Kecha Boksi
Member
- Nov 5, 2010
- 55
- 109
Wasalaam,
Hizi barabara mpya na za kisasa za kuingia kwenye miji yetu mikubwa ni kwa ajili ya kupendezesha miji?
Fikiria barabara kubwa ya kuingia mji mkubwa wa kibiashara Tanzania? Njia nne kwenda njia nne kurudi. Anzia Kimara mwisho hadi inapoishia ni vibao vya hamsini mwanzo mwisho. Kila mita chache kibao cha hamsini na trafiki waliojificha wengi vibao vinapoishia.
Madereva kwenye barabara hii wanateseka sana. Wanatembea kwa mateso sana kwenye hii barabara. Wakizidisha spidi ya hamsini ni tozo ama kubrashi viatu kwa kwenda mbele.
Haya tuseme hii ya kuingia jiji la Makala haijaisha na haijakabidhiwa. Twende Chuga. Barabara mpya na ya kisasa toka Tengeru hadi town. Mandhari yamependeza.
Ila kuta madereva walivyo waoga barabara hii? Kila kona vibao vya hamsini. Zidisha ulipe tozo ama ubrashi viatu. Yaani Tengeru hadi town Arusha ni kipande kigumu sana kwa madereva.
Sawa, kuna watumiaji wengine wa barabara. Waenda kwa miguu na wengineo. Ina maana hii miradi mikubwa ya mabarabara imeshindwa kutambua haya? Kwanini hawakuweka vivuko vya waenda kwa miguu ili madereva waache hofu? Mbona kwingine wamefanya hivi kwenye barabara zao na kila mtu ana amani?
Hao wanaofanya upembuzi yakinifu na usanifu miradi hii ya barabara ni trafiki ili wapate tozo na kubrashi viatu? Ama lengo kuu ni kutoa na kuingiza magari na watumiaji wengine kwa usanifu kwenye miji yetu?
Aagh..naomba nikachote maji nasikia yameanza kutoka.
Hizi barabara mpya na za kisasa za kuingia kwenye miji yetu mikubwa ni kwa ajili ya kupendezesha miji?
Fikiria barabara kubwa ya kuingia mji mkubwa wa kibiashara Tanzania? Njia nne kwenda njia nne kurudi. Anzia Kimara mwisho hadi inapoishia ni vibao vya hamsini mwanzo mwisho. Kila mita chache kibao cha hamsini na trafiki waliojificha wengi vibao vinapoishia.
Madereva kwenye barabara hii wanateseka sana. Wanatembea kwa mateso sana kwenye hii barabara. Wakizidisha spidi ya hamsini ni tozo ama kubrashi viatu kwa kwenda mbele.
Haya tuseme hii ya kuingia jiji la Makala haijaisha na haijakabidhiwa. Twende Chuga. Barabara mpya na ya kisasa toka Tengeru hadi town. Mandhari yamependeza.
Ila kuta madereva walivyo waoga barabara hii? Kila kona vibao vya hamsini. Zidisha ulipe tozo ama ubrashi viatu. Yaani Tengeru hadi town Arusha ni kipande kigumu sana kwa madereva.
Sawa, kuna watumiaji wengine wa barabara. Waenda kwa miguu na wengineo. Ina maana hii miradi mikubwa ya mabarabara imeshindwa kutambua haya? Kwanini hawakuweka vivuko vya waenda kwa miguu ili madereva waache hofu? Mbona kwingine wamefanya hivi kwenye barabara zao na kila mtu ana amani?
Hao wanaofanya upembuzi yakinifu na usanifu miradi hii ya barabara ni trafiki ili wapate tozo na kubrashi viatu? Ama lengo kuu ni kutoa na kuingiza magari na watumiaji wengine kwa usanifu kwenye miji yetu?
Aagh..naomba nikachote maji nasikia yameanza kutoka.