Baraza Dogo la Mawaziri na Muundo wa Wizara



Mkandara

Soma tena post yangu. Sijasema kuwa hizo Wizara ziko kwenye ngazi ya states- nilichosema ni kuwa federal government inashughulikia masuala mapana. Ndio maana inaweza kuwa na wizara chache tu. Lakini kuna mambo mahususi ambayo usimamizi wake unafanyika kwenye ngazi ya states pekee.

Nakupongeza kwa initiative yako kuhusu soko la kahawa!

Ni kama Tanzania na Zanzibar- utaambiwa hili ni suala la muungano, hili silo hivyo Zanzibar wanawizara zao katika masuala ambayo si muungano. Kama kungekuwa na serikali ya Tanganyika; ni wazi serikali ya Muungano ingekuwa na Wizara chache tu za masuala ya Muungano. Mambo mengine yote mahususi Tanganyika na Zanzibar wangejiamulia wenyewe kila mmoja kivyake. Sasa ile miundo ya usimamizi ya state level, si lazima iitwe wizara- wanaweza kuwa makatibu au makamishna nk. La msingi ni mgawanyo wa majukumu kati ya federal government na state!

Hayo ya Azimio la Zanzibar na masuala ya utandawazi ni mjadala mwingine.

JJ
 
Katika mabadiliko ya Katiba ambayo tutaanza kuyavalia njuga siku chache zijazo jambo moja ambalo tunaweza kufanya ni kudefine Wizara Kuu za Kikatiba ambazo Rais yeyote bila kujali itikadi au chama chake lazima aziunde. Pia ni lazima tuweke kikomo cha kikatiba cha kusema Rais anaweza kuunda wizara zisizodi ngapi.

Binafsi naamini Katiba inaweza kudefine wizara zifuatazo kuwa ni za msingi na lazima ziundwe.

a. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
b. Wizara ya Usalama na Mambo ya Ndani (Prison, Magereza na TISS)
c. Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
d. Wizara ya Katiba, Haki, na Sheria (Mara nyingi I have this feeling kuwa Magereza iwe chini yake)
e. Wizara ya Afya na Mazingira
f. Wizara ya Fedha na Uchumi
g. Wizara ya Elimu (kusimamia elimu zote)
h. Wizara ya Sayansi, Technolojia na Nishati
i. Wizara ya Rasilimali Madini
j. Wizara ya Mawasiliano na Habari

Halafu ukiondoa hizo. Rais anaweza kuunda wizara nyingine zisizozidi kumi katika wakati wa kawaida.

Na wakati maalumu au wakati wa dharura au wenye kuhitaji uangalizi maalumu Rais anaweza kuunda wizara yoyote lakini isiyofanya idadi ya wizara at any given time isizidi Wizara 23.

Hivyo wakati wa vita kwa mfano, Rais anaweza kuunda Wizara ya Vita, wakati wa Ukame kwa mfano na njaa anaweza kuunda Wizara ya Majanga n.k

Faida ya kuwa na mfumo huo:

a. Wizara kumi hazitahitaji kubadilisha vitendea kazi au gharama za kuset up wizara mpya. WAnabadilisha majina ya wakuu wake tu n.k HIvyo hakuna kukisia kuwa Raia ataunda wizara "gani" kwani tunajua kumi tayari.

b. Kwa kuweka idadi ya wizara inamzuia Rais kujiundia "viwizara" kama zawadi za kisiasa. Hili ndilo lilikuwa tarizo la Baraza lilipoita kwamba Rais ikamlazimu kuunda wizara ili atoe shukurani. Hivyo tukimwekea mipaka Rais wa chama chochote kile tunajua before hand kuwa hataunda wizara thelathini au arobaini hadi na zaidi ili watu wake na wenyewe wapate.

