TANZIA Balozi Emanuel Ole Naiko afariki Dunia Dar

TANZIA Balozi Emanuel Ole Naiko afariki Dunia Dar

Adaption ya makabila ya watu kwa interest binafsi i.e kisiasa nk
 
RIP Olenaiko, Pole kwa familia na wadau, Mzee huyu alifaidi Sana maisha. Miaka ya 80.... Alikuwa meneja mgodi wa dhahabu wa serikali Backreef ... TIC....Balozi....
 
R.I.P hivi natakiwa nifute namba ya simu za Marehemu...
 
View attachment 2169523
Familia ya Emmanuel Ole Naiko inasikitika kutangaza kifo cha BABA YAO, BALOZI EMMANUEL OLE NAIKO kilichotokea leo 30/03/22, nyumbani kwake Bahari Beach, Dar es Salaam.

Habari ziwafikie wana familia waliopo Dar es Salaam, Monduli-Arusha na kwengine kote.

Balozi Ole-Naiko amewahi kushika nyadhifa mbali mbali kwenye serikali ikiwemo Mkurugenzi mkuu wa kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

Wakati wa mauti unamfika alikuwa ni balozi wa Heshima wa Botswana.

Mipango ya mazishi inaendelea nyumbani kwake Utulivu Road, Bahari Beach, Dar es salaam

Balozi Naiko alizaliwa tarehe 24 Julai 1951.

Bwana ametoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe

2 Timotheo 4; 7
Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda
Kama hii ni kweli Ole Naiko R.I.P👉
"Nimevipiga
vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda."

Kama sio kweli Mungu mwenyewe aamue pa kukuweka.
 
View attachment 2169523
Familia ya Emmanuel Ole Naiko inasikitika kutangaza kifo cha BABA YAO, BALOZI EMMANUEL OLE NAIKO kilichotokea leo 30/03/22, nyumbani kwake Bahari Beach, Dar es Salaam.

Habari ziwafikie wana familia waliopo Dar es Salaam, Monduli-Arusha na kwengine kote.

Balozi Ole-Naiko amewahi kushika nyadhifa mbali mbali kwenye serikali ikiwemo Mkurugenzi mkuu wa kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

Wakati wa mauti unamfika alikuwa ni balozi wa Heshima wa Botswana.

Mipango ya mazishi inaendelea nyumbani kwake Utulivu Road, Bahari Beach, Dar es salaam

Balozi Naiko alizaliwa tarehe 24 Julai 1951.

Bwana ametoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe

2 Timotheo 4; 7
Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda
Kuna wakati nilifikiria TIC ni kampuni yake binafsi.
 
Kuna mmeru anajina la Ole?
Kule kenya alikuwepo mwamba ammoja Mkikuyu lakini akajipachika jina Saitoti jina la kimasai wakati ni Mkikuyu, wengi walibadili majina kwa kujipa majina ya kimasai sababu ya kupata fursa za kusoma miaka ya nyuma wakati Wamasai walikuwa wanabembelezwa kwenda shule na hata ukiwa Mmasai maksi za kufaulu zilikuwa zipo chini kulinganisha na makabila mengine,na hata misaada mingi miaka hiyo walipewa Wamasai,kwa hiyo usishanga e Mmeru kujiita mmasai. Kama umezaliwa kile kipindi cha TANU yajenga nchi nadhani usingeuliza hili swali nina wasiwasi umezaliwa labda kipindi Mzee Mrema alipokuwa waziri wa mambo ya ndani na naibu waziri mkuu enzi zile akitoa siku 7 ufike ofisini kwake na lambo la wekundu wa Msimbazi
 
Back
Top Bottom