chiembe
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 16,859
- 28,112
Nimemuona Rais Mwinyi akiwa Uchina akipigia debe, pamoja na mambo mengine, Bandari ya Mangapwani. Katika hotuba zake kadhaa, Rais Mwinyi ameonyesha nia ya dhati kuifanya bandari hiyo iwe kubwa kabisa Afrika Mashariki.
Upande wa pili, inaelezwa kwamba bandari ya Bagamoyo ikikamilika, itakuwa na uwezo wa kubeba kontena sawa na bandari zote kusini mwa jangwa la sahara. Inakadiriwa kuwa na uwezo wa kontena milioni ishirini.
Kama nchi, wapi panalipa? Bandari ya Bagamoyo inajiunga moja kwa moja na nchi kavu. Mangapwani? Itabidi uchukue kontena halafu ulibebe tena kulileta bara?
Wajuvi, mna maoni gani? Kqa nini tuliipiga vita bandari ya Bagamoyo enzi za jiwe, baadae tukamuona jiwe anajenga bandari ya nyamirembe huko chato, bandari ambayo sidhani ilishawahi kupokea hata meli moja, achilia mbali mtumbwi!
Upande wa pili, inaelezwa kwamba bandari ya Bagamoyo ikikamilika, itakuwa na uwezo wa kubeba kontena sawa na bandari zote kusini mwa jangwa la sahara. Inakadiriwa kuwa na uwezo wa kontena milioni ishirini.
Kama nchi, wapi panalipa? Bandari ya Bagamoyo inajiunga moja kwa moja na nchi kavu. Mangapwani? Itabidi uchukue kontena halafu ulibebe tena kulileta bara?
Wajuvi, mna maoni gani? Kqa nini tuliipiga vita bandari ya Bagamoyo enzi za jiwe, baadae tukamuona jiwe anajenga bandari ya nyamirembe huko chato, bandari ambayo sidhani ilishawahi kupokea hata meli moja, achilia mbali mtumbwi!