mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,309
- 4,798
Miezi 14 baada ya kuvuliwa uanachama, mwanadiplomasia, Balozi Ali Karume ameendelea kusisitiza kwamba yeye ni mwanachama halali wa Chama cha Mapundizi (CCM) na hawezi kuvuliwa uanachama na “mdandia reli”.
Mwanasiasa huyo amekuwa kimya katika kipindi chote hicho tangu alipovuliwa uanachama wa CCM, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ukiukaji wa maadili na misingi ya chama kwa kumkosoa hadharani Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais Hussein Mwinyi.
Uamuzi wa kumfukuza uanachama ulitolewa Juni 8, 2023 saa 9:00 usiku na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja, chini ya Katibu wa Mkoa huo, Amina Mnacho
Hatua hiyo ilifikiwa zikiwa zimepita siku 23 tu tangu Balozi Karume alipopewa barua ya onyo Juni 15, 2023 kabla ya kuibuka tena akisisitiza kauli zake kwamba hakuna demokrasia ndani ya CCM.
Kabla ya hatua hiyo, Karume alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM tawi la Mwera, akahojiwa na kamati ya maadili ya CCM Jimbo la Tunguu na alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM Wilaya ya Kati na kupewa barua ya onyo, akiwekwa chini ya uangalizi wa miezi mitatu.
Mwananchi limefanya mahojiano maalumu na Balozi Karume nyumbani kwake Maisara na amezungumzia mambo mbalimbali, ikiwemo hatima ya uanachama wake wa CCM, Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) na ushauri wake kwa Rais Mwinyi.
Akizungumzia uanachama wake, Balozi Karume anasema yeye ni mwanachama halali wa CCM na hakuna mtu wa kumfukuza katika chama hicho kwa sababu yeye ni miongoni mwa waasisi wake.
Anasema aliwaeleza kuwa utaratibu uliotumika kumfukuza kwenye chama hautambuliki.
“Mtu anafukuzwa kwenye chama kwa kuandikiwa barua na kuambiwa ‘rejesha kadi yetu’, lakini siyo kutangaza kwenye vyombo vya habari. Mimi sijawahi kupata barua na kadi yangu ninayo,” anasema Balozi Karume.
Anasisitiza kwamba: “Mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi, siwezi kufukuzwa kwa utaratibu huo.”
Mwanadiplomasia huyo anasema chama hicho kina wanachama wa aina mbili, wanachama waasisi na wadandia reli, hivyo yeye kama mwasisi, hawezi kufukuzwa na mdandia reli.
“Mdandia reli hawezi kunifukuza kwenye chama kwa sababu mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi.
“Wakati tunaunda chama hiki kutoka Afro Shiraz (ASP) kwenda CCM, wanaotaka kunifukuza walikuwa na umri wa miaka 10 na mwezi mmoja, sasa atakuja vipi kunifukuza chama?” anahoji Balozi Karume.
Chanzo: Mwananchi
Pia soma
Mwanasiasa huyo amekuwa kimya katika kipindi chote hicho tangu alipovuliwa uanachama wa CCM, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ukiukaji wa maadili na misingi ya chama kwa kumkosoa hadharani Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais Hussein Mwinyi.
Uamuzi wa kumfukuza uanachama ulitolewa Juni 8, 2023 saa 9:00 usiku na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja, chini ya Katibu wa Mkoa huo, Amina Mnacho
Hatua hiyo ilifikiwa zikiwa zimepita siku 23 tu tangu Balozi Karume alipopewa barua ya onyo Juni 15, 2023 kabla ya kuibuka tena akisisitiza kauli zake kwamba hakuna demokrasia ndani ya CCM.
Kabla ya hatua hiyo, Karume alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM tawi la Mwera, akahojiwa na kamati ya maadili ya CCM Jimbo la Tunguu na alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM Wilaya ya Kati na kupewa barua ya onyo, akiwekwa chini ya uangalizi wa miezi mitatu.
Mwananchi limefanya mahojiano maalumu na Balozi Karume nyumbani kwake Maisara na amezungumzia mambo mbalimbali, ikiwemo hatima ya uanachama wake wa CCM, Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) na ushauri wake kwa Rais Mwinyi.
Akizungumzia uanachama wake, Balozi Karume anasema yeye ni mwanachama halali wa CCM na hakuna mtu wa kumfukuza katika chama hicho kwa sababu yeye ni miongoni mwa waasisi wake.
Anasema aliwaeleza kuwa utaratibu uliotumika kumfukuza kwenye chama hautambuliki.
“Mtu anafukuzwa kwenye chama kwa kuandikiwa barua na kuambiwa ‘rejesha kadi yetu’, lakini siyo kutangaza kwenye vyombo vya habari. Mimi sijawahi kupata barua na kadi yangu ninayo,” anasema Balozi Karume.
Anasisitiza kwamba: “Mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi, siwezi kufukuzwa kwa utaratibu huo.”
Mwanadiplomasia huyo anasema chama hicho kina wanachama wa aina mbili, wanachama waasisi na wadandia reli, hivyo yeye kama mwasisi, hawezi kufukuzwa na mdandia reli.
“Mdandia reli hawezi kunifukuza kwenye chama kwa sababu mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi.
“Wakati tunaunda chama hiki kutoka Afro Shiraz (ASP) kwenda CCM, wanaotaka kunifukuza walikuwa na umri wa miaka 10 na mwezi mmoja, sasa atakuja vipi kunifukuza chama?” anahoji Balozi Karume.
Chanzo: Mwananchi
Pia soma