Barakoa 😷 Kujilinda na COVID-19 zauzwa Tshs. 2000 na Bila kuivaa huingii lango la Hospitali kwenda kupata matibabu

Barakoa 😷 Kujilinda na COVID-19 zauzwa Tshs. 2000 na Bila kuivaa huingii lango la Hospitali kwenda kupata matibabu

Fya-fyafya

Member
Joined
May 2, 2019
Posts
43
Reaction score
125
Ugonjwa wa Corona Virus au Covid-19 unazidi kuleta madhara na kusababisha vifo mbali mbali duniani na hapa nchini.

Bila shaka nchi yetu ndo miongoni mwao nchi chache barani Afrika ambazo zimechukua tahadhari kadhaa bila kufungia wananchi wake ndani (Lockdown) na kuacha wananchi waendelee kufanya shughuli za uzalishaji huku wakihadhari. Hili ni jambo ambalo sisi watanzania tunalipongeza sana tena sana.

Kutokana na hali kuonekana kuanza kuwa mbaya kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotangazwa kwa sasa, Hospitali na vituo vya afya zimeanza kutoruhusu wagonjwa kuingia Getini la Hospitali bila kuwa wamevaa Barakoa. Hili ni jambo la kupongezwa na la maana sana kujilinda na maabukizi.

Hata hivyo, hali ya barakoa moja kuuzwa Tshs 2000 imekuwa kidogo changamoto kwa wagonjwa hasa walala hoi. Je hakuna uwezekano bei ikapungua angalau ikauzwa kwa rejareja tshs 500 au tsh 1000.

Hakuna mtu anayependa kuugua huu ugonjwa au kuambukiza wengine huu ugonjwa. Sasa kama vifaa vya kujikinga vitakuwa bei ghali je wananchi wa hali ya chini watamudu?

Tunakoelekea, itakuwa kwamba huwezi ingia sokoni bila kuvaa barakoa😷 nalo ni jambo jema sana na kama watendaji wanaliona basi mapema lianze maana masokoni nako japokuwa tunanawa mikono hatuko salama 100%.Basi watu tuvae barakoa kujilinda kikamilifu na iwe lazima kwa muuzaji na mteja wote tuvae barakoa.

Inasemekana barakoa moja inashauliwa kuvalia kwa masaa 4 mfululizo na baada ya hapo itolewe na mtu avae nyingine. Je kama zitakuwa zinauzwa Aghali je wananchi watamudu?

Si kila anende hospitali anaumwa, wengine huwapelekea chakula ndugu zao wagonjwa waliolazwa. Sasa kama mtu alikuwa amejiandaa na nauli halafu anakuta stop getini ya kotoingia bila kuvaa barakoa hapo huwa mtihani.

Kama mama amempeleka mtoto kwenye matibabu, hapa inamlazimu kununua barakoa Mbili : ya kwake (mama) na mtoto pia.Kwa hali hiyo mama atagharamia sh 4000.

My takes.

Barakoa zigawe bure au zipungue bei na zivaliwe na kila mtu sehemu ya mkusanyiko.

Kwa sasa si muda wa Hospitali na maeneo ya public ya mkusanyiko kufanya biashara za hizi Barako. Wazitoe kama huduma na kama inagalimu basi zitolewe kwa bei nafuu sana.
 
... sio maeneo ya hospitali tu; kwa hali ya ugonjwa iliyopo hususan Dar es Salaam kwa sasa, barakoa inapaswa ivaliwe kwa lazima in all public areas! In short ni nyumbani kwako tu, ila zaidi ya hapo wananchi wanapaswa kuvaa barakoa kama serikali ingekuwa proactive!
 
..barakoa zigawiwe bure kwa wananchi.
Huo ndio utaratibu tuliotegemea kuusikia kutoka kwa viongozi hususan Dar es Salaam kwenye maambukizi mengi. Nilitegemea Makonda awe ameelekeza hivyo muda mrefu uliopita ila ndio hivyo!
 
Nimeenda hospitali leo pale Mnazi Mmoja hakuna kuchekiwa wala nini zaidi ya kupuliziwa maji yenye dawa tu .

You'd think a hospital of all places wangekua strict ila waapi . Si Madokta wala manesi waliovaa hizo mask
 
Ugonjwa wa Corona Virus au Covid-19 inazidi kuleta madhara na kusababisha vifo mbali mbali duniani na hapa Nchini.

Bila shaka nchi yetu ndo miongoni mwao nchi chache barani Afrika ambazo zimechukua tahadhari kadhaa bila kufungia wananchi wake ndani ( Lockdown) na kuacha wananchi waendelee kufanya shughuli za uzalishaji huku wakihadhari.

Kutokana na hali kuonekana kuanza kuwa mbaya kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotangazwa kwa sasa, Hospitali na vituo vya afya zimeanza kutoruhusu wagonjwa kuingia Getini la Hospitali bila kuwa wamevaa Barakoa. Hili ni jambo la kupongezwa na la maana sana kujilinda na maabukizi.

Hata hivyo, hali ya barakoa moja kuuzwa Tshs 2000 imekuwa kidogo changamoto kwa wagonjwa hasa walala hoi. Je hakuna uwezekano bei ikapungua angalau ikauzwa kwa rejareja tshs 500? Kwa kweli hili nalo ni janga.

Hakuna mtu anayependa kuugua huu ugonjwa au kuambukiza wengine huu ugonjwa. Sasa kama vifaa vya kujikinga vitakuwa bei ghali je wananchi wa hali ya chini watamudu?

