarasa ya shule za msingi 3,000.

Kwa sasa inakadiriwa kuwa nchi ina upungufu wa madarasa 11,000, lakini Rais Samia ameamua kuona mbali.

Ameamua kufuta mfumo wa zima moto, ambapo kila mwaka wazazi wanakabwa koo vijijini kuchangia ujenzi wa madarasa.

Baadhi ya wazazi pia wameanza minong’ono kuwa watoto wao wamepewa mikopo kidogo, yaani Sh 600,000 kama ada vyuoni.

Hawajui kuwa miaka yote imekuwa hivyo na wakati mwingine wengi wanakuwa hawapati kabisa hata senti tano ya mkopo.

Sitanii, naomba nizungumzie kwa ufupi miezi sita ya Rais Samia akiwa Rais wa Tanzania baada ya kuapishwa Machi 19, 2021.

Nakumbuka vema kilichotokea, maana baada ya kifo cha Rais John Magufuli kulitokea kama sintofahamu hivi.
Wapo watu walioamini Rais Samia angeendelea kuwa Kaimu Rais, baadhi walidhani tunakwenda kwenye uchaguzi mpya na wengine hawakufahamu nini kitatokea.

Asubuhi ya Machi 18, 2021 niliamkia studio za Televisheni ya Taifa (TBC1) na TBC Taifa (radio) kufanya mahojiano na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba.

Hii ilikuwa ni baada ya kifo cha Rais John Magufuli, kilichotokea Machi 17, 2021. Ikumbukwe wiki moja kabla nilikuwa nimefanya mahojiano na kituo cha Star TV nikasema tuambiwe bayana Rais Magufuli yuko wapi na anafanya nini.

Machi 18 pamoja na kwamba nilikuwa bado Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), ambapo baadaye nilichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TEF Mei 22, 2021, ilinilazimu kutoa ufafanuzi huo uliokuwa tamko zito.

Sitanii, tamko nililolitoa lilizaa kuapishwa kwa Rais Samia kuwa Rais wa Awamu ya Sita Machi 19, 2021. Nilirejea Katiba ya Tanzania (1977) Ibara ya 37(5) inayosema: “Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya 40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka Rais atapendekeza jina la mtu atakayekuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua asilimia hamsini ya wabunge wote.”

Kwa mara ya kwanza kupitia makala hii ninakisema kilichotokea baada ya tamko hilo. Walinipigia simu watu wengi wakiwa na hofu.

Baadhi hawakufahamu Katiba inasemaje. Walinishutumu wakidai nimetangaza utaratibu wa kwangu, kwani baada ya kifo cha Rais kinachofuata ni uchaguzi.

Hii ilinipa shida kuona hata baadhi ya wabunge hawakufahamu nini kinafuata baada ya kifo hicho. Machi 18, 2021 itabaki kuwa siku ya kihistoria kwangu, kwani ujumbe nilioutoa ulitangazwa katika radio zote za ndani na za kimataifa na siku moja baadaye Rais Samia akaapishwa.

Sitanii, leo ninazungumzia mzigo wa madeni ambao Rais Magufuli amelitwisha taifa letu. Nimetangulia kusema na ninarudia, mimi ni msema kweli. Wala sipepesi macho katika kusema ukweli.

Wakati Rais Magufuli kwa miaka mitano yote alikuwa anawaaminisha Watanzania kuwa nchi inajenga miundombinu na inanunua ndege kwa kutumia fedha zetu wenyewe, uhalisia ni kinyume chake.

Kwa kipindi cha miaka mitano tu, Rais Mafuguli amekopa fedha nyingi kuliko fedha zote alizokopa Rais Benjamin Mkapa kwa miaka 10 aliyokaa madarakani.

Kwa miaka mitano, amekopa pia fedha nyingi kuliko alizokopa Rais Jakaya Kikwete kwa miaka 10 naye aliyokaa madarakani.

Rais Mkapa alirithi madeni mengi mno. Alipambana nayo, akaiingiza nchi katika Mpango wa Kusamehe Madeni Nchi Maskini (HIPC) na hadi anatoka madarakani, Tanzania ilikuwa inadaiwa Sh trilioni 20 tu.

Rais Kikwete wakati wake deni la taifa liliongezeka kwa Sh trilioni 23, hivyo akatoka madarakani deni la taifa likiwa Sh trilioni 43 kwa miaka 10. Rais Magufuli kwa miaka mitano tu, deni la taifa limeongezeka kwa Sh trilioni 29 na kufikia Sh trilioni 72 hadi anafariki dunia Machi, 2021.

