ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,652
Wamiliki wa baadhi ya baa za mji wa babati wamekuja na mtindo mpya. Huu unahusisha kuwawekea dawa za kienyeji wateja wanaowaona wana hela ili wawe wanywaji wa kudumu kwenye baa zao hali inayowafanya waingize kipato kizuri kupitia wanywaji hao.
Hutokeaje? Wamiliki wakishajua wewe ni mtu mwenye nazo, wanangoja uende chooni, wao kwa kuwatumia watu unaokunywa nao, wanaweka hilo 'limbwata' kwenye pombe iliyomo kwenye chupa au glasi. wewe ukirudi na kufakamia hicho kinywaji, ndo ntolee.
Hii imeshawatokea watu sita ninaowajua ambao hadi sasa wamefilisika kabisa kwani waligeuka na kuwa wanywaji wa pombe toka asubuhi hadi usiku wa manane. Hata kwenda kazini kwao ilikuwa ni vigumu. Wakiamka ni kwenda baa, baada ya kazi ni baa.
Kwa wageni mnao au mtakaotembelea babati, habari ndo hiyo...........wambulu wameamua kuja kivingine kabisa, kazi kwenu!
Hutokeaje? Wamiliki wakishajua wewe ni mtu mwenye nazo, wanangoja uende chooni, wao kwa kuwatumia watu unaokunywa nao, wanaweka hilo 'limbwata' kwenye pombe iliyomo kwenye chupa au glasi. wewe ukirudi na kufakamia hicho kinywaji, ndo ntolee.
Hii imeshawatokea watu sita ninaowajua ambao hadi sasa wamefilisika kabisa kwani waligeuka na kuwa wanywaji wa pombe toka asubuhi hadi usiku wa manane. Hata kwenda kazini kwao ilikuwa ni vigumu. Wakiamka ni kwenda baa, baada ya kazi ni baa.
Kwa wageni mnao au mtakaotembelea babati, habari ndo hiyo...........wambulu wameamua kuja kivingine kabisa, kazi kwenu!