Banki sio rafiki kwa Mfanyakazi/mtu wa kipato Kidogo

Hapo mkuuu umedanganya, mimi nimesoma somo la Financial, hakuna kitu kama icho ulichozungumza apo
 
Kweli mkuu,kuna bi mkubwa hua anatuletea maziwa ofisini kwetu kila ijumaa na minimum order anayouza ni 5 litres/head nae anafugia huko Pwani.
 
Hata biashara hapo huwezilipa huomkopo. Milioni 40hl hata nyumba ya kupangisha 350,000 kwa mwezi haimalizi.
Unalipa vizuri tuu, mfano apa nina ndugu yangu yupo maeneno ya changanyikeni UDSM. Walijenga nyumba 2 viapartment fulani kwa gharama ya kama 36M. Mwaka 2012. Kawapangisha watu kwa gharama ya 500K@ Monthly na amesharudisha pesa yake na kodi imebadirika badirika sana tokea 2012. Sema ni bihashara za wenye fedha sio za ujasiriamali izi bihashara mkuuu
 
Mkuu biashara haiko hivo usiweke hesabu as if utakuwa unakula wewe unga. Kuna kodi hapo kibao tu TRA, TFDA, Mazingira plus plus hali ya soko, kupanda kwa bei ya mahindi, wafanya kazi n. k hio Bil 1 ni hesabu za ndotoni.
😀😀as if anakula yeye😀
 
Tatizo la Rate ya mkopo wanakuchaji kwa kuangalia mzunguko wa fedha na dhamana gani? Unayoweka mfano unaweka dhamana kumbi yako ya harusi na wanajua kila weekend, pana shughuli lazima mkopo upate kwa rate nnzuriii tuuu, ili sio Tanzania tuuu, hata ktk nchi za wazungu kupata dhamana ya mkopo ni ishu. Kama ulaya yenyewe kuwa na nyumba tuuuu ni ishu ile mmbaya
 
hiyo biashara mzuri sana, niliifanya kwa brother mwaka 2006 2007 ni mzuri mno. Changamoto kubwa niliyoiona, mashine zinasumbua sana. Mara chekeche limetoboka, Mara rola imezingua, Mara motor imeungua basi tafrani. kwa ufupi ukiwa na mashine hata kulala ulali ni mwendo wa kugongagonga tu usiku kucha. lkn mambo mengine ni ya kawaida na unaweza kupambana nayo. wastani wa Tani moja ni viroba 30 vya kg 25. Pumba gunia 4. Kwa kipindi kile tulivyokuwa tunafanya sisi Tani 11 tulikua tunapata viroba 310 vya kg 25 na tukitoa gharama za uwendeshaji tulikua tunapata laki tatu Kama faida. Na tulikua tuna saga kila baada ya Siku 3. Pia kuna changamoto ya Umeme, Umeme bei juu Sana, hiyo ndo ilikua inatuumiza kichwa hasa ukikutana na mahindi Kama ya tanga ambayo hayatoi wastani mzuri.
 
Ulaya mortgage ndio mkombozi wao.
 
Lazima kuwe na sababu ya msingi( yakibiashara) ndio ukope.

Nawaona huruma Sana watumishi wanaokopa ili wajenge.
 
Sio simple hivo unavyodhani.
Kweli sio simple kihivyo. Sitarajii ukianza hii biashara ukae ukitegemea wateja na masupplier wajilete lazima upambane, pia uchaguz wa eneo ni muhimu Sana. Chukulia mfano uende ukaanzishe eneo kama msasan au uende mbeya ukaanzishe kiwanda kama hicho utalia. Kitu chochote juhud binafs ndo zinaweza fanikisha pia uwe na malengo. Mfano kuna mwingine unakuta yeye ashajipangia kuwa Kwa kila tani kumi apate faida labda 800k haijalishi ameuuza ndani ya wiki au mwezi. Na kuna mwingine yeye amejipangia kila siku walau alale na laki baada ya mwez lazima kutakuwa na utofauti. Ishu kubwa ni malengo. Hola kubwa Tu hapa nitaonekana kama inspiration speaker maana kiukwel ndo tumezoea hivyo, hatuamini kuwa kuna maeneo ndan Tanzania's hii kuna watu wananunua vitu na kuuza na wakata faida ya mara mbili. Wengi wetu tumekaa dar na kuridhika.sio lazima dar au Tanzania jamani. Mfano kuna watu wananunua zile sabuni za kigoma Kwa 20000 kigoma wakaenda kuuza sehem Kwa 44000 jumla. Kuna watu wananunua katoni za Azam energy Kwa 10500 wakaenda uza Kwa 22000 hapo wanatoa usafiri Kwa katoni 5000.
Sio kila MTU anayeongea ni inspiration speaker
 