Sitanii, kwa kasi hii ya ukopaji ina maana kama angekaa madarakani kwa miaka 10 kamili na akaendelea na kasi ya ukopaji wa wastani wa Sh trilioni 29 kwa miaka mitano, basi angetoka madarakani deni la taifa likiwa Sh trilioni 101 kufikia mwaka 2025.

Kuna jambo baya halisemwi. Rais Magufuli amekopa mikopo ya kibiashara inayoanza kulipwa baada ya miaka mitatu na inapaswa kulipwa ndani ya miaka minane, ikiwa na riba za kati ya asilimia 6 na 8.

Baadhi ya mikopo hii imeiva tayari. Imeanza kukuza deni la taifa kwa kasi kutokana na riba. Deni la taifa sasa limefikia Sh trilioni 78.

Kwa vyovyote vile iwavyo, Rais Samia anapaswa kuchukua hatua za haraka, ikiwamo kuunda timu ya majadiliano na wakopeshaji kwa ajili ya kubadili masharti ya mikopo ya kibiashara aliyochukua Rais Magufuli.

Anapaswa kuomba msamaha wa riba na pengine kuomba kuongezewa muda wa kulipa deni kama ulivyo utaratibu wa mikopo kwa serikali nyingi duniani.

Mikopo mingi kwa serikali huwa inalipwa kati ya miaka 20 hadi 50 kulingana na ukubwa wa mkopo na hutozwa riba kati ya asilimia 0.3 hadi asilimia 1. Mikopo ya aina hii inapatikana katika Benki ya Dunia, Shirika la Maendeleo Duniani, Benki ya Maendeleo Afika na nyingine za aina hii.

Kwa bahati mbaya na kwa masikitiko makubwa, kwa miaka mitano Wazungu tuliowaita mabeberu, ila tukawa tunakopa fedha zao kupitia benki za biashara. Kwa hali halisi, madeni haya yakiiva yote, ikiwa hakuna majadiliano ya dharura kuomba marekebisho ya masharti ya mikopo tuliyochukua chini ya Rais Magufuli, itafika mahala asilimia 60 ya bajeti ya taifa letu itakuwa inakwenda kulipa madeni. Waliomo serikalini watajua la kufanya katika hili.

Sitanii, ninafahamu baadhi ya wasomaji watakuwa wanaanza kufuka moshi kwa kusema ukweli huu. Wanajiuliza taarifa hizi nimezipata wapi? Taarifa hizi si za siri. Ziko wazi kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Nimepitia taarifa za mapitio ya mwenendo wa uchumi tangu mwaka 2000 hadi 2021. Zipo mtandaoni na zinaonyesha deni lilivyokua hatua kwa hatua. Kwa nia ya kuweka uelewa unaofanana, ifuatayo ni hali ya deni la taifa tangu mwaka 2005 hadi 2021.

Oktoba 2005, deni la nje lilikuwa USD milioni 8,361.9 sawa na Sh 19,286,471,493,000 na deni la ndani lilikuwa Sh 1,712,800,000,000. Jumla kuu ya deni wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani lilikuwa Sh 20,999,271,493,000 (Sh trilioni 20.9). Nimekokotoa hesabu hizi kwa kutumia viwango vya BoT vya kuuza dola ya Marekani ambavyo ni USD 1 kwa Sh 2,306.47.

Oktoba 2015, wakati Rais Kikwete anatoka madarakani deni la nje lilikuwa USD milioni 15,321.3, sawa na Sh 35,338,118,811,000 na deni la ndani lilikuwa Sh 7,826,200,000,000. Jumla kuu deni la nje na deni la ndani lilikuwa ni Sh 43,164,318,811,000 (Sh trilioni 43.1).

Deni la taifa lilianza kupanda kwa kasi Oktoba 2016. Deni la nje lilipanda na kuwa USD milioni 16,407.6 sawa na Sh 37,843,637,172,000, huku deni la ndani nalo likipanda na kuwa Sh 10,089,000,000,000. Jumla kuu ya deni ikafikia Sh 47,932,637,172,000 (Sh trilioni 47.9).