Na baada ya kufanya mambo hayo kikatiba, hatuna budi pia kuelezea kuwa wizara gani haziwezi kuwa na manaibu waziri (kama ilivyo sasa kwenye baadhi ya "Wizara za Nchi". Ni vizuri pia kudefine kwenye zile wizara kuu kuwa watakuwa na manaibu waziri wasiozidi wawili. Wakati wizara zitakazoundwa na Rais hazitakuwa na Manaibu Waziri bali zitaongezewa Makatibu Wakuu wa Idara zake, Na Katibu Mkuu Mwandamizi wa Wizara.

That is what I'll do anyway...
 
Hivi kweli SMZ ina Wizara Chache- is it more effective?

Maanake ktk Afya na Elimu kumechoka Visiwani hakuna dawa, madaktari choka mbaya na shule za mwisho2 mtihani uliopita zilitoka Visiwani!
 
Mi nakubaliana na muunganiko wa baadhi ya Wizara na pia kufutwa kwa baadhi ya Wizara kama zilivyoainishwa na ndugu yangu Mnyika bila ya kujali hiyo ni manifesto ya CHADEMA au chama kingine chochote cha siasa. Kama ni jambo/wazo zuri sioni ubaya wa kulitumia maana hata wapinzani dhamira ni moja tu. Kujenga. na si vinginevyo.
 
Mimi napenda hizi wizara ziwe fixed (za kudumu),
sio kila anayekuja anakuja na utashi wake,kuongeza au kupunguza.
Hapo ndio mwanzo wa mafaili kupotea,na gharama kubwa ya kuchapa headed paper, magari kubadilisha nembo, n.k

Nafikiri inabidi tufikie wakati tuseme wizara zetu ni hizi, (hata na historia zake zinaweza kufuatiliwa vizuri).
 


John nadhani Mkandala anachomaanisha ni kwamba kwa nchi masikini mfano wa Tanzania,siyo lazima tuwe na sera ya majimbo ya CHADEMA ndipo tuweze kuwa na baraza dogo la mawaziri.Baraza dogo ni LAZIMA hata kwa serikali ya CCM na litaleta ufanisi hata pasipo serikali za majimbo.

'It is the mark of an educated mind to be able to entertain a thought without accepting it'
 
John,
Hivi unataka kusema Rais aunde wizara kwa kufuata manifesto ya CHADEMA na wala siyo yale ambayo anataka kuyatelekeza kwa mujibu ya manifesto ya Chama chake?
Tafadhali naomba ufafanuzi.
HUYU PUNDAMILIA NAYE NA MAMBO YAKE YA VYAMA!
 
Ni wazi kuwa ni wazo zuri na JK anaelewa hilo!Huko CHADEMA KUNA VICHWA NA ONCE AGAIN JK ANAELEWA HILO..HATAKI KUWEKA WAZI..LAKINI MUULIZE ZITTO ATAKUMEGEA..JK ANAZIMIA VICHWA FLANI UPINZANI SEMA KUNA KINA PUNDAMILIA NA VINGUNGE AMBAO WANAHISI JOTO HIVYO WANAKUMBATIA SIASA ZA DIVISION IN LEAU OF OUR NATIONAL INTERESTS!WANAMMINYA JK KWA VISINGIZIO VYA UCCM NA UCHADEMA..NANI KASEMA MAWAZO YA KUIENDELEZA NCHI YETU YATOKE KWENYE TABAKA MOJA MILELE?
 
NI KWELI TUMESHUPALIA MAJINA YA MAWAZIRI ZAIDI YA WIZARA ZITAKAZOUNDWA!TUNAPENDA MAJINA ZAIDI YA WAJIBU WA VIONGOZI HAO NA NINI WATAKACHOKWENDA KUKIFANYA HUKO KWENYE WIZARA ZAO!
 