Tunakoelekea, itakuwa kwamba huwezi ingia sokoni bila kuvaa barakoa😷 nalo ni jambo jema sana na kama watendaji wanaliona mapema na kianze maana masikini nako japokuwa tunanawa mikono basi watu tuvae na barakoa kujilinda kikamilifu. Iwe lazima kwa muuzaji na mteja kuvaa barakoa.

Barakoa inashauliwa kuvalia kwa masaa 8 mfululizo na baada ya hapo itolewe na mtu ambaye nyingine. Je kama zitakuwa zinauzwa Aghali je wananchi watamudu?

My take.

Barakoa zipungue bei na zivaliwe na kila mtu sehemu ya mkusanyiko.
Kama inatakiwa kuvaliwa kwa masaa 8 tu,ina maana kwa siku mtu unatakiwa utumie Barakoa 2 hasa kwa sisi tunaokwenda kwenye mihangaiko ya kutafuta pesa,hiyo ina maana tayari ni 4,000.00...!!
 
Ugonjwa wa Corona Virus au Covid-19 inazidi kuleta madhara na kusababisha vifo mbali mbali duniani na hapa Nchini.

Bila shaka nchi yetu ndo miongoni mwao nchi chache barani Afrika ambazo zimechukua tahadhari kadhaa bila kufungia wananchi wake ndani ( Lockdown) na kuacha wananchi waendelee kufanya shughuli za uzalishaji huku wakihadhari.

Kutokana na hali kuonekana kuanza kuwa mbaya kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotangazwa kwa sasa, Hospitali na vituo vya afya zimeanza kutoruhusu wagonjwa kuingia Getini la Hospitali bila kuwa wamevaa Barakoa. Hili ni jambo la kupongezwa na la maana sana kujilinda na maabukizi.

Hata hivyo, hali ya barakoa moja kuuzwa Tshs 2000 imekuwa kidogo changamoto kwa wagonjwa hasa walala hoi. Je hakuna uwezekano bei ikapungua angalau ikauzwa kwa rejareja tshs 500? Kwa kweli hili nalo ni janga.

Hakuna mtu anayependa kuugua huu ugonjwa au kuambukiza wengine huu ugonjwa. Sasa kama vifaa vya kujikinga vitakuwa bei ghali je wananchi wa hali ya chini watamudu?

Tunakoelekea, itakuwa kwamba huwezi ingia sokoni bila kuvaa barakoa😷 nalo ni jambo jema sana na kama watendaji wanaliona mapema na kianze maana masikini nako japokuwa tunanawa mikono basi watu tuvae na barakoa kujilinda kikamilifu. Iwe lazima kwa muuzaji na mteja kuvaa barakoa.

Barakoa inashauliwa kuvalia kwa masaa 8 mfululizo na baada ya hapo itolewe na mtu ambaye nyingine. Je kama zitakuwa zinauzwa Aghali je wananchi watamudu?

My take.

Barakoa zigawe bure au zipungue bei na zivaliwe na kila mtu sehemu ya mkusanyiko.
....hoja yako ni mhimu Sana mamlaka husika wanapaswa kuliona hili mapema mfano serikali imefungua akaunti wadau waweze kuchangia chochote kukabiliana na janga hili pia juzi kati mh waziri mkuu kapokea pesa kutoka kwa wadau ili kusaidia janga hili nazani serikali ingetumia ilo fungu kutengeneza barakoa kwa wingi na kuzigawa ili kila mwananchi asitembee bila kuvaa sehemu yoyote au waongee na viwanda vya ndani vizalishe barakoa kwa bei ya tsh 200 hii kila mwananchi ataweza kumudu....

Tukumbe vipato vya wanachi wetu vimeyumba sababu ya mdororo wa uchumi wa dunia kwasababu ya covid-19 sasa tukiacha wauzaji wauze bei ya 2,000 wakati pato la mwananchi liko chini ya Dora moja tutaumia sisi wanyonge tusiokua na uhakika ata wa mlo mmoja
 
Je ni lazima wagonjwa wanunue mask kutoka kwao?
Sehemu nyingi nchi zingine sasa hivi ni lazima kuvaa mask au kufunika mdomo na pua kwa njia yoyote ya kitambaa hili kupata uduma. Kama mtu hana mask maalum, wanatumia kilemba, kitambaa chochote kufunika pua na mdomo.

Kwahio ni muhimu kuruhusu raia watumie kitambaa chochote kuziba pua na mdomo hili kupunguza usumbufu. Kanga za zamani mtu anaweza kutumia kukata na kukunja mara tatu akafunika mdomo na pua kama hana hela ya kununua mask. Muhimu ni kuhakikisha kitambaa ni kisafi.

Tuache uvivu wa kufikiri kwamba kila kitu hatuwezi au hakiwezekani. Kuna mitambala mibovu majumbani mengine mnatumia kupigia deki lakini mnashindwa kutumia kuziba midomo na pua kujikinga na hili janga.

Huu ugonjwa upo na uamaliza watu. Ni muhimu kuchukua hatua mapema kuliko kusubiri hapo baadae hali ikiwa mbaya.
 
Nimeenda hospitali leo pale Mnazi Mmoja hakuna kuchekiwa wala nini zaidi ya kupuliziwa maji yenye dawa tu .

You'd think a hospital of all places wangekua strict ila waapi . Si Madokta wala manesi waliovaa hizo mask
...duu! huo ni uzembe mkubwa ilitakiwa kuwaliporti mamlaka husika.... kwasasa haitakiwi kumchekea mtu ukiona anahatalisha maisha ya watu kwa uzembe bora uonekane mbaya lakini ulinde jamii....hii ngoma ikikorogeka hapa tutaumia wote
 
Back
Top Bottom