Benki zote ni hovyo kabisa ila sasa kwenye huo uhovyo kuna wenye uhovyo afadhari na uhovyo sana. Cha msingi benki bomu kuliko zote ni NMB, ila kama maisha yako yatakuwa ni ya vijijini huna ujanja maana ndio benki pekee inayopatikana mpaka vijijini. Benki inayofuatia kwa uhovyo ni NBC, hawana tofauti kubwa na NMB, foleni ni ndefu mno, kama una muda wa kuchezea wa kukaa benki masaa manne mpaka nane unaweza ukaopt hizo benki mbili. Benki zingine customer care yao ni hovyo sana kama vile wamelazimishwa kufanya kazi. Ila kwa benki ambayo ni hovyo afadhari ni CRDB, wanajitahidi kuendana na wingi wa wateja wao maana wana mabranch mengi, so ukiona branch moja mizingua unaweza enda branch nyingine, ila km kuna tatizo lolote utakalopata linalohusiana na Card yako, inabidi usubiri mwezi kuweza kurekebishiwa tatizo.
Barclays ni benki hovyo sana japo pia inajitahidi kuwa na branch nyingi, unaweza ingia bank mkawa watu 6 tu ila utasubiri hapo masaa mawili, huku wakitoa majibu mepesi tu kuwa system ipo slow au down, watu hawajitumi kabisa, unaweza ukakuta foleni ndefu halafu bank teller mmoja, wengine wanapiga story tu. Kadi zao hazina picha, so ili ufanye transaction ni lazima uwe na kitambulisho kingine, pia wizi mkubwa waliofanya wafanyakazi wao wakati wanatoa mikopo kiholela umesababisha wawe na kero nyingi zaidi kwa wateja wao.
Benki zingine zote ni matatizo tu, zina branch chache sana hapa nchini. Kwa ujumla ukiamua kuweka hela zako bank inabidi uwe na moyo wa uvumilivu.