Balozi Ali Karume: Siwezi kuvuliwa uanachama CCM na mdandia reli

Balozi Ali Karume: Siwezi kuvuliwa uanachama CCM na mdandia reli

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Miezi 14 baada ya kuvuliwa uanachama, mwanadiplomasia, Balozi Ali Karume ameendelea kusisitiza kwamba yeye ni mwanachama halali wa Chama cha Mapundizi (CCM) na hawezi kuvuliwa uanachama na “mdandia reli”.

Mwanasiasa huyo amekuwa kimya katika kipindi chote hicho tangu alipovuliwa uanachama wa CCM, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ukiukaji wa maadili na misingi ya chama kwa kumkosoa hadharani Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais Hussein Mwinyi.

Uamuzi wa kumfukuza uanachama ulitolewa Juni 8, 2023 saa 9:00 usiku na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja, chini ya Katibu wa Mkoa huo, Amina Mnacho

Hatua hiyo ilifikiwa zikiwa zimepita siku 23 tu tangu Balozi Karume alipopewa barua ya onyo Juni 15, 2023 kabla ya kuibuka tena akisisitiza kauli zake kwamba hakuna demokrasia ndani ya CCM.

Kabla ya hatua hiyo, Karume alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM tawi la Mwera, akahojiwa na kamati ya maadili ya CCM Jimbo la Tunguu na alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM Wilaya ya Kati na kupewa barua ya onyo, akiwekwa chini ya uangalizi wa miezi mitatu.

Mwananchi limefanya mahojiano maalumu na Balozi Karume nyumbani kwake Maisara na amezungumzia mambo mbalimbali, ikiwemo hatima ya uanachama wake wa CCM, Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) na ushauri wake kwa Rais Mwinyi.

Akizungumzia uanachama wake, Balozi Karume anasema yeye ni mwanachama halali wa CCM na hakuna mtu wa kumfukuza katika chama hicho kwa sababu yeye ni miongoni mwa waasisi wake.

Anasema aliwaeleza kuwa utaratibu uliotumika kumfukuza kwenye chama hautambuliki.

“Mtu anafukuzwa kwenye chama kwa kuandikiwa barua na kuambiwa ‘rejesha kadi yetu’, lakini siyo kutangaza kwenye vyombo vya habari. Mimi sijawahi kupata barua na kadi yangu ninayo,” anasema Balozi Karume.

Anasisitiza kwamba: “Mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi, siwezi kufukuzwa kwa utaratibu huo.”

Mwanadiplomasia huyo anasema chama hicho kina wanachama wa aina mbili, wanachama waasisi na wadandia reli, hivyo yeye kama mwasisi, hawezi kufukuzwa na mdandia reli.

“Mdandia reli hawezi kunifukuza kwenye chama kwa sababu mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi.

“Wakati tunaunda chama hiki kutoka Afro Shiraz (ASP) kwenda CCM, wanaotaka kunifukuza walikuwa na umri wa miaka 10 na mwezi mmoja, sasa atakuja vipi kunifukuza chama?” anahoji Balozi Karume.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma
 
Miezi 14 baada ya kuvuliwa uanachama, mwanadiplomasia, Balozi Ali Karume ameendelea kusisitiza kwamba yeye ni mwanachama halali wa Chama cha Mapundizi (CCM) na hawezi kuvuliwa uanachama na “mdandia reli”.

Mwanasiasa huyo amekuwa kimya katika kipindi chote hicho tangu alipovuliwa uanachama wa CCM, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ukiukaji wa maadili na misingi ya chama kwa kumkosoa hadharani Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais Hussein Mwinyi.

Uamuzi wa kumfukuza uanachama ulitolewa Juni 8, 2023 saa 9:00 usiku na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja, chini ya Katibu wa Mkoa huo, Amina Mnacho

Hatua hiyo ilifikiwa zikiwa zimepita siku 23 tu tangu Balozi Karume alipopewa barua ya onyo Juni 15, 2023 kabla ya kuibuka tena akisisitiza kauli zake kwamba hakuna demokrasia ndani ya CCM.

Kabla ya hatua hiyo, Karume alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM tawi la Mwera, akahojiwa na kamati ya maadili ya CCM Jimbo la Tunguu na alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM Wilaya ya Kati na kupewa barua ya onyo, akiwekwa chini ya uangalizi wa miezi mitatu.

Mwananchi limefanya mahojiano maalumu na Balozi Karume nyumbani kwake Maisara na amezungumzia mambo mbalimbali, ikiwemo hatima ya uanachama wake wa CCM, Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) na ushauri wake kwa Rais Mwinyi.

Akizungumzia uanachama wake, Balozi Karume anasema yeye ni mwanachama halali wa CCM na hakuna mtu wa kumfukuza katika chama hicho kwa sababu yeye ni miongoni mwa waasisi wake.