FDL,
Shukran mkuu ndiyo maana yangu haswa kwa sababu J.J. Mnyika mkuu wangu ulitumia mfano wa Majimbo kuwa ndio solution na CCM hawautaki hapo ndipo nikazua hoja.
Nadhani muhimu zaidi sio kutazama sera za chama tunapofikiria muundo wa baraza la Mawaziri na mimi nakubaliana na wale wote waliosema muundo wa baraza la Mawaziri liwe la kudumu kisheria hata kama itakuwa ni serikali ya mseto (coalition government).
Pia kisheria inatakiwa ziwekwe ilani zinazoeleza wazi ni wakati gani serikali inatakiwa kuunda serikali ya mseto na ni hatua gani lazima zifanyike na sio Mtawala kuamua kuvuta watu anaowataka yeye bila kujali mawasiliano na chama kinacho msimamisha..
Nasema hivi kwa sababu nasikia JK ana mpango huo bila kuwasiliana na vyama vinavyohusika. Ni kama vile CCM wamepata dawa ya kupambana na vyama pinzani -Kuiba watu toka vyama pinzani kwa kuwaahidi nafasi za Uawaziri hivyo kujijengea jina kwa uchaguzi wa 2010.
Jamani tuweni macho na nyie kina Zitto kuweni macho, fikirini nje ya kabati la Kuula ama kufikiria kwamba mnaweza safisha machafu ya CCM ndani ya kapu la CCM.
 
Hivi ile sera ya majimbo si ni better kwasababu wananchi wanapata nafasi ya kupata maendeleo na huduma muhimu za jamii kwasababu pasenti flani at least 10% ya mapato inabaki jimboni kuwasaidia wananchi katika shughuli muhimu za jamii pamoja na huduma muhimu?Kwani sera ya sasa si ni bado ya central govenment ambapo pesa zote za wavuja jasho zinapelekwa huko halafu mafisadi wanazipiga panga kwenye bajeti zao njaa na kujichote nyingine bila huruma?Si Mh Rais mwenyewe ndiye alikiri kwa yule waziri mkuu wa nchi moja za ulaya kuwa zile bilioni 133 za EPA scandal zilikuwa za wananchi na sio za misaada?Labda mimi sijailewa vizuri..tafadhali tuelimishane kwenye hili.
 
Wakuu hivi kweli watu mnategemea anything new in this cabinet? (no pun intended) but knowing our president and his style of work, I really doubt if he is upto the task of giving us fresh and committed people/managers to run our country. Why because in TZ as in most African countries ministerial appointment is just to reward political royalty. Thats no different in Tanzania. Trust me, mtaniambia..I really dont see anything new coming out. If competence was the main criteria then Iam sure we could expect something positive. But unfortunately not. You will just hear the usual names..Chiligatis, Meghjis, et al! Yaani sisi watanzanzia ni kondoo kabisa..just see how people are very excited as if the process is going to open a new era in our country..its business as usual.....

Anyhow, being eternal optimist, perhaps something good will come out of this process. But its a big IF and only a big IF!
 
Masanja,

Kazi iko kwake kuthibitishia Watanzania kuwa JF ni waongo na hawana upevu kujua mambo!😉
 
Pundamilia naona John bado hajakujibu, I hope atafanya hivyo baadaye. Lakini kama nimemwelewa John, hapa sio issue ya manifesto ya chama tena hapa ni issue ya utaifa. Yawezakuwa ni mambo ambayo walishawahi kuongea kama Chadema but ni proposal ambayo kama umeipitia pasipokuweka issue ya uchama imekaa vizuri ina mapungufu kidogo ya hapa na pale lakini imesimama anyway.

Kuna mtu amesema kwamba lazima kila mkoa utoe mawaziri wawili. Hii kitu hata msanii wetu mkuu jk aliwahi kuiongelea mimi siielewei kbs na nimeanza kuisikia hivi karibuni sijawahi kuisikia wakati wa nyerere wala mwinyi. Hivi what is the point here, tunakuwa na mawaziri kwa minajiri ya kufurahisha kila mkoa au tunakuwa na mawazri kwa ajili ya kuleta maendeleao kwenye hiyo mikoa? Ninahofu kwamba tumeanza kuiga vitu ambavyo kama watz sio asili yetu kabisa na huenda vikatucost baadaye. Nionavyo mimi siwezi kuwa na mawaziri 60 kuiplease mikoa wakati ni mzigo wa kurudisha nyuma maendeleo ya hiyo mikoa ninayotaka kuiplease.
 
