Serikali inapaswa kujua nini kinachotakiwa kufanyika ili kuongeza ufanisi wa mashirika yetu ya umma kama TANESCO, TTCL, ATCL, TRC, TPA, n.k. Ukichunguza sana utagundua kwa mashirika haya ambayo tayari tulishawekeza kama taifa kwenye miundombinu ya msingi hatuhitaji WAWEKEZAJI bali WAENDESHAJI. Kwa mfano hatuhitaji mwekezaji ATCL, TRC, BANDARI, au TANESCO, tunahitaji waendeshaji kwani hata sasa bado tunawekeza matrilioni kwenye mashirika haya ila ufanishi hakuna kwasababu ya uendeshaji mbovu.
Kwa ujumla hoja ya kushirikiana na wataalam kuendeleza bandari yetu sio mbaya, ubaya ni vipengele visivyokuwa na ufafanuzi wa kutosha kwa mfano katika mkataba wa bandari na DP World, ilipaswa kuweka wazi kwamba DP wanakuja kuendesha bandari na sio kuwekeza. Huu mkataba ni wa jumla jumla (vague) na hauna maelezo ya kina mfano ukomo wa muda na wigo. Siku zote ni hatari kuwa na mkataba usiokuwa bayana. Hili limenitia wasiwasi mkubwa kuhusu weledi na uzalendo wa viongozi wetu.
Ukweli ni kwamba bila kutafuta washirika wanatakaotusaidia KUENDESHA mashirika yetu ya umma, basi tutegemee hasara tu. Tukubali kuwa weledi wa uendeshaji wa mashirika makubwa hatuna na tunahitaji watu wa kushirikiano nao kwenye undeshaji. Sio lazima kufanya UBINAFSISHAJI, tunaweza kuruhusu wajuzi wakatusaidia kuendesha baadhi ya vitengo au hata shirika zima kwa ufanisi zaidi.
Ni suala la muda tu ila hayo mashirika niliyoyataja hapo juu yatatutia hasara kubwa kabla ya hayajafa! Serikali tafuteni management teams kutoka mataifa yenye uwezo mkubwa tuingie mikataba inayoeleweka ya KUENDESHA mashirika yetu kwa manufaa ya umma.
Kwa ujumla hoja ya kushirikiana na wataalam kuendeleza bandari yetu sio mbaya, ubaya ni vipengele visivyokuwa na ufafanuzi wa kutosha kwa mfano katika mkataba wa bandari na DP World, ilipaswa kuweka wazi kwamba DP wanakuja kuendesha bandari na sio kuwekeza. Huu mkataba ni wa jumla jumla (vague) na hauna maelezo ya kina mfano ukomo wa muda na wigo. Siku zote ni hatari kuwa na mkataba usiokuwa bayana. Hili limenitia wasiwasi mkubwa kuhusu weledi na uzalendo wa viongozi wetu.
Ukweli ni kwamba bila kutafuta washirika wanatakaotusaidia KUENDESHA mashirika yetu ya umma, basi tutegemee hasara tu. Tukubali kuwa weledi wa uendeshaji wa mashirika makubwa hatuna na tunahitaji watu wa kushirikiano nao kwenye undeshaji. Sio lazima kufanya UBINAFSISHAJI, tunaweza kuruhusu wajuzi wakatusaidia kuendesha baadhi ya vitengo au hata shirika zima kwa ufanisi zaidi.
Ni suala la muda tu ila hayo mashirika niliyoyataja hapo juu yatatutia hasara kubwa kabla ya hayajafa! Serikali tafuteni management teams kutoka mataifa yenye uwezo mkubwa tuingie mikataba inayoeleweka ya KUENDESHA mashirika yetu kwa manufaa ya umma.