Anasema aliwaeleza kuwa utaratibu uliotumika kumfukuza kwenye chama hautambuliki.

“Mtu anafukuzwa kwenye chama kwa kuandikiwa barua na kuambiwa ‘rejesha kadi yetu’, lakini siyo kutangaza kwenye vyombo vya habari. Mimi sijawahi kupata barua na kadi yangu ninayo,” anasema Balozi Karume.

Anasisitiza kwamba: “Mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi, siwezi kufukuzwa kwa utaratibu huo.”

Mwanadiplomasia huyo anasema chama hicho kina wanachama wa aina mbili, wanachama waasisi na wadandia reli, hivyo yeye kama mwasisi, hawezi kufukuzwa na mdandia reli.

“Mdandia reli hawezi kunifukuza kwenye chama kwa sababu mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi.

“Wakati tunaunda chama hiki kutoka Afro Shiraz (ASP) kwenda CCM, wanaotaka kunifukuza walikuwa na umri wa miaka 10 na mwezi mmoja, sasa atakuja vipi kunifukuza chama?” anahoji Balozi Karume.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma
Kwani hawezi kuishi bila ya kuwa Mwanachama wa chama Cha Siasa? Mbona maisha yapo tu kwa Watu ambao hawapo kwenye hivyo vyama vya Siasa, kwa nini yeye anang'ang'ania kwamba lazima awe mwanachama wa CCM???

Kwa taarifa yake, hata Mwl. Nyerere mwenyewe ambaye ni Mwanzilishi au muasisi wa hiyo CCM alishawahi kutamka kwamba "CCM siyo mama yangu na wala siyo baba yangu."
 
Miezi 14 baada ya kuvuliwa uanachama, mwanadiplomasia, Balozi Ali Karume ameendelea kusisitiza kwamba yeye ni mwanachama halali wa Chama cha Mapundizi (CCM) na hawezi kuvuliwa uanachama na “mdandia reli”.

Akizungumzia uanachama wake, Balozi Karume anasema yeye ni mwanachama halali wa CCM na hakuna mtu wa kumfukuza katika chama hicho kwa sababu yeye ni miongoni mwa waasisi wake.
Anasisitiza kwamba: “Mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi, siwezi kufukuzwa kwa utaratibu huo.”

Mwanadiplomasia huyo anasema chama hicho kina wanachama wa aina mbili, wanachama waasisi na wadandia reli, hivyo yeye kama mwasisi, hawezi kufukuzwa na mdandia reli.

Chanzo: Mwananchi
Pia soma
Balozi Karume anajifurahisha tuu, CCM haina uanachama wa aina mbili, wala mtu kuwa muasisi wa CCM sio kinga ya kutokufukuzwa CCM unapo kiuka maadili.

Alifukuzwa muasisi wa ASP, muasisi na mshiriki wa yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya 1964 na mjumbe wa Baraza la Mapinduzi, Hassan Nassor Moyo, itakuwa yeye wakati wa Mapinduzi ya Zanzibar akikuwa kinda, na Baba yake Mzee Abedi aliyatoroka Mapinduzi yeye na wanaye Amani na Ali.

Mtu yeyote awaye yote anaweza kufukuzwa CCM!.
P
 
Uamuzi wa kumfukuza uanachama ulitolewa Juni 8, 2023 saa 9:00 usiku na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja, chini ya Katibu wa Mkoa huo, Amina Mnacho

Hatua hiyo ilifikiwa zikiwa zimepita siku 23 tu tangu Balozi Karume alipopewa barua ya onyo Juni 15, 2023 kabla ya kuibuka tena akisisitiza kauli zake kwamba hakuna demokrasia ndani ya CCM.
Mwenyekiti Mzanzibari, Makamu Mzanzibari aliyefukuzwa Mzanzibari
Nje ya Muungano wazanzibari watakuwa wamoja?
 
Miezi 14 baada ya kuvuliwa uanachama, mwanadiplomasia, Balozi Ali Karume ameendelea kusisitiza kwamba yeye ni mwanachama halali wa Chama cha Mapundizi (CCM) na hawezi kuvuliwa uanachama na “mdandia reli”.

Mwanasiasa huyo amekuwa kimya katika kipindi chote hicho tangu alipovuliwa uanachama wa CCM, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ukiukaji wa maadili na misingi ya chama kwa kumkosoa hadharani Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais Hussein Mwinyi.

