Ahaa ! Kumchamba mtu ni pale wanawake hasa wa pwani kuenda kumsema mwenzao ambaye ni muongo au mfitini ili akome! Tendo hili hufanywa mbele ya halaiki au kadamnasi ya watu. Wakati mwingine wachambaji hupendelea kuvaa nguo aina ya dira sare sare na kibwebwe kiunoni ili kukoleza mambo ! Mchambwaji Hua hapewi hata nafasi ya kujitetea na anaweza kusingwa vile vile. Inasemekana kabila la wazaramo ndio wataalam wa kuchamba maana huweza kumchamba mwenzao mpaka akazimia bila hata kuguswa! π Nadhani nimefafanua vya kutosha.π