A
Anonymous
Guest
Mimi ni mkazi wa Kigamboni, na tunakabiliwa na changamoto ya barabara ya kutoka Mjimwema hadi Dege.
Barabara hii ipo karibu na makazi ya watu, na katika ukarabati wa sehemu zilizoharibika, lami huchimbwa na kuacha barabara ya vumbi kwa zaidi ya miezi sita kabla ya kurekebishwa. Hali hii imekuwa kero kwa wakazi wa maeneo hayo kutokana na vumbi linalosababishwa.
Aidha, wakati ukarabati ukikamilika, mara nyingi sehemu nyingine tayari zimeharibika, jambo ambalo linakwamisha juhudi za kuboresha barabara hiyo kwa ufanisi.
Tunaomba mamlaka husika zizingatie muda wa ukarabati ili mashimo yanapochimbwa, marekebisho yafanyike kwa haraka, na kero hii iishe.
Barabara hii ipo karibu na makazi ya watu, na katika ukarabati wa sehemu zilizoharibika, lami huchimbwa na kuacha barabara ya vumbi kwa zaidi ya miezi sita kabla ya kurekebishwa. Hali hii imekuwa kero kwa wakazi wa maeneo hayo kutokana na vumbi linalosababishwa.
Aidha, wakati ukarabati ukikamilika, mara nyingi sehemu nyingine tayari zimeharibika, jambo ambalo linakwamisha juhudi za kuboresha barabara hiyo kwa ufanisi.
Tunaomba mamlaka husika zizingatie muda wa ukarabati ili mashimo yanapochimbwa, marekebisho yafanyike kwa haraka, na kero hii iishe.