Oktoba 2017 deni la nje lilipanda kwa kasi kubwa na kufikia USD milioni 19,074.4 sawa na Sh 43,994,531,368,000. Kutokana na makandarasi kutolipwa deni la ndani nalo lilikua na kufikia Sh 12,563,300,000,000. Jumla kuu ya deni kwa mwaka huo likawa Sh 56,557,831,368,000 (Sh trilioni 56.5).

Oktoba 2018, deni la nje lilizidi kupanda na kuwa USD milioni 20,759.1 sawa na Sh 47,880,241,377,000, huku deni la ndani nalo likipanda na kuwa Sh 14,116,100,000,000. Jumla kuu ikawa Sh 61,996,341,377,000 (Sh trilioni 61.9).

Oktoba 2019, mwanamume aliongeza tena deni la taifa, deni la nje likafikia USD milioni 22,569.4, sawa na Sh 52,055,644,018,000, huku deni la ndani likipanda na kufikia Sh 14,187,400,000,000. Jumla kuu ya deni ikafikia Sh 66,243,044,018,000 (Sh trilioni 66.2).

Oktoba 2020, deni la nje lilipanda na kufikia USD milioni 23,599.3, sawa na Sh 54,431,077,471,000, huku deni la ndani likifikia Sh 15,608,500,000,000. Jumla kuu ikafikia Sh 70,039,577,471,000 (Sh trilioni 70).

Machi, 2021 wakati Rais Magufuli anafariki dunia, deni la nje la Tanzania lilikuwa limefikia USD milioni 24,429.2, sawa na Sh 56,345,216,924,000. Deni la ndani nalo lilipanda na kufikia Sh 16,116,500,000,000. Jumla kuu, deni la taifa lilifikia 72,461,716,924,000 (Sh trilioni 72.4).

Kilichofuata baada ya hapo, madeni yameanza kuiva kwa ajili ya kulipwa, huku mengine yakizalisha riba ya kufa mtu.

Makandarasi wengi Tanzania wanadai mabilioni kati ya hizo Sh trilioni 16 ambazo ni deni la ndani hawajalipwa siku nyingi. Kutokana na hali hiyo, madeni haya yaliyokopwa bila mpangilio katika benki za biashara yameanza kuwa msalaba kwa Rais Samia.

Taarifa ya hali ya Uchumi ya BoT ya Septemba, 2021 inayorejea mwezi Agosti, 2021 kutokana na mazingira hayo, deni la nje limekua na kufikia USD milioni 25,956.1 sawa na Sh 59,866,965,967,000, huku deni la ndani nalo likikua na kufikia Sh 18,225,000,000,000. Ukuaji huu unafanya kiwango cha deni la taifa kufikia jumla kuu ya Sh 78,091,965,967,000 (trilioni 78).

Sitanii, deni hili likigawanywa kwa Watanzania milioni 60, bila kujali mkubwa na mdogo, kila Mtanzania anadaiwa Sh 1,301,533 (Sh milioni 1.3). Hata hivyo, wataalamu wa uchumi wanasema deni hili si tishio kwa uchumi wa taifa letu kwa sasa kwani liko katika uwiano wa asilimia 30 kwa uchumi wa taifa letu, wakati kuna mataifa Afrika ambayo tayari yana uwiano wa asilimia 54 ya deni kwa uchumi wa nchi zao, ila wanaionya serikali iepuke mikopo ya kibiashara ina riba kubwa, masharti mabaya na inalipwa kwa muda mfupi.

Pale Dodoma, tumeona Rais Samia ameanzisha utaratibu mpya wa ukweli na uwazi katika mikopo. Ameeleza fedha alizokopa zitafanya nini kwa kuorodhesha miradi itakayotekelezwa na akatueleza amezikopa kutoka wapi.

Ninajiuliza, hivi ilikuwa ni kwa faida ya nani Rais Magufuli na wapambe wake kuficha ukweli kuwa miradi ya reli, barabara, umeme, ujenzi wa hospitali na mingine mingi aliyoijenga alikuwa anakopa?

Hivi sisi kama tungejua anakopa, tungemzuia? Lakini si tungepata fursa ya kumshauri asichukue mikopo ya kibiashara inayoanza kututoa utumbo sasa? Mungu ibariki Tanzania.

