BANDAMA: Je ni kweli ukitolewa organ hii mtu unashindwa kucheka?

I am Groot

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
3,929
Reaction score
10,747
Nimekuwa nikisikia kuwa mtu akifanyiwa upasuaji na kuondolewa bandama mtu anakuwa hawezi kucheka.

Je ni kweli huwa hivyo? Na nini kinasababisha kuwa hivyo?.

Wataalamu; naombeni mnielimishe juu ya jambo hili.
 
Niliwahi kusoma na Dada mmoja alikuwa na Matatizo kwenye mbavu yeye alikuwa hatakiwi kucheka muda mwingi alikuwa akikaa pekee yake.

Sijajua kuhusu Bandama.
 
Bandama ni spleen,,na kazi yake physiologically haiusiani na kucheka
 
Kazi yake ni kuchuja damu na kuondoa seli nyekundu za damu zilizokufa,na pia zina chembe hai nyeupe za damu ambazo ni walinzi wa mwili..
Nimeelewa sasa. Asante sana.

je, unaufahamu ni nini ambacho kikiondolewa mwilini mtu hushindwa kucheka?. Sababu kwa maelezo yako inaonyesha kuwa Bandama haihusiani na jambo hilo.
 
Nimeelewa sasa. Asante sana.

je, unaufahamu ni nini ambacho kikiondolewa mwilini mtu hushindwa kucheka?. Sababu kwa maelezo yako inaonyesha kuwa Bandama haihusiani na jambo hilo.
Kucheka kunatofautiana,,ila ile ya kujionyesha kabisa kuwa umecheka navyoona misuli ya koo(throat muscles) ikiondolewa mtu hataweza kucheka,pia jaw(taya)
 
bandama spleen ndo kiungo ambacho kiki tolewa kwenye mwl wa binadamu hakina madhara. Mara nying bandama hutumika kwenye kuvunja cell nyekundu za damu zilizo zeeka au kuwa na abnormality kama sickle cell, . Hakuna ushaidi wa moja kwa moja kuwa spleen iki tolewa mtu ata shindwa cheka.
 
Nimeelewa sasa. Asante sana.

je, unaufahamu ni nini ambacho kikiondolewa mwilini mtu hushindwa kucheka?. Sababu kwa maelezo yako inaonyesha kuwa Bandama haihusiani na jambo hilo.
We jamaa shida yako hutaki watu wacheke,maana ulivong'ang'ania watu wasicheke
 
Kazi yake ni kuchuja damu na kuondoa seli nyekundu za damu zilizokufa,na pia zina chembe hai nyeupe za damu ambazo ni walinzi wa mwili..
Du sasa kama hii ndiyo kazi ya bandama vipi likitolewa huyo MTU anaweza kuishi kwa muda mrefu kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…