Uamuzi wa kumfukuza uanachama ulitolewa Juni 8, 2023 saa 9:00 usiku na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja, chini ya Katibu wa Mkoa huo, Amina Mnacho

Hatua hiyo ilifikiwa zikiwa zimepita siku 23 tu tangu Balozi Karume alipopewa barua ya onyo Juni 15, 2023 kabla ya kuibuka tena akisisitiza kauli zake kwamba hakuna demokrasia ndani ya CCM.

Kabla ya hatua hiyo, Karume alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM tawi la Mwera, akahojiwa na kamati ya maadili ya CCM Jimbo la Tunguu na alihojiwa na kamati ya maadili ya CCM Wilaya ya Kati na kupewa barua ya onyo, akiwekwa chini ya uangalizi wa miezi mitatu.

Mwananchi limefanya mahojiano maalumu na Balozi Karume nyumbani kwake Maisara na amezungumzia mambo mbalimbali, ikiwemo hatima ya uanachama wake wa CCM, Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) na ushauri wake kwa Rais Mwinyi.

Akizungumzia uanachama wake, Balozi Karume anasema yeye ni mwanachama halali wa CCM na hakuna mtu wa kumfukuza katika chama hicho kwa sababu yeye ni miongoni mwa waasisi wake.

Anasema aliwaeleza kuwa utaratibu uliotumika kumfukuza kwenye chama hautambuliki.

“Mtu anafukuzwa kwenye chama kwa kuandikiwa barua na kuambiwa ‘rejesha kadi yetu’, lakini siyo kutangaza kwenye vyombo vya habari. Mimi sijawahi kupata barua na kadi yangu ninayo,” anasema Balozi Karume.

Anasisitiza kwamba: “Mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi, siwezi kufukuzwa kwa utaratibu huo.”

Mwanadiplomasia huyo anasema chama hicho kina wanachama wa aina mbili, wanachama waasisi na wadandia reli, hivyo yeye kama mwasisi, hawezi kufukuzwa na mdandia reli.

“Mdandia reli hawezi kunifukuza kwenye chama kwa sababu mimi ni mwasisi wa Chama cha Mapinduzi.

“Wakati tunaunda chama hiki kutoka Afro Shiraz (ASP) kwenda CCM, wanaotaka kunifukuza walikuwa na umri wa miaka 10 na mwezi mmoja, sasa atakuja vipi kunifukuza chama?” anahoji Balozi Karume.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma
sijui nini kinaendelea, ila hii ndio huwa mentality ya waafrika na ndio maana viongozi wengi wanaodaiwa kuwa walipigania uhuru kamwe hawakutaka kuondoka madarakani wakiona kuwa kwa kuwa walipigania uhuru nchi ni za kwao na hakuna mtu tofauti na cycle yao anapaswa kuwaongoza au kuwambia nini cha kufanya.
Huenda ameonewa ila kauli yake ya kwamba yeye ni muasisi na hao waliomfukuza walikuwa na miaka kumi hivyo hawawezi kumwondoa inazungumza mentality ya viongozi wengi wa afrika
 
Kwani hawezi kuishi bila ya kuwa Mwanachama wa chama Cha Siasa? Mbona maisha yapo tu kwa Watu ambao hawapo kwenye hivyo vyama vya Siasa, kwa nini yeye anang'ang'ania kwamba lazima awe mwanachama wa CCM???

Kwa taarifa yake, hata Mwl. Nyerere mwenyewe ambaye ni Mwanzilishi au muasisi wa hiyo CCM alishawahi kutamka kwamba "CCM siyo mama yangu na wala siyo baba yangu."
Nyerere hakuwa mwanzilishi wa chama chochote,alidandia vyama vya watu
 
Balozi Karume anajifurahisha tuu, CCM haina uanachama wa aina mbili, wala mtu kuwa muasisi wa CCM sio kinga ya kutokufukuzwa CCM unapo kiuka maadili.

Alifukuzwa muasisi wa ASP, muasisi na mshiriki wa yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya 1964 na mjumbe wa Baraza la Mapinduzi, Hassan Nassor Moyo, itakuwa yeye wakati wa Mapinduzi ya Zanzibar
Balozi Karume anajifurahisha tuu, CCM haina uanachama wa aina mbili, wala mtu kuwa muasisi wa CCM sio kinga ya kutokufukuzwa CCM unapo kiuka maadili.

Alifukuzwa muasisi wa ASP, muasisi na mshiriki wa yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya 1964 na mjumbe wa Baraza la Mapinduzi, Hassan Nassor Moyo, itakuwa yeye wakati wa Mapinduzi ya Zanzibar akikuwa kinda, na Baba yake Mzee Abedi aliyatoroka Mapinduzi yeye na wanaye Amani na Ali.

Mtu yeyote awaye yote anaweza kufukuzwa CCM!.
P
Nape: CCM Ina wenyewe.

Sasa huelewi nn P!
 
Back
Top Bottom