Barabara ya Moro - Dodoma yafunguliwa Baada ya kufungwa kwa saa mbili na Wananchi wa mkundi akipinga ajali za mara kwa mara

Barabara ya Moro - Dodoma yafunguliwa Baada ya kufungwa kwa saa mbili na Wananchi wa mkundi akipinga ajali za mara kwa mara

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Barabara Kuu ya Morogoro-Dodoma ambayo mapema leo Septemba 5, 2024 ilifungwa na wananchi wa Mtaa wa Mkundi Sheli, Kata ya Mkundi, Manispaa ya Morogoro, kwa takriban saa mbili wakipinga ajali za mara kwa mara zinazotokea katika eneo hilo imefunguliwa.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, ACP Yohana Mjengi amewataka wananchi hao kuwa wavumilivu na kuepuka kuchukua sheria mkononi pia kuacha kufunga barabara na kueleza kuwa Jeshi la Polisi linafuata taratibu na sheria katika kushughulikia matatizo ya usalama barabarani.

Wananchi hao walifunga barabara hiyo baada ya malalamiko ya muda mrefu ya ajali zinazodaiwa kusababishwa na madereva wa mabasi na magari makubwa hususani ya mizigo yanayopita katika barabara hiyo.

 
Barabara Kuu ya Morogoro-Dodoma ambayo mapema leo Septemba 5, 2024 ilifungwa na wananchi wa Mtaa wa Mkundi Sheli, Kata ya Mkundi, Manispaa ya Morogoro, kwa takriban saa mbili wakipinga ajali za mara kwa mara zinazotokea katika eneo hilo imefunguliwa...
"Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, ACP Yohana Mjengi amewataka wananchi hao kuwa wavumilivu"! Kauli hii ni ya mlevi, hauwezi kuvumilia kufa labda polisi wanaweza kutokana na kuishi kwa amri toka juu. Kamanda anayo taarifa ya matukio ya ajali eneo hilo isipokuwa "wanalifanyia kazi"!
 
ACP Yohana Mjengi amewataka wananchi hao kuwa wavumilivu na kuepuka kuchukua sheria mkononi pia kuacha kufunga barabara na kueleza kuwa Jeshi la Polisi linafuata taratibu na sheria katika kushughulikia matatizo ya usalama barabarani
Aache uongo
  1. Wao wakiwapiga wananchi huwa wamefuata sheria gani?
  2. Wakiwateka watu huwa wamefuata sheria hpgani?
  3. Wakichukua rushwa huwa wamefuata sheria gani?
 
Bado eneo la Nane Nane_Oil com Morogoro nako ajali kila siku. Matuta madogo yani gari zinapepea tu
 
Back
Top Bottom