Banki sio rafiki kwa Mfanyakazi/mtu wa kipato Kidogo

Hizi fikra hazina tofauti na ule mpango wa kilimo cha matikiti cha kupata mil.20 ndani ya msimu mmoja. Ukitoa 2 ya mtaji unabaki na 18m faida 😁😁😁
 
Nilikopaga bank 10ml aisee mpaka Leo nataabika mbaya hata mapenzi yamepungua nyumbani na wife kuishi kwa 230000 ndani ya mwezi sio mchezo aisee
Bila shaka mke anakusaidia kufanya marejesho benki, 😁😁😁 lazma anune tu, hela ya mwanamke haijawahi kumuacha kidume salama.
 
Sio simple hivo unavyodhani.
 
Hayo ni mawazo ya masikini!masikini kila tajiri ni mwizi,mchawi,mzumaji tafta benk zenye riba nafuu...ya kwanza kwa riba nafuu tz ni n.m.b matajiri wote duniani wanakopa benk yoyote ukikopa pesa ukakaa nayo mda mrefu riba ni kubwa sana kopa pesa kaa nayo mwaka mmoja au miwili tu ukizidi 3...lakini kama kweli unataka kutoboa kakope huo ndio ukweli.
 
BANK NI KUNDI LA WAHUNI LA KUWAFANYA WATU MASIKINI...NA NILIJITAHIDI KUWANASUA KWENYE HII ISHU ILA NDO HVY WENYE BANK WAKANIUA ..."JF KENEDY"
 
Tatizo mwajiri wetu nae roho mbaya, hataki kitudhamini kwenye hizi Bank ili tukope yaani yeye naweza sema anapenda kuona tukiwa watumwa wake tu

Hivi hawa NSSF huwa hawatoi mikopo?
Hili ndio tatizo jingine la private co....Matajiri kamwe hawataki kudhamini mtu Bank. Na bank wanahutaji kitu kama hiko...so watu wanabaki njia panda....
 
Bank wahuni sana, ukienda kwa shida ya mkopo wa kufungua kiwanda kupata inakuwa ngumu sana. Sema tupambane wadau, maisha ni magumu sana
 
Ndio shida ya kumix imani za kiislam na mambo ya riba.

Bank imetumwa pesa.
 
Mshukuru Mungu kuwa kakupa akili ya kupambanua mambo.
 
Weka mathematics tuone tena kwa pesa iyo unaweka na ile aliyochukua mwanzoni. Tatizo hesabu ni changamoto kwa watu wengi sana.
Kama amechukua 40 Miliioni
40M*0.18*20= 144M
144M+40=184M
Mpaka anamaliza mkopo atakuwa katoa pesa iyo ndio gharama atakiwayo kutoa pesa
184M÷12÷20=Tshs 766,666.67 kwa iyo ndio ivyo sema kama ni mtu wa maesabu inakulipa, kama ni nyumba ya bihashara kama ni Hostel nzuri inakulipa tuuu, maanna mpaka miaka iyo 20 na pango ya nyumba itakuwa ishapanda kulingana na soko la nyumba
 
Haiwezi fika 184 kwa sababu inakuwa calculated annually. Mfano
Mwaka wa kwanza utadaiwa 40+40*0.18
Next year kama balance imebaki 37 utachajiwa 37+37*0.18 na kuendelea in a downward trending manner kama mkopo wa board vile. Ndo mana inakuja kuwa kama 147m.
 
Bank wahuni sana, ukienda kwa shida ya mkopo wa kufungua kiwanda kupata inakuwa ngumu sana. Sema tupambane wadau, maisha ni magumu sana
Wanachoboa hawa jamaa ukiandika proposal imesimama na imetulia na inaonyesha kuna mpunga wa utapiga hata baada ya miezi 6 hawakupi hela kabisa. Ila ukiwa tayari ushaanza kufanyia kazi wazo lako na wanaona kuna faida ndo wanaanza kuja eti mkopo wako ulioombaga tunaweza kukupa sa ivi. Shenzi kabisa. Hapo washajua kuna ka profit mgawane.
 
Inategemea na unajenga nn? Kama ni nyumba ya bihashara inalipa lakini ni kwa ajili ya kuishi hakuna faida yoyote apo
Hata biashara hapo huwezilipa huomkopo. Milioni 40hl hata nyumba ya kupangisha 350,000 kwa mwezi haimalizi.
 
[emoji16][emoji16][emoji2][emoji2][emoji2]Kweli kabisa mkuuuu
 
Leo siku nzuri sana. Watu wanajadili maswala ya maendeleo tupu. Shule nzuri sana, umeimwaga apa. Tatizo wengi tunataka tuwekeze apo DSM kitu ambacho ni kigumu sanaaaa. Mfano mzuri DSM kuna soko kubwa la maziwa fresh ya ng'ombe lakini sehemu za kufugia hakuna, lakini ukijificha mkoa wa pwani ukafuga unapata zako faida vizuri sana
 
Huo mkopo sio wa kwenda Bank. Ndugu zako 2 tu wanaweza kupa hio na ukarudisha bila riba. Shida wengi hamuaminiki. Nilimpa jamaa bodaboda aendeshe arudishe tu nusu ya hela (mdogo wangu) hadi leo sijamsikia nimeamua kukaa kimya.
Mkuu ndugu niliyenaye ni Dada yangu wa Damu kabisa na yeye yupo serikalini hivyo kuhusu swala la kuchukua mkopo bank haina tatizo ila haniamini nahisi kama ulivyosema nilishawahi kumwambia anichukulie 3mil nitairejesha ndani ya mwaka mmoja,
Akanambia ye bado anadaiwa alikopa 8mil akanunua gari sa hv kakopa tena anajenga nyumba

Nmeamua kuachana nae napambana na hali yangu
Najua mwakani ndo mwaka wa mwisho kuajiriwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…