Copyright ©2021. Gazeti la Jamhuri
CC: joto la jiwe
 
Wapo waliojitokeza kumkabili Magufuli na kumwambia live, kupitia press conferences na hata bungeni (Tundu Lissu), kupitia mitandaoni tena kwa kutumia majina yao halisi (Ben Saanane), kupitia taratibu za kikazi ( Prof. Assad na Prof. Benno Ndulu). Kwa kweli waliothubutu kumkabili NDULI Magufuli hawakuwa wengi, na sababu ni majanga yaliyowakuta hao waliothubutu.
Tundu Lissu alinusurika kuwa executed kwa muujiza wa Mungu tu. Ben Saanane hakuwa na bahati hiyo. Assad alikumbana na misukosuko kibao, na Prof. Ndulu pia.

Wapo ambao naweza kuwaita wanafiki, mfano Spika Ndugai. Lakini wale wa aina ya Balile wala siwalaumu. Kama walishindwa kutimiza wajibu wao wakati ule, wakiutimiza sasa hivi kuna shida gani?
Hata hivyo mimi na wewe hatuwezi kulinganishwa na watu aina ya Balile. Wao wanaongea kwa majina yao halisi. Mimi na wewe tunaojificha kwenye keyboard tunapata wapi ujasiri wa kuwakosoa??
Ni vyema kusimamia unachokiamini muda wote badala ya kuwa mnafiki. Mbona hakuogopa alipoandika madudu ya Bandari na JPM akawasifu. Kama walikuwa wanaogopa basi wangenyamaza kimya pia kwa hilo.
 
Duuh ndio maana wamerudisha stika za usalama bara barani wanatafuta kila sehemu ya kuchanga hela...
 
Mama Samia anaubunifu? Yeye alishasema kazi yake ni kuangali graph! Sasa hapo ujiongeze nini kitatokea? Mama samia tumwache apambane kivyake msije hapa kumtetea wakati mwenzake JPM alikopa na akafanya vitu vya kuonekana!
Tembelea serikali za mitaa uone anavyomwaga pesa. Hana mbwembwe wala majivuno hivyo unaweza ukawa haufahamu.
 
Tupe na thamani ya miradi iliyotokana na deni, kama uwiano wa deni na uchumi kukua ni 30% huko kutendwa kunatokeaje?

Anzia upanuzi wa bandari, SGR, Upanuzi wa highways, mabarabara ya mitaa, stand za mabasi nchi nzima, New mwendokasi roads, vituo vya afya nchi nzima, Hospitali za wilaya nchi nzima, Mashule, Ndege, upanuzi wa viwanja, ujenzi wa Dodoma plus Ikulu ya Chamino, usambazaji umeme kila kijiji, vivutio vya utalii, Hydropower ya Nyerere na vingine vingi. Ulitegemea hela haitumiki?

Then go back angalia uwiano wa uchumi na ukuaji wa madeni! Njoo kwenye probability means of return. Angalia makusanyo per annual sio kuandika kinafiki.
Mkuu, hata kama Magu kafanya yote hayo, kama kulikuwa na uwezekano wa kufanya mengi zaidi, kwa gharama nafuu zaidi, kuna ubaya gani kusema?

Kwa mfano, katika ujenzi wa SGR, Wabunge wa upinzani walipendekeza kitumike chuma cha kwetu, badala ya kuagiza toka nje. Nadhani kwa kuwa Magufuli alikuwa na haraka ili aonekane kafanya yeye, alikataa. Kitaifa tungefaudika zaidi kuvuna chuma chetu, na kwa maslahi ya muda mrefu. Ila alifanya hivyo kwa maslahi binafsi. Ingechukua muda zaidi kuanza. Matokeo yake gharama kubwa inatumika. Pia financing ya SGR kulikuwa na better options. Sasa hivi miaka 6, bado hatujaanza kutumia Dar - Moro.

Kamati ya Bunge inayohusika na bajeti, chini ya Hawa Ghasia, waliwahi kuhoji iweje serikali inatumia zaidi commercial loans, ambazo zina riba kubwa zaidi na zinaiva mapema, badala ya concessional loans ambazo riba ni ndogo zaidi na maturity ndefu zaidi.

Bila shaka ubabe na nia ovu zilimvuta zaidi kwenye commercial loans.

Pia hii habari ya kununua ndege cash, kuna catch-22 ambayo ina harufu mbaya. Ukinunua bila cash, kuna njia nyingi, inabidi uwe na Business Plan, ambayo itaonesha utakavyofanya ili mradi uwe na mafanikio. Lakini ukinunua cash, hata ukiipaki ndege miaka 3, hakuna shida.