Kiukwel wengi wetu tumekariri biashara lazima iwe dar kitu ambacho sio. Unakuta MTU anakomaa na Duka la chakula. Mfano ananunua tomato paste Kwa 8000 akiuza rejareja packet 24 anapata faida ya 4000, mpaka amalize ishakuwa mwez au wiki. Wakati nikijisogezaa mfano Tu kigoma na milion zangu hizo za Duka la chakula nikaamua niwe nakusanya mbosa kutoka vijijin kama malagarasi na kwingineko na baadae Naja nakamulisha kupata mafuta naweza piga faida mara tatu ya Duka. Mfano kipind cha mvua mawese kigoma huwa yanafika mpaka 24000 Kwa dumu na wateja wanakosekana lakin mwanza au dar muzar oil yanakuwa yanahitajika Kwa wingi. Kukodi behewa kigoma dar haizid 1.5mil na hapo unaweza pakia dumu kama 700 lakin unakuta MTU kakomaaa dar Tu miaka.
Kwangu Mimi dar sio sehem sahihi ya kutafutia Bali sehem ya kuja tembea tu
 
Mhh komaaaa ndugu hakuna atayekuamini. Mimi niliwahi Fanya kazi na mzaz wangu kila nilipotaka kutoka nianzishe yangu anagoma. Nikalazimisha toka sikuwa na hata senti nilipomuomba hata 1.5mil anikope nisonge akanichinjia baharini. Bahat Tu nikasukuma kiwanja nikaanza yangu alipoona Niko mbali akataka ushirikina nikamchinjia baharini
 
Mbona maeneo kama haya siwaonagi hawa watu,magonjwa mtambuka,Yehodaya,cocochannel inamaa wenzetu ubongo wao upo kwa ajiri ya kusifia tu???
 
Tatizo sio bank ila ni uwezo wako wa kufikiri na kuogopa ku take risk. Nipe mimi hizo milioni 40 ntakurudishia milioni 50 ndani ya mwaka na nitabaki na faida si chini ya milioni 30
 
Kuna mahind ya tanga, mbeya songea ni janga la kitaifa. Kiujumla kwangu changamoto ya mashine hasa kama za kusaga tulikuwa tunanunua plate nzito za 12inch tunachongesha mashine wenyewe kwahiyo unakuta mashine inakuwa nzito hata pale tulipokuwa tunabadilisha pull ili kuongeza speedy ilikuwa haisumbui. Kuhusu chekeche, Kwa SASA mahindi mengi ni masafi hayaji na vyuma vyuma. Roller hizo ni ajali kazini. Kuungua mota Sisi tulikuwa tunatumia mota kubwa 50hp mpaka 60hp hapo unapiga masaa 24 na mara nyingi tulikuwa tunanunua mpya kabisa sio hizi used. Mashine zetu ilikuwa kukoboa roller tano roller SITA, kusaga ni oversize. Kwa kuwasha mashine mbili yaani ya kusaga na kukoboa Kwa masaa 24 tulikuwa nanuwezo kupiga 15000 Sawa na viroba 420 vya unga.tukija kwenye faida hapa kwenu iko chini Sana maana Sisi iko mara moja na nusu ya ya kwenu. Location siwez taja hata Kwa dawa maana Nina mpango nirejee kivyangu
 
Itakuwa ushirikiano na sio ushirikina! Nawaza tu
 
Nyinyi naona mlikuwa mnatumia roller tatu na mashine zile ndogo za Sido za mota 30hp
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…