Banki sio rafiki kwa Mfanyakazi/mtu wa kipato Kidogo

Mhh Kwa miaka 20 kiwango mbona kidogo sana.
Tuchukue update hizo milion 40 uwekeze mfano kwenye biashara ya utengenezaji wa unga wa sembe.
Kukodi jengo 300000*12'=3600000
Mashine ununuzi =8000000
Kuingiza umeme=2000000
Mifuko grade1 ya kuanzia(2000)=1000000
Mpaka hapo jumla=14600000
Unabaki na 25400000
Toa 25000000 kipind cha mavuno nunua Mahindra utapata kg 40000
TUJE KWENYE UZALISHAJI
Ukijiwekea target kila siku usage tani kumi Kwa wastan wa faida ya 300000 Kwa tani kumi. Hapa bila pumba.
Ukifanya Kwa siku 20 Kwa mwezi,
20*300000= utaingiza 6000000 Kwa mwezi.
Kwa mwaka 12*6000000=720000000
Kwa miaka 20*72000000=1.44bil
1.44bil-147mil=?

TUJE KWENYE DECISIONS
Kwa maono yangu tatizo sio benki Bali maono ya mtu na exposure.
Nipe Mimi hizo nikupe 200mil Kwa miaka miwili Ila au nipe machinery za that amount hiyo nichague eneo la kufanyiwa biashara nikupe mara kumi ya capital yako ndani ya mwaka.
 
Ni kweli mikopo ya bank sio poa,
Ila naomba nikurekebishe hapo kwenye riba, hiyo riba ya 18% itakuwa calculated kwa deni litakalobaki kwa kila mwaka na sio kwa hell uliyokopa.
Mfano ukikopa 40m riba ya 1st year 7.2m
Then 2nd year deni Ni 32.6 riba 5.86m

So trend inaenda namna hiyo so sidhani Kama itafika 144m
 
Mikopo haina tatizo bali tatizo linaweza kuwa kwa mkopaji.
Ukikopa halafu usiwe na mkakati uliosimama vema wa namna ya kupata rejesho kwa wakati na mkopo ukaanza kugeuka kuwa deni hapo ndo shida inapoanzia.
Nini kinatakiwa kufanyika kabla ya kukopa? Kwanza kabisa ni uwe tayari kuingia chimbo kupata ufahamu sahihi wa namna ya kuuhudumia mkopo. Usikubali kukopa kichwa kichwa bila kujua chanzo kipi kitakuwa kinakupatia pesa ya rejesho.
Mbinu ambayo haitakuweka katika wakati mgumu ni wewe kutafuta watu watakaohusika na kulipa rejesho kwa kiasi fulani na wewe kulipa kiasi fulani,lakini kama unatarajia Utalipa mwenyewe mwanzo mwisho mkopo utakutafuna sana. Hiyo ndo mbinu ninayoifahamu ambayo inasaidia namna Bora ya kupata rejesho bila kukuweka mtu kati. Unawapataje watu watakaohusika na kukulipia rejesho ? hapo ndo mkakati unatakiwa kuwepo kwanza kabla hujavuta mzigo.
Ninachoamini mkopo hauna tatizo lolote maandalizi yakifanyika vizuri kabla ya kuuchukua.
 
Biashara ya kwenye makaratasi hii ila kwenye uhalisia haiwezekani kabisa
 
Mkuu biashara haiko hivo usiweke hesabu as if utakuwa unakula wewe unga. Kuna kodi hapo kibao tu TRA, TFDA, Mazingira plus plus hali ya soko, kupanda kwa bei ya mahindi, wafanya kazi n. k hio Bil 1 ni hesabu za ndotoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…