Pia Magufuli alikuwa Fisadi wa kupindukia. Alipata wapi fedha za uwekezaji mkubwa vile kule Chato, bilakupitia bajeti? Kiwanja cha ndege, navingine vingi ?
 
Tupe na thamani ya miradi iliyotokana na deni, kama uwiano wa deni na uchumi kukua ni 30% huko kutendwa kunatokeaje?

Anzia upanuzi wa bandari, SGR, Upanuzi wa highways, mabarabara ya mitaa, stand za mabasi nchi nzima, New mwendokasi roads, vituo vya afya nchi nzima, Hospitali za wilaya nchi nzima, Mashule, Ndege, upanuzi wa viwanja, ujenzi wa Dodoma plus Ikulu ya Chamino, usambazaji umeme kila kijiji, vivutio vya utalii, Hydropower ya Nyerere na vingine vingi. Ulitegemea hela haitumiki?

Then go back angalia uwiano wa uchumi na ukuaji wa madeni! Njoo kwenye probability means of return. Angalia makusanyo per annual sio kuandika kinafiki.
Makusanyo ya wapi propagamda tupu
 
Hata kama watu wanajifanya hawaoni lakini ukweli ndo huo... tulikuwa tunaelekea pabaya!!

Mara zote niliamini JK ndo rais msaanii zaidi kuwahi kutokea Tanzania, na asingetokea mwingine zaidi yake! Baada ya kuja JPM, ndo nikaja kugundua kwa usanii, JK cha mtoto!!

Na zile gia zake za kujifanya ana uchungu na wanyonge, basi akawageuza wengi kuwa ndondocha wake wa kuamini kila anachowaambia!!!

Eti kuna wengine wanatoa povu hata kwa hii habari ya Balile wakati Balile katumia takwimu za hiyo hiyo serikali lakini HAWATAKI... wanachukulia mambo yote too personal!!! Hapo wanaona ni chuki tu bila kuangalia facts zilizotolewa
Mafisadi lazima mjipe moyo...poleni nchi hii hairudi tena kwenye mikono yenu hata mkatambikie makaburi ya babu zenu...Kama alivyoingia 2015 bado Mungu anampango na nchi hii
 
Mkuu, hata kama Magu kafanya yote hayo, kama kulikuwa na uwezekano wa kufanya mengi zaidi, kwa gharama nafuu zaidi, kuna ubaya gani kusema?

Kwa mfano, katika ujenzi wa SGR, Wabunge wa upinzani walipendekeza kitumike chuma cha kwetu, badala ya kuagiza toka nje. Nadhani kwa kuwa Magufuli alikuwa na haraka ili aonekane kafanya yeye, alikataa. Kitaifa tungefaudika zaidi kuvuna chuma chetu, na kwa maslahi ya muda mrefu. Ila alifanya hivyo kwa maslahi binafsi. Ingechukua muda zaidi kuanza. Matokeo yake gharama kubwa inatumika. Pia financing ya SGR kulikuwa na better options. Sasa hivi miaka 6, bado hatujaanza kutumia Dar - Moro.

Kamati ya Bunge inayohusika na bajeti, chini ya Hawa Ghasia, waliwahi kuhoji iweje serikali inatumia zaidi commercial loans, ambazo zina riba kubwa zaidi na zinaiva mapema, badala ya concessional loans ambazo riba ni ndogo zaidi na maturity ndefu zaidi.

Bila shaka ubabe na nia ovu zilimvuta zaidi kwenye commercial loans.

Pia hii habari ya kununua ndege cash, kuna catch-22 ambayo ina harufu mbaya. Ukinunua bila cash, kuna njia nyingi, inabidi uwe na Business Plan, ambayo itaonesha utakavyofanya ili mradi uwe na mafanikio. Lakini ukinunua cash, hata ukiipaki ndege miaka 3, hakuna shida.

Pia Magufuli alikuwa Fisadi wa kupindukia. Alipata wapi fedha za uwekezaji mkubwa vile kule Chato, bilakupitia bajeti? Kiwanja cha ndege, navingine vingi ?
Fisadi anawekeza kwenye public goods mie binafsi namuunga mkono....
 
Tuliambiwa tozo zitajenga vituo vya afya shule umeme maji lakn tunakopa kwa ajil ya shule afya maj umeme

Hapo ndyo mnatuchanganya sisi darasa la Saba B

..serikali iwe inatoa ufafanuz wa lugha nyepesi kwa sisi la 7B tuweze kuelewa ..
 
Back
Top Bottom