Nyani Ngabu, Ni mawazo yako yaliyopitwa na wakati
Unafikiri ule ubalozi wa Marekani Tanzania ulijengwa na pesa za Babu yako?
Kama Balozi hatambuliki zile chanjo za korona zilitolewa kwa msaada zilitoka Marekani au kwenye Familia yako hapo Mbezi ya Tangi bovu
Unafahamu maana ya Balozi, Balozi ni muwakilishi wa Rais Katika nchi husika
Huyo Balozi ndiye muwakilishi wa Biden hapa Tanzania, Raia wa Marekani kufahamu au kutokufahamu inategemea kama wana lengo la kuja Tanzania au kuna tukio kubwa sana Tanzania
Obama alivyofika Tanzania, alifikia nyumbani kwenu hapo Tangi bovu au alielekea kwenye ubalozi wake kwanza
Kuna watu wazima humu jamii forum lakini wana mawazo ya kipuuzi na kipumbavu sana
Mimi mtanzania sina lengo la kwenda Iraq, Syria, Somalia, Au Cambodia,. Nianze kuulizia mabalozi wa huko kwa faida gani?
Balozi ana kazi zake maalum na hapo kwenda jamii forum ana mambo anayotaka kujifunza na kuyaona ili ajiongezee maarifa na uzoefu Katika maisha yake
Wewe Nyani ngabu una mfahamu Balozi wa Tanzania huko uzebakstan? au nchi ya Tajikstan?
Sasa Mimi nimeishia huko uzebakstan na Balozi anayesimamia huko namfahamu vizuri toka Tanzania, Watu ambao hawana mpango wa kwenda huko uzebakstan wamtafute Balozi wa kazi gani?