Mara nyingi husikia watoto wakisema ashikrimu wakitaka hizo lambalamba (wengine husema rambaramba hichi si kiswahili sahihi neno kuu ni Lamba na sio ramba)
Lamba inamaana ya kula kutumia ulimi kwa mtindo wa kutembeza ulimi ama kinacholiwa kwa kupakaza ulimi.
Baba Wa3 kuna maneno umeyatumia huwa yananichefua kidogo nikikutana na mtanzania mtumiaji wa kiswahili akiyatamka mfano
unitatiza badala ya Hunitatiza (ukiacha ile herufi H basi maana inabadilika na kumtatiza msomaji/msikilizaji)
vilevile kwa maneno "umaanisha" usahihi wake ni humaanisha.
Mkuu kibunango hebu tizama/tazama maneno niliyoyatilia rangi uniambie yakoje masikioni mwa msikilizaji
'Kuna barafu ambayo inatokana na uchanganyaji wa maziwa na maji na radha kidogo ya kahawa ama iriki ama maji na ukwaju, na inaweza kuongezwa rangi ili kuvutia inaitwa Malai.'
lengo langu sio linginelo zaidi ya kutaka tujitahidi kutumia kiswahili vizuri zaidi kwa kadri tuwezavyo ili tuweze kuwafunza na wengine kiswahili kizuri.