Baraza la mawaziri litakuwa na mawaziri arobaini,litagawanyika kama ifutavyo;-
mawaziri ishirini na tano
ma naibu kumi na tano
 
You bet..!!


mh......,
sio mtu wa kubet mkuu,mie nina kawaida ya kutumia darubini naaangaliaga kwa mbali,tangu enzi za bcs,hila kwa hili karibu sana,
lingine ni usalama wa raia unarudi mambo ya ndani.
kwakifupi nimekubali kama mie nitakuwa sahihi naomba tushikiana katika mjadala wa jinsi ya kuwashugulikia hawa MAFISADI kwamujibu wa sheria zetu za Taifa,kupitia sheria zifuatazo;-

The Proceeds of Crime Act,
Mutual Assistance in Criminal Matters Act,
Tanzania Intelligence and Security Service Act,
Tanzania Public Leaders Code of Ethics,
Prevention and combating of Corruption Act, and
The Tanzania Anti Money laundering Act

Sizani kama watatuponyoka kwenye zote hizo,
Halafu kama nitakua nimekosea wewe utaamua nini nifanye
hila ushauri wa bure kwako,ningekuwa wewe ningeanza kuzipitia pitia hizo sheria hapo juu,Taifa litakuitaji sana katika hilo,shukran
 
Ndugu zangu wachangiaji nadhani hapa lazima tufikie kwa makini. Serikali yetu inamatatizo sana BOT,RICHMOND,MIKATABA YA MADINI na kadhalika. Imeonekana kwamba sasa hivi hakuna ule uamuzi halisi wa kufumbua vitanadawili hivyo vote ispokuwa kuunda serikali ya MSETO. Hii haina maana kwamba hao mawziri ambao watatoka katika upande wa upinzani watapiga porojo la CCM wakati watakapokuwa mawaziri wa serikali ya MSETO. Hapa itabidi tuweke “rangi zeu za vyama kando” ili kuliokoa TAIFA.

Kumbukeni serikali ya Mzee Nyerere ya kwanza pia ilikuwa ni SERIKALI YA MSETO kina Dereck Brysson na wengineo walikuwemo serikalini. Mabalozi wengine walitoka katika chama cha UTP kama Mtemvu mwenyewe.

Nadhani serikali ikiwa ni ya MSETO itavunjwa pia kabla ya uchaguzi 2010 wakati ambao huenda matatizo haya ya sasa yamekwisha pata ufumbuzi.

Njia ambao iko mbele yetu ni ngumu sana. MPAKA SASA NCHI YETU NI MASIKINI INGAWAJE TUNA UTAJIRI MWINGI KAMA MADINI YA DHAHABU, ALMASI, TANZANITE,MAKAAA YA MAWE(mgofi umepewa rais mstaafu Mkapa.. dhulam tupu), MISITU, na kadhalika.


SISI SOTE NI WATANZANIA HATA WAPINZANI PIA NI WATANZANIA.INABIDI KUOKOA NCHI YETU PAMOJA.

UMOJA NI NGUVU NA UPWEKE NI UDHAIFU! CCM PEKEE HAIWEZI NA HAITAWEZA KUTATUA SHIDA ZA NCHI YETU ASILAN. IMEDHIHIRIKA.
 

John,
Ahsante kwa ufafanuzi wako, nimekuelewa vizuri.
Have a good day.
 

Bobby,
Ahsante sana kwa angalizi lako, tayari John ameshanipatia maelezo nadhani unaweza kuyaona humu ndani.
Kila la heri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…