Baraza jipya la Mawaziri kujulikana Feb 12

Baraza la Mawaziri limekuwa gumzo hasa; nasikia JK anafanya mawasiliano na Wapinzani kuwa ndani ya Baraza, sijui ni za kweli soma Tanzania Daima ya leo.

Hio sio poa kaka maana upinzani lazima wawepo upinzani na kufanya kama wapaswavyo.We need a robust opposition to put the govt in check.Upinzani ukiungana na serikali nd'o basi tena kwa walalahoi!
 

Sasa akichukuwa upinzani nani atapiga kelele bungeni. Hawa jamaa wa CCM wanatufanyia mazingaombwe tu. Akina Anna Kilango-Malecela sasa wanatafuta ujiko. Wakati Kabwe na Silaa wanawasha moto wao walikuwa wapi? Wanataka kusema hawakuwa wanazijua hizi skandali. Bado kuna ufisadi mkubwa unaendelea TZ, hivyo wapinzani wazidi kufichua.
 
Sio rahisi ku-come up na new cabinet haraka hivyo. mimi mwenyewe nimesubiri sana only to get it that, postponed! Hata kesho hakuna uhakika wa kujua new cabinet. Wana JF wasipoteze muda wao kuwa ktk tension ya kusubiri, waendelee na shughuli zao tu hadi itakapotangazwa rasmi.
 

Invisible,heshima yako upewe,
mie ningependa kutofautiana nawe kuhusu hio ishu ya JK kuwateua wana-upinzani kuwemo serikalini.My belief is we need a robust opposition to keep the govt side in check.They should only come together in principle to benefit the masses.
Mature democracies dictate that the two sides have different principles of governance nd'o maana wako on two different sides. Opposition lazima waonesha they are the better side ili umma wawape kura next time around.If we are not careful CCM will gobble up everybody na kusiwe na upinzani wala nini.
Naomba kuwasilisha.
P.S. Uteuzi wa hili baraza kwani ni dili/siri.Akhhh!!!
 
mi naona kazi ni ngumu kwani kumtemesha mtu chakula ni ngumu sana,ila ngoja tusubili tuone.JK naye akichagua sana hawezi kuwapata mawaziri walio timilika kwa sababu kila waziri anatuhumiwa kwa njia moja au nyingine kuhusika na ufisadi
 
Swafi kabisa Mr Zero
Hao kina Malecela nd'o wanaitwa 'Johnny-come-lately'.Yaani wakisema hawakujua hizo skendo ni kama kututusi sie wabongo.Wewe na mie tunazijua na wao wakubwa wetu hawajui?Isshhhhhhhhhhhhhhh!!!!Huo ni uongo ulioje jamani?
 

Kithuku,safi sana ulivyosema kaka!Need i say more? I don't think so!
 
Jk asimrudishe tena mramba.Kwa kweli nitafurahi endapo Mramba,Msola,Mungai na Chenge hawatarudio bungeni.Jk inaonekana sasa ameanza kutulia
 
Baraza la Mawaziri limekuwa gumzo hasa; nasikia JK anafanya mawasiliano na Wapinzani kuwa ndani ya Baraza, sijui ni za kweli soma Tanzania Daima ya leo.

Huhitaji kuwa serikalini, usalama wa taifa, au ikulu kujua kwamba JK haundi serikali ya MSETO, vyama vya upinzani vinajua... na hata mwanakijiji kule kalimanzira anajua hilo...

Waziri Mkuu mpya ni kiboko... siri za kiani hamtazisikia tena.
 
Kuna taarifa kule Rock City eti watu wameandaa party Diallo akimwagwa wafanye sherehe ng'ombe zimeandaliwa watu wale nyama. Hawa naona wana matatizo na wivu binafsi Huyu EL kaiba hela hatuoni kaziivest wapi? na yule mtoto wake akitanua tu lakini Diallo kaleta ndege hadi nauli zimekuwa nafuu bora!!! WIVU TU
 
mi naona kazi ni ngumu kwani kumtemesha mtu chakula ni ngumu sana,ila ngoja tusubili tuone.JK naye akichagua sana hawezi kuwapata mawaziri walio timilika kwa sababu kila waziri anatuhumiwa kwa njia moja au nyingine kuhusika na ufisadi

Kitio...mmmhhh!...bonge la jina.Heshima yako bro.

Kama JK hana watu wasafi wenye maadili ya kueleweka then dissolve the damn Bunge na itisha kura upya.The campaign theme should be "viongozi safi wasio na skendo". Nakwambia asilimia kubwa ya hawa mabwana hawatorudi.Asante.
 

Ngoma nzito,
Kitanda usichokilalia huwezi kujua kunguni wake. Nahisi mimi na wewe hatuko Mwanza na wala huenda hatuzijui siasa za Mwanza. Hawa wapiga kura wa Mwanza huenda wana lao jambo na Mheshimiwa wao Tony Diallo, na ndio sababu inayowafanya waandae sherehe. Kumbuka habari za Marehemu Akukweti kule Tunduru, kama unafahamu ilikuwaje kule basi huenda una jibu la hawa ndugu wa Mwanza.
 

Wivu tu? are you sure? Sasa wewe ndugu una hakika huyo jamaa hizo pesa amepata kutokana na mshahara wake au biashara zake halali? Unajua kama kusingekuwa nan ufisadi Tanzania hali isingekuwa ovyo kama ilivyo sasa? Ni hakika watu wa mwanza si wendawazimu wameurahie mabaya yanapomfika mwanamwanza mwenzao!
 
JK awache wapinzani nje ya baraza lake la mawaziri. Kama hana watu wa kutosha kwenye chama chake basi wajiuzulu uchaguzi ufanyike upya. Kuwachukua wapinzani ni mbinu za kufifisha nguvu za upinzani na kuwahadaa wananchi.Nani atatetea masilahi ya taifa? kweli Slaa na Zitto wataweza simama kama alivyofanya kama ni mawaziri wa serikali? Ataua upinzani na itampa ticketi ya bure kushinda 2010. Hii itakuwa mbinu ya kuzima atu midomo.letu sikio.
 

yaah nafikiri ni kazi ngumu sana kupanga upya maana wizara nyingine zitapunguzwa. Habari nilizopata ni kuwa Hazina itaungana na wizara ya mipango kuwa wizara moja.
 
JK ni CCM damu na haamini katika Upinzani kwa undani ila kwa nje. Ana chuki mbaya na upinzani na hata imefikia sasa anaogopa kuwa na Mgombea binafsi. JK anasema yote ila chini kwa chini wanawanunua wapinzani. Makamba anafanya haina maana kwamba JK hajui haya. Wako wapi akina Tambwe and the likes. JK anaweza kufanya mabadiliko lakini si kuwapa wapinzani nafasi. Mimi wala siombei wapewe nafasi ila sheria ya Uchaguzi ziwe huru kabisa hapo utaona watakavyo washindwa CCM na kuichukua Nchi. Kazi ni kubwa hata donors wamegomea pesa zao hadi waone mwelekeo JK ana mengi moyoni .Anavyo penda safari kaacha kwenda Ulaya? Kweli yamemfika.
 
Pia Mwanasheria Mkuu asirudi kabisa. Hili litakuwa fundisho kubwa kwa Mwanasheria atakayefuata. Siku zote tumekuwa tukilalmikia mikataba mibovu na mwnasheria (tangu enzi za Chenge). I this this could be our break through kwenye tatizo la mikataba mibovu!!!
 
Wapinzani kupewa nafasi ya uwaziri sio kwamba watafungwa midomo, mi nadhani changa moto kwa government itakuwa kubwa zaidi na ndicho kile kitu mi natazamia kutoka kwa JK. Kama hakuna watu wa kuhoji mambo toka kwenye preliminary stages then tutakuwa tuna cheza tu kusubiri mpaka Slaa au Kabwe aibue hoja bungeni wakati tayari Taifa limeshaingia hasara ya billions, pia mda unapotea kujadili mambo yaliyo wazi kabisa! Bunge sasa linatakiwa kutumiwa vizuri kama tulivyo ona hivi majuzi. Sio wabunge wanatumia pesa za serikali kujadili mambo ya watu binafsi ihali wananchi hawana huduma muhimu karibu. Jamani naishia hapa, ngoja tusubiri baraza kuwekwa wazi hapo kesho kama tulivyopatia dondoo.

Kaka K
 
Swafi kabisa Mr Zero
Hao kina Malecela nd'o wanaitwa 'Johnny-come-lately'.Yaani wakisema hawakujua hizo skendo ni kama kututusi sie wabongo.Wewe na mie tunazijua na wao wakubwa wetu hawajui?Isshhhhhhhhhhhhhhh!!!!Huo ni uongo ulioje jamani?

In all fairness to Mama Kilango, nilivyofuatilia mjadala wa Zitto kuzibwa mdomo Mama Kilango aliprotest kwa kutoka nje ya bunge naamini baada ya machinery ya CCM kum-silence, mpaka magazeti yaliandika.

Sio kila mbunge wa CCM ana partisan politics.Tunahitaji kila mbunge atakayetusaidia katika vita dhidi ya ufisadi.Bila huyu mama taarifa za Hansard zingekuwa zina rekodi ya mwisho kwamba Lowassa kaonewa according to his resignation speech (albeit with no point by point rebuttal).Mama Kilango ali set the record straight kwa kusoma vimemo bungeni.It takes courage in CCM to do that at a time when some CCM MPs were clearly defending Lowassa.
 

Diallo bonge la primitive,

kuanzia kufiligua housegirls mpaka wafanyakazi wake, very primitive indeed.I will celebrate kama watu crude kama hawa wanaondolewa katika serikali, wanapunguzia heshima hizi ofisi.

Kama mtu ni primitive familia yako mwenyewe inaweza kufurahia downfall yako, sembuse watu wa mkoa mmoja tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…