Josephat Mgimwa
Member
- Apr 8, 2014
- 60
- 18
Bango hilo lilikuwa na ujumbe uliokuwa ukilinganisha posho ya mjumbe mmoja wa bunge la katiba na mshahara wa mwalimu kwa mwezi. Bango hilo limezua mvutano kati ya walimu vijana na mwenyekiti wa chama mkoa wa Kagera kitendo kilichopelekea polisi kuingilia kati na kuzuia kuingia kwa bango hilo ndani ya uwanja wa Kaitaba ambapo maadhimisho ya siku ya Mwalimu duniani inaadhimishwa kitaifa mkoani Kagera huku mgeni rasmi akiwa ni Mizengo Pinda ambaye amekuja ghafla hku mgeni rasmi katika taarifa alikuwa ni Jakaya Mrisho Kikwete rais wa